Waziri John Magufuli hili la kuvunja jengo la TANESCO Ubungo tumia busara

Nakumbuka msemo wa kikwetu usemao "...Ukimsifu mgema tembo hulitia maji...! Magufuli amesema yale majumba ya shirika la umeme yanayoleta mandhari ya aina yake hapa jijini yaliyojengwa kwa mabilioni ya shilingi ni lazima yavunjwe eti yamejengwa kwenye sehemu iliyohifadhiwa kwa ajili ya kupita barabara.

Huyu mtu kama hana wazimu atakuwa na kitu gani hivi anafikiria hela iliyotumika ni hela ya serikali, ? Au ya shirika la umeme ,akili za watu wengine zinakuwa za ajabu ajabu ,anachotaka ni kuwapa tanesco eneo jingine wajenge upya ,kwa maana kwa dau hilo hela ingine itapatikana na wajanja kupata chao.

Mtu huyu alikuwa wapi wakati majumba hayo yakijengwa ?Serikali ilikuwa wapi ?
Tanescobuild.jpg
Unaenda kuvunja mijumba hiyo kwenye nchi ambayo uchumi wake ni wa kubahatisha au wakuu mnataka na kutafuta njia mbadala ya kufanya ufisadi,
Mwiba, amini nakuambia wewe ndio unawazimu!.
Unajisikiaje kuitwa 'Mwiba una wazimu!', hizi lugha nyingine, sio za kutumia!, Magufuli ni waziri halali wa JMT wewe unamuita anawazimu, sio tuu unataka kumshushia hadhi, bali pia unaidharaulisha JF.

Unataka kuithaminisha sheria na fedha?. Eneo lile inajengwa fly over, hebu kwa akili piga kila hesabu hiyo fly over ichepushiwe wapi?.
Sio jengo tuu la Tanesco pale, majengo yote kuzunguka pale yanaondoka, na kama CCM watamsimamisha Magufuli 2015, tutamshauri Dr, asipoteze muda!, maana akishinda, mtu wa kanza kumpandisha kizimbani ni JK!,
 
Mwiba, amini nakuambia wewe ndio unawazimu!.
Unajisikiaje kuitwa 'Mwiba una wazimu!', hizi lugha nyingine, sio za kutumia!, Magufuli ni waziri halali wa JMT wewe unamuita anawazimu, sio tuu unataka kumshushia hadhi, bali pia unaidharaulisha JF.

Unataka kuithaminisha sheria na fedha?. Eneo lile inajengwa fly over, hebu kwa akili piga kila hesabu hiyo fly over ichepushiwe wapi?.
Sio jengo tuu la Tanesco pale, majengo yote kuzunguka pale yanaondoka, na kama CCM watamsimamisha Magufuli 2010, tutamshauri Dr, asipoteze muda!, maana akishinda, mtu wa kanza kumpandisha kizimbani ni JK!,

Wewe unahitaji kupata mwalimu wa saikolojia na akakufundisha somo la wazimu,nafikiria pia hujui kama kuna somo la aina hiyo ,ndgu wazimu upo wa aina nyingi sana,maana hata kuchana nywele kwa mastyle basi hapo ujue kuna wazimu wacha kufunga vifungo kimoja au kuweka shati fundo. Na hapo hata papite mafly over bado huo utakuwa ni ufisadi,Na mhusika anahusika na kupata faida haiwezekani kwa nchi masikini kuvunjavunja hovyohovyo,kama si wazimu ni kitu gani?
 
Nimekuelewa kwa kina ila jibu langu limekupita.
Huwezi kusema sheria imevunjwa wakati kwa kujengwa Jumba hilo ,bia ya shaka yeyote ile hizo landmark za zinjia au hiyo master plan ilikuwepo kabla ya jumba hilo au sio ? Kama ni hivyo majengo hayo ni lazima yapitie katika idara kwa kupasishwa na kama kuna kizingiti chochote kile ,ujengaji huwa hauruhusiwi ,kumbuka tu aliejenga hapo si mwananchi anaekaa karibu na mipaka ya njia badala ya kuona kwa muda mrefu barabara haijajengwa akaamua kujenga,pengine na alama za upitishaji njia akazing'oa,majumba hayo yamejengwa kwa baraka zote za serikali iliopo madarakani,iweje leo hukohumo ndani ya serikali azuke mtu aseme ni lazima majumba hayo yavunjwe? Hivi serikali yeti ina uwezo gani wa kuyafanya hayo yote ?

