chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 19,685
- 22,694
Kwako Katibu Mkuu wa CHADEMA Ndg John Mnyika.
Mwaka 2015 uligombea ubunge Jimbo la Kibamba, hongera ulifanikiwa kupita kutokana na mawakala waliojitoa kufa kupona kwa ajili yako, wapo waliokataa kuhongwa, wapo walioumizwa na wapinzani wako, na wengine walitaka mpaka kuondolewa Uhai kwa kulinda kura zako na CHADEMA.
CHADEMA Mwaka 2015 mlicheza sana na maslahi ya mawakala wenu, chakula kilikuwa cha kubabaisha sana, mawakala wa vyama vingine waliwahishiwa chakula kwa wakati huku mawakala wenu wakipiga miayo tu, hii siyo sawa kabisa na ni kuwatia majaribuni Mawakala wenu.
Pia posho hamkuwa tiyari kuwalipa, Mnyika unakumbuka vizuri mawakala wako uliwafanya wakakesha pale Ngome mpaka saa sita usiku wakikusubiri wewe ili walipwe posho zao na wakati unajua kabisa ulishashinda bado hukujali mawakala wako ukawalipa elfu 10 TU, na wengine walichoka kukusubiri wakaondoka wenyewe kwa gharama zao bila kupata chochote!
Sasa endelezeni tena huu Uhuni kwenye Uchaguzi huu wa 2020.
Mwaka 2015 uligombea ubunge Jimbo la Kibamba, hongera ulifanikiwa kupita kutokana na mawakala waliojitoa kufa kupona kwa ajili yako, wapo waliokataa kuhongwa, wapo walioumizwa na wapinzani wako, na wengine walitaka mpaka kuondolewa Uhai kwa kulinda kura zako na CHADEMA.
CHADEMA Mwaka 2015 mlicheza sana na maslahi ya mawakala wenu, chakula kilikuwa cha kubabaisha sana, mawakala wa vyama vingine waliwahishiwa chakula kwa wakati huku mawakala wenu wakipiga miayo tu, hii siyo sawa kabisa na ni kuwatia majaribuni Mawakala wenu.
Pia posho hamkuwa tiyari kuwalipa, Mnyika unakumbuka vizuri mawakala wako uliwafanya wakakesha pale Ngome mpaka saa sita usiku wakikusubiri wewe ili walipwe posho zao na wakati unajua kabisa ulishashinda bado hukujali mawakala wako ukawalipa elfu 10 TU, na wengine walichoka kukusubiri wakaondoka wenyewe kwa gharama zao bila kupata chochote!
Sasa endelezeni tena huu Uhuni kwenye Uchaguzi huu wa 2020.