John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

Mkuu sikiliza,

Mwigulu tangu wakati anaomba mwongozo na sikusikia maneno ya kusamehe.
Hivyo, thread ile ama mleta mada alikurupuka ama amedhamiria kupotosha kilichoelezwa.
Suala la kuvunja Bunge hilo si mada yangu. Tusirefushe thread kwa kuleta hoja ambazo mngeweza kuanzisha thread nyingine ingekuwa ni efficient step.
kumbuka maneno yako ktika thread no 1
Hivyo, watanzania tuamke tulitizame jambo hili kwa muono huo na si kulalamika kama tumeishiwa hoja. Tunajadili katiba mpya na hivyo kesi kama hizi ni kipimo kwetu kuona kama kweli tunaelewa tunalojadili au la.
Hatuwezi kuendelea kuona Spika akivunja katiba kwa kutoa upendeleo na ubaguzi ambao umekatanzwa na vifungu tele vya katiba yetu. Sasa tujikite wote tulitizame kuwa ni jambo la katiba.
Wabunge wa CHADEMA watumie nafasi yao kulipeleka hili suala Mahakamani maana nis suala la kuvunjwa kwa katiba. Ushahidi upo mwingi tu kuonyesha Bunge ni taasisi inayoendekeza ubaguzi.

Jamaa yangu huenda wewe sio Mbunge lakini km ni Mbunge kwa nini usitoke nje kwamba hukubaliani na yanayoendelea humo ndani na wanaokukubali nao wafuate nyuma
Lakini km Raia wa kawaida usiwachochee wao wakiona hawaelewani watapatana kwa jambo jingine tu, lakini sio kuwadanganya eti Wamshtaki Spika Anne na Naibu Job ili iweje Bunge livunjwe?
Mbona Kikao kikimalizika wanakusanya Posho zao na wanakutana Chako ni chako kwenye kuku, na hakuna anayekataa eti kakandamizwa na kuanza kupigana vikumbo.
Naomba ya Ngoswe muachie Ngoswe wao kukashifiana watajijua sisi tuangalie Bajeti ya leo ya Ardhi wamepitisha suala la WAPANGAJI NA WENYE NYUMBA?
Kumbuka Ndugai keshasema taarifa anazipata katika mitandao ya kijamii wanazitembelea na kuona tunavyodanganyana
Ushauri wa mwisho chukua fomu za kuingia mjengoni na ukamshitaki Spika mm nitakuunga mkono sio humu hata 0.3% ya Watanzania hawatusikii
 
Mkuu nikupateje,

Nimefurahi kuleta thread uliyoijengea hoja na unaomba wachangiaji wapinge kwa hoja,hiki ndo vitu vinatakiwa kwa Great Thinkers ndo maana hata unaona wengi wanapwaya kwa kwenda nje ya hoja yenyewe.

Nikirudi kwenye hoja yako nachokiona kwa wabunge wengi wa CDM bungeni ni kushindwa kukwepa mtego uliopo kwenye kiti cha Spika.Kwani kama kiti cha maamuzi kinayumba usiishie kulalamika kuhusu kuyumba kwa kiti,fanya maamuzi kuonyesha kiti kinayumba kwani hata kiti kina kamati inayokiwajibisha.
Ukianza kupuuzia kuchukua maamuzi mwisho wa siku utakuta unawajibishwa wewe,naamini hili la Mnyika litakuwa somo zuri kwa wabunge wa CDM kuanza kuchukua hatua pale wanapoona kiti kina Double std.
 
kumbuka maneno yako ktika thread no 1
Hivyo, watanzania tuamke tulitizame jambo hili kwa muono huo na si kulalamika kama tumeishiwa hoja. Tunajadili katiba mpya na hivyo kesi kama hizi ni kipimo kwetu kuona kama kweli tunaelewa tunalojadili au la.
Hatuwezi kuendelea kuona Spika akivunja katiba kwa kutoa upendeleo na ubaguzi ambao umekatanzwa na vifungu tele vya katiba yetu. Sasa tujikite wote tulitizame kuwa ni jambo la katiba.
Wabunge wa CHADEMA watumie nafasi yao kulipeleka hili suala Mahakamani maana nis suala la kuvunjwa kwa katiba. Ushahidi upo mwingi tu kuonyesha Bunge ni taasisi inayoendekeza ubaguzi.