Mkuu Mwiba, nashukuru kwa majibu yako unayoamini kwamba yamenipita!

Hata hivyo nasikitika kukuarifu kwamba hujajibu swali langu kwa sababu hujalielewa.

Hebu jaribu hili labda utabahatisha. Yale magorofa yaliyovunjwa pale masaki yaliyokuwa na kibali cha manispaa ya kinondoni yalikuwa ya gharama ya shilingi ngapi? Kwa nini yalivunjwa?
 
Sanity must prevail. We cannot allow shambolic construction that flouts the basic city plans or that which impedes future infrastructural development ust because such buildings beautify the city. Magufuli you are right brother, keep it up!
 
Magufuli alichosimamia ni kizuri sana mi nimefurahi sana kwa kauli yake kwa sababu inaashiria kuwa mchezo wa kudharau sheria kuanzia sasa si mzuri maana madhara yake ni makubwa sana kiuchumi. Kuna watu leo hii wanauziwa mashamba ya mananasi na mikorosho na kuyageuza viwanja bila kupata baraka za wizara husika. Yaani mipango miji ni sifuri, sasa tujifunze kutokanana makosa.

Hata hivyo, kwa kuwa majengo yale yamejengwa kwa gharama za walipa kodi cha kufanya sasa ni kuwashitaki wale wote walizembea katika kutekelewa wajibu wao wakati wa ujenzi huo bila ya kuangalia sura wala chama anachotoka. Then Majengo hayo tuya reserve kwa kigezo hicho kwani tunaweza kufanya mbadala wa kupanua barabara ubungo kwa kujenga flyovers na ku abandon mataa yale, then barabara ipanuliwe kuanzia eneo la Rombo ambapo flyovers hizo zitaishia, magari yote yanayoenda magomeni yanapita chini kama kawaida na yale yanayoelekea TAZARA ama MWENGE yanaanza kupanda juu from Rombo ambapo barabara itaanza kupanuka taratibu kuelekea Chalinze. kwa upande wa kutokea magomeni yanaanza kupanda juu kuanzi stend ya mikoani

Kwenye design ya hilo hakuna shida shida inakuwa kama Blah blah blah zitaingiwa badala ya kuwaachia wataalam wafanye kazi yao.
 
Mkuu Mwiba, nashukuru kwa majibu yako unayoamini kwamba yamenipita!

Hata hivyo nasikitika kukuarifu kwamba hujajibu swali langu kwa sababu hujalielewa.

Hebu jaribu hili labda utabahatisha. Yale magorofa yaliyovunjwa pale masaki yaliyokuwa na kibali cha manispaa ya kinondoni yalikuwa ya gharama ya shilingi ngapi? Kwa nini yalivunjwa?

Sasa huoni kama hapo wendawazimu wameongezeka,inakuwajekuwaje serikali inajenga majumba ya bei mbaya halafu inayavunja ? Kwa kisingizio cha kupita njia,kwanza si wangezijenga hizi njia zilizojaa mashimo na kutuwekea taa za barabarani ,zinazowaka? Huoni kama huo ni ubadhirifu na hakuna wa kuusemea na kuukemea na kuwawajibisha wahusika ? Mwengine anaiba hela anajenga jumba kubwa la danganya toto ,mwengine anachota hela analivunja jumba hilo ,huoni kama something wrong ?
 
Kama akivunja kweli sitamuona kua ana wazimu ispokua nitamuaona kua hakutumia hekima. Kwa kuangalia public interests sidhani kua kufanya hivyo na hali ya uchumi ya nchi ilivyo hivi sasa, kutakua na maslahi kwa jamii. Ningemuunga mkono sana kama yangekua ni majumba ya mtu binafsi kwani sana kungekua na mazingira ya rushwa, ambapo kwa kufanya hivyo angekua ametuma very strong message kwa waliohusika.

