John Mnyika awataka viongozi wa CHADEMA kuzungumzia kero za wananchi

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,668
15,067
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika amewataka viongozi wa chama hicho mkoani Simiyu kutokaa kimya badala yake wapaze sauti kueleza changamoto zinazowakabili wananchi.

Mnyika ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akizindua Tawi la Chadema Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu huku akisema wajibu wa viongozi wa chama hicho ni kuikumbusha Serikali changamoto zinazowakabili wananchi wake.

"Tunapokabiliwa na matatizo ya kupanda kwa bei za bidhaa na mafuta usafiri na huduma nyingine za msingi zinazowagusa wananchi Chadema tuendelee kuwa sauti ya wananchi ili kutetea haki zao," amesema

Ameongeza; "Tunapokabiliwa na matatizo mbalimbali kwenye bei za pamba na mambo mengine Chadema iwe sauti katika kutetea wananchi. Tufanye majukumu ya chama lakini rai yangu kwenu pamoja na kupambania Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi kazi ya kuwatetea wananchi endeleeni nayo," amesema Mnyika

Mnyika amesema Serikali itachukua hatua zinazoleta mabadiliko kwa jamii iwapo itakumbushwa majukumu yake jambo ambalo litafanikiwa iwapo viongozi hao wakitimiza wajibu wao.

Katibu wa Chadema Kanda ya Victoria, Zakaria Obadi amesema Chama hicho kimeandaa mpango wa kuwakutanisha wanachama wake ili kuwajengea uwezo wa kuwapambania wananchi.

"Tunaendelea kuandaa mpango wa kuwaandaa kuwasemea wananchi na kupaza sauti zenu kwa niaba ya wananchi," amesema Obadi
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika amewataka viongozi wa chama hicho mkoani Simiyu kutokaa kimya badala yake wapaze sauti kueleza changamoto zinazowakabili wananchi.

Mnyika ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akizindua Tawi la Chadema Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu huku akisema wajibu wa viongozi wa chama hicho ni kuikumbusha Serikali changamoto zinazowakabili wananchi wake.

"Tunapokabiliwa na matatizo ya kupanda kwa bei za bidhaa na mafuta usafiri na huduma nyingine za msingi zinazowagusa wananchi Chadema tuendelee kuwa sauti ya wananchi ili kutetea haki zao," amesema

Ameongeza; "Tunapokabiliwa na matatizo mbalimbali kwenye bei za pamba na mambo mengine Chadema iwe sauti katika kutetea wananchi. Tufanye majukumu ya chama lakini rai yangu kwenu pamoja na kupambania Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi kazi ya kuwatetea wananchi endeleeni nayo," amesema Mnyika

Mnyika amesema Serikali itachukua hatua zinazoleta mabadiliko kwa jamii iwapo itakumbushwa majukumu yake jambo ambalo litafanikiwa iwapo viongozi hao wakitimiza wajibu wao.

Katibu wa Chadema Kanda ya Victoria, Zakaria Obadi amesema Chama hicho kimeandaa mpango wa kuwakutanisha wanachama wake ili kuwajengea uwezo wa kuwapambania wananchi.

"Tunaendelea kuandaa mpango wa kuwaandaa kuwasemea wananchi na kupaza sauti zenu kwa niaba ya wananchi," amesema Obadi
Hawa chawa wao kutwa mzima kusema Magufuli utafikiri alikuwa na serikali yake binafsi na kumsifu huyo mamaaa eti ni bora tu kwa sababu wameonja harafu ya dollar
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika amewataka viongozi wa chama hicho mkoani Simiyu kutokaa kimya badala yake wapaze sauti kueleza changamoto zinazowakabili wananchi.

Mnyika ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akizindua Tawi la Chadema Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu huku akisema wajibu wa viongozi wa chama hicho ni kuikumbusha Serikali changamoto zinazowakabili wananchi wake.

"Tunapokabiliwa na matatizo ya kupanda kwa bei za bidhaa na mafuta usafiri na huduma nyingine za msingi zinazowagusa wananchi Chadema tuendelee kuwa sauti ya wananchi ili kutetea haki zao," amesema

Ameongeza; "Tunapokabiliwa na matatizo mbalimbali kwenye bei za pamba na mambo mengine Chadema iwe sauti katika kutetea wananchi. Tufanye majukumu ya chama lakini rai yangu kwenu pamoja na kupambania Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi kazi ya kuwatetea wananchi endeleeni nayo," amesema Mnyika

Mnyika amesema Serikali itachukua hatua zinazoleta mabadiliko kwa jamii iwapo itakumbushwa majukumu yake jambo ambalo litafanikiwa iwapo viongozi hao wakitimiza wajibu wao.

Katibu wa Chadema Kanda ya Victoria, Zakaria Obadi amesema Chama hicho kimeandaa mpango wa kuwakutanisha wanachama wake ili kuwajengea uwezo wa kuwapambania wananchi.

"Tunaendelea kuandaa mpango wa kuwaandaa kuwasemea wananchi na kupaza sauti zenu kwa niaba ya wananchi," amesema Obadi
Etwege tulikuonya kwamba iko siku utaisifu Chadema , umeona sasa ?
 
Back
Top Bottom