Jamaa yangu huenda wewe sio Mbunge lakini km ni Mbunge kwa nini usitoke nje kwamba hukubaliani na yanayoendelea humo ndani na wanaokukubali nao wafuate nyuma
Lakini km Raia wa kawaida usiwachochee wao wakiona hawaelewani watapatana kwa jambo jingine tu, lakini sio kuwadanganya eti Wamshtaki Spika Anne na Naibu Job ili iweje Bunge livunjwe?
Mbona Kikao kikimalizika wanakusanya Posho zao na wanakutana Chako ni chako kwenye kuku, na hakuna anayekataa eti kakandamizwa na kuanza kupigana vikumbo.
Naomba ya Ngoswe muachie Ngoswe wao kukashifiana watajijua sisi tuangalie Bajeti ya leo ya Ardhi wamepitisha suala la WAPANGAJI NA WENYE NYUMBA?
Kumbuka Ndugai keshasema taarifa anazipata katika mitandao ya kijamii wanazitembelea na kuona tunavyodanganyana
Ushauri wa mwisho chukua fomu za kuingia mjengoni na ukamshitaki Spika mm nitakuunga mkono sio humu hata 0.3% ya Watanzania hawatusikii

Mahakama ni kimbilio la kila binadamu anayeishi duniani. NImefurahi kukutana na kichekesho chako kwamba ni uchochezi kumshauri mtu aende mahakamani.

Kichekesho ambacho naamini hata Job Ndugai na Anne Makinda wakikiona ni lazima wacheke.
 
Ni suala la msingi sana,hata leo hii mi sijamwelewe J.Ndugai. Anadai ushahidi haujajitosheleza kwani amejadili na nini? Je,yeye anajua nini kuhusu EPA? Yeye anao ukweli kadiri gani kuhusu EPA na anawaambia nini Watanzania?

Ndugu yangu,
Hili nalo ni bunge au jumba la sanaa? Yaani limekuwa ni mahakama ya ccm dhidi ya Wananchi na CHADEMA.

Theirs are brutally biased, unjust and unlawful practices all perputuated in the name party interests. The kind of interpretations served by Makinda, Ndugai and ilk (i.e. chairpersons) are of some unheard certainties. I happened to conclude that those ambigious laws inspired by convinience are to be dealt with immediately after 2015 elections.

It's a massive shame that abused building has apparently turned into a full-time house of theatre and drama, painfully funded by the national basket.
 
Lakini km Raia wa kawaida usiwachochee wao wakiona hawaelewani watapatana kwa jambo jingine tu, lakini sio kuwadanganya eti Wamshtaki Spika Anne na Naibu Job ili iweje Bunge livunjwe?

Ukwaju,

Ungekuwa umesoma Katiba au Kanuni za Bunge ungeona kwamba kumshitaki au kumuondoa Spika hakusababishi kuvunjwa Bunge, bali kunasababisha wabunge wachague Spika mwingine kuziba nafasi yake.

Wakiziba nafasi yake wanaendelea na utaratibu wake na kama ni Anne Makinda na Job Ndugai wanarudi kwenye viti vya kuomba mwongozo kama uvunjaji wao wa Katiba haukuwaathiri hadi kujiuzuru ubunge ambako nako waliapa kulinda na kutetea katiba.
 
ukweli ni kuwa tuna mhimili mmoja! Rais anaingilia mihimili yote! Makinda kawekwa na Kikwete kila anachofanya remote control kaishika JK! Majaji wote wanateuliwa na JK.
 
Wakuu heshima mbele,
Nakumbuka kama siyo ndani ya Katiba, Kanuni za bunge basi ni sheria flani ambayo inatamka wazi hakuna jambo lolote litakalofanyiwa maamuzi au kutamkwa ndani ya vikao vya bunge litashtakiwa mahakamani. vile vile Mbunge hashtakiwi kwa matamshi yake aliyoyasema akiwa ndani ya Bunge! Kwa msingi huu Mnyika hawezi kwenda mahakamani.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - United Kingdom),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Nikupataje asante sana kwa hoja zako nzuri.
Tatizo kubwa la msingi ndani ya bunge ni sheria na kanuni zenyewe zinazoendeshwa na bunge lenyewe zinaonekana kuwabana zaidi wabunge ktk kutoa hoja kuliko kupanua uhuru zaidi wa kutoa hoja kwahiyo ninachoona mimi kuna haja ya kwenda extra mile kwa kuchambua sheria na kanuni ambazo zinakwamisha bunge kuwa uwanja mzuri wa hoja kwa kutumia mahakama kuzibadili hizi sheria tukianza na hii issue ya mnyika ikienda vizuri basi kuna haja ya kuingia mpaka chumbani.
 