Ni vyema akawawajibisha wote waliohusika ktk ujengaji huo na akatafuta ufumbuzi mwengine ambao utafanikisha zoezi hilo la barabara kama kupindishwa barabara na mengineyo, lakin sio kuvunja, itakua ni kuanza nyuma sana na gharama za maisha ndio zinatupunga mkono.
 
mamlaka za serikali hazina coordination? kuna majengo ya mwaka 54 ya serikali yana mkasi!
 
kupindishwa kuliko kulitia hasara Taifa, Kama Makufuli anataka kuyavunja hayo majumba basi ni lazima afanye uchunguzi na kulijulisha Taifa ilikwendakwendaje hata majumba hayo ikawezekana kujengwa hapo ili hao wahusika walipe gharama za majengo hayo na gharama za uvunjaji,hii sio nchi ya Magufuli peke yake ,afanye kila kitu vile aonavyo yeye
sio kazi ya magufuli kujua ilikuaje majengo haya yakajengwa hapo yalipo!kazi yake ni kuangalia standards za barabara na maeneo yake zinazingatiwa.nakubaliana na wewe kwamba magufuli asifanye nchi kama ya baba yake hii haimaanishi sheria zinapokiukwa akae kimya kisa gharama kubwa zilitumika kuvunja hiyo sheria.

"Kutokujua sheria sio kinga ya kuhukumiwa"
 
hilo jengo halifiki thamani ya barabara itakayojengwa jaribu kufikiria tunapoteza kiasi gani kwa siku kwa foleni zisizo na tija! na kadiria shughuli za kiuchumi ngapi zitarahisishwa kwa kujenga barabara itakayoweza kuondoa foleni?
 
Wewe unahitaji kupata mwalimu wa saikolojia na akakufundisha somo la wazimu,nafikiria pia hujui kama kuna somo la aina hiyo ,ndgu wazimu upo wa aina nyingi sana,maana hata kuchana nywele kwa mastyle basi hapo ujue kuna wazimu wacha kufunga vifungo kimoja au kuweka shati fundo. Na hapo hata papite mafly over bado huo utakuwa ni ufisadi,Na mhusika anahusika na kupata faida haiwezekani kwa nchi masikini kuvunjavunja hovyohovyo,kama si wazimu ni kitu gani?

kama nchi imejengwa hovyohovyo itahitaji kubomolewa bila kujali aliyejenga!
 
sio kazi ya magufuli kujua ilikuaje majengo haya yakajengwa hapo yalipo!kazi yake ni kuangalia standards za barabara na maeneo yake zinazingatiwa.nakubaliana na wewe kwamba magufuli asifanye nchi kama ya baba yake hii haimaanishi sheria zinapokiukwa akae kimya kisa gharama kubwa zilitumika kuvunja hiyo sheria.

"Kutokujua sheria sio kinga ya kuhukumiwa"

Inawezekana hatufahamiani,tatizo hapa sio kuvunjwa ,nilipo ni utumiaji mbaya wa mamlaka kwa waliopo serikalini,hapa kuna mtu anajifanya ni dictator ,huyu jamaa hakuanza leo au jana kuvnjavunja ,tokea huko mwanzo anahistoria ya aina hii ya ubabe mnakumbuka kesi ya samaki,hata sijui imeishia wapi au ameshakatiwa chake.

Sasa inaposemwa serikali inajenga halafu inabomoa ,hivi utaielewaje serikali hiyo ? Wanaojenga na kubomowa wote wamo serikalini,vibali vya ujenzi vyote vinapatikana huko,sidhani kama Tanesco ilikurupuka na kujiamulia kujenga hapo hasa ukizingatia ni chombo cha serikali,mkisikia watu wanavunja msifikirie wanakurupuka kama anavyokurupuka Magufuli.

Majumba haya ya magorofa yana muda wake na ukifikia inabidi yavunjwe ,sasa hayo majumba sijui kama muheshimiwa anajua muda wake ni miaka mingapi ? Barabara inaweza kujengwa iwapo majumba hayo yatakuwa yameshafikiwa muda wake,ila hizo sio niliokusudia.

Unaposema kuwa sheria imekiukwa ,wananchi wanaweza kukiuka sheria lakini sio serikali inayofuata misingi ya sheria kama unavyodai au kutaka kumuonyesha Magufuli kuwa anafuata sheria za nchi itakuwa huitendei haki jamii ya walipa kodi.

