Kijana John Mnyika,
Naomba utueleze una mpango,mikakati gani ya kutatua kero za Wananchi wa Ubungo ikiwa ukishinda Uchaguzi?
Swali la kwanza, jimbo letu linakituo kikubwa na mabasi yanayounganisha jiji na mikoa mingine, je ana mpango gani wa kuhakikisha kwamba mapato yanayopatikana kutokana na kituo hicho sehemu yake pia yanachangia maendeleo ya jimbo letu (kuongeza huduma za kijamii kama vyoo, miundo mbinu ya na kadharika).