Jamaa yangu mbona umetutoa kwenye utamu unatuleta huku ambako siko (tuanchokifuata ni kweli MWIGULU kamsamehe MNYIKA? basi)
Haya mambo unayoyaleta kabisa hayaingiliani na Mihimili mitatu
Nakuuliza ni nani anayelivunja Bunge na wote wakarudi majimboni kuomba kura upya?
usiwape wasomaji habari za uchochezi, eti waende mahakamani wakashtakiwe Anne na Job
turudishe kwenye mada

Mahakama ni kwa ajili ya kutafuta haki; wakiamua kuwashitaki mahamani kwa kuvunja katiba kama walivyozoea watashitakiwa hata kama mahakama ikiamua vinginevyo kinachoendelea nchini kinajulikana
 
swali kwa nikupataje ??
inakuwaje mnyika aliposema kuwa nchemnba anahusika na issue ya EPA akaambiwa alete ushahidi wakati ndugulile aliposema kuwa waziri amewaonga madiwani akatolewa nje kwa siku tatu?? mbona inaonekana kanuni tofauti zinatumiwa ili ali makosa yanaonekana kufanana?
 
Ndugu zangu wanaJF mwaka jana mwezi january niliweka thread juu ya CHADEMA waende mahakamani kwa aidha kutokubaliana na maamuzi ya Spika pale inapotokea kuona kuna ukandamizaji bungeni,lakini pia nilisema masuala haya EPA yapelekwe mahakamni ili kuweka rekodi sawa na sio kufanya agenda za kisiasa! sasa matatizo kama haya ya Mnyika kulipuka na kushadadia akina mwigulu na kuleta taabu ya kushindwa kutoa ushahidi!
 
Nadhani Wabunge wa CDM watumie mbinu za msituni. Mfano leo, Ndugai aliingia kwenye 18 za Mdee kwa kusema Jimbo la Kawe wamechagua kituko, CDM wangemtaka afute kauli ile ya kuudhi kama Ndugai angepinga basi Mdee au Wabunge wa CDM wangetoka nje kuonyesha kutokuwa na imani na Naibu Spika.
 
Hili swala ndungai kalichukulia kishabiki mno, kwanini?

Kwanza nchembe kuulizia ushahidi wake kwa spika ni kosa maana hapo unakuwa unataka kumfundisha spika na ofisi yake kaze na hata lema alishawah kuulizia ushahidi wake spika akamwambia usinifundishe kazi ila leo haikuwa hivyo kwa job, pili job kaanza kulitolea maamuzi swala ambalo kiti kwa kipindi hicho (muhagama) alishaalipoke na kulifanyia kazi lakini yeye kaanza kutolea majibu swala ambalo siyo yeye aliyeamua mnyika alete ushahidi siku hiyo naadhani kwa haya machache utaona ni kwanini tunasema Sitta alikuwa the best speaker
 
Nadhani Wabunge wa CDM watumie mbinu za msituni. Mfano leo, Ndugai aliingia kwenye 18 za Mdee kwa kusema Jimbo la Kawe wamechagua kituko, CDM wangemtaka afute kauli ile ya kuudhi kama Ndugai angepinga basi Mdee au Wabunge wa CDM wangetoka nje kuonyesha kutokuwa na imani na Naibu Spika.

Ezekiah Wenje ameshamtaka naibu Spika afute kauli yake!
 
swali kwa Nikupataje ??
inakuwaje mnyika aliposema kuwa nchemnba anahusika na issue ya EPA akaambiwa alete ushahidi wakati ndugulile aliposema kuwa waziri amewaonga madiwani akatolewa nje kwa siku tatu?? mbona inaonekana kanuni tofauti zinatumiwa ili ali makosa yanaonekana kufanana?

Sijaelewa ni vigezo gani hutumika na baadhi ya members humu JF ku-address issue au swali kwa mtu mmoja tena kwa kumtaja.
 
Mkuu hapo umenena lakini mahaka zenyewe majaji wameteuliwa na yule dhaifu juzi juzi una fikiri kuna haki hapo?
 
Back
Top Bottom