Magufuli kama Waziri husika alikuwa achunguze (sijui kama amefanya hivyo na kutoa kauli),alijulishe Taifa baada ya kugundua kuwa majumba hayo yalijengwa kinyume cha sheria na kwa kuwa ni mali ya Taifa hili sheria kama unavyosema ifuate mkondo wake .
 
kama nchi imejengwa hovyohovyo itahitaji kubomolewa bila kujali aliyejenga!
Ndugu kuna watu wanavunjiwa nyumba bila ya kulipwa ,hio sio haki,watu wanauliza tulipokuwa tukijenga mlikuwa wapi.kwa maana hii wahusika wanaovunja vunja na kutoa vibali vya ujengaji hawana maispector wanaopita pita na kuangalia hali ya mazingira na plan za mji kama wapo watakuwa wanapokea rushwa,weka kando hayo.
Magufuli anataka kutoa kafara majumba hayo ili kuhalalisha uvunjaji wa nyumba za walala hoi bila ya kuwalipa kwa kigezo kama hicho kuwa hata majumba ya serikali yamevunjwa itakuwaje mengine yasivunjwe.
 
Kama hilo jumba ni la mtu binafsi hakuna tabu kwani itakuwa ametoa rushwa ili kupata kibali cha ujenzi na haswa ilivyokuwa kuna uhakika wa kutotakiwa majumba marefu,haya majumba ya Tanesco sidhani kama kutakuwa na rushwa zaidi ya ufisadi na kuyavunja na bila ya shaka kutahitajiwa kujengwa tena sehemu nyingine ,hiyo hela hapo ni ya walipa kodi ,Tanzania ni kubwa sana na bara bara na future plan inawezekana kupindishwa kuliko kulitia hasara Taifa, Kama Makufuli anataka kuyavunja hayo majumba basi ni lazima afanye uchunguzi na kulijulisha Taifa ilikwendakwendaje hata majumba hayo ikawezekana kujengwa hapo ili hao wahusika walipe gharama za majengo hayo na gharama za uvunjaji,hii sio nchi ya Magufuli peke yake ,afanye kila kitu vile aonavyo yeye,hilo haliwezekani ,ila ikiwa yeye anamiliki kampuni za uvunjaji majumba,sasa napata wasiwasi kuwa kampuni za kuvunja majumba ni za kwake au hela inayotumika kuvunja majumba na yeye anachota zake na kuwalipa matingatinga hela ya chai.

Serikali kutumia pesa za walipa kodi katika kutenda haki ni jambo la kawaida tu. Ndio maana pesa zinatumika kuwalipa akina Mkono na mawakili mbambali, na kuhudumia shughuli za mahakama. Yote hiyo ni kutenda haki. Haki mbele ya sheria. Sasa kama unataka jengo la TANESCO lisibomolewe kwasababu ni hela za walipa kodi, je haki itatendeka? Itakuwaje kwa raia wengine wa kawaida wenye vibanda vyao waliovunja sheria kwa kujenga kwenye road reserve? Na hata hizo hela za walipa kodi unazozitetea zisitumike katika suala hili, zisipotumika, zitakufikiaje wewe na wananchi wengine? Zitaliwa tu.

Jambo lingine unatakiwa kulijua ni kuwa nchi hii imeoza kwa kiwango kikubwa. Usifikiri kwa vile ni jengo la TANESCO basi ujenzi wake kwenye eneo la barabara haukuwa na rushwa hata kidogo. Inawezekana kabisa Rushwa ilitembea kwa njia ile ile ambayo mwananchi wa kawaida kule msasani aliitumia. Inawezekana kabisa, TANESCO walitoa rushwa ili wajenge pale kwa vile kujenga pale kuli-facilitate ulaji kwa namna moja au nyingine, ulaji ambao labda usingekuwa mkubwa kama wangejenga eneo lingine..

Bottom line: jengo lipo eneo la barabara, linatakiwa kuvunjwa kama ambavyo wananchi maskini watavunjiwa vibanda/nyumba zao walizojenda kwenye road reserve.
 
wameamua badala ya kuweka nguzo za umeme waweke sehemu ya ofisi yao ili kurahisisha public service,[/COLOR][/B]
sasa kila taasisi ