diwani ubungo
New Member
- Sep 14, 2012
- 4
- 2
Leo ilikuwa vifijo na nderemo kwa wakazi wanaoishi kata ya Makuburi na Ubungo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika maeneo ya Riverside, baada ya Mnyika kuwapa taarifa kwa upande wa Makuburi kuwa fidia ya wakazi waishio kwenye nyumba tatu pembeni ya mto gide kuwa imeshalipwa na wamepewa notisi ya siku 60 kupisha ujenzi wa barabara ya kwenda Makoka na ikiwa imeshatengewa kiasi cha shilingi milioni 110 soon baada ya nyumba hizo kuvunjwa.
Kwa upande wa wakazi wa kata ya Ubungo barabara inayounganisha barabara ya Mandela na Maziwa Road imeshapata mkandarasi wa kujenga kwa kiwango cha rami pamoja na daraja la double road, ikiwa na mafanikio ya kuibana TANROADS pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.
Kwa upande wa wakazi wa kata ya Ubungo barabara inayounganisha barabara ya Mandela na Maziwa Road imeshapata mkandarasi wa kujenga kwa kiwango cha rami pamoja na daraja la double road, ikiwa na mafanikio ya kuibana TANROADS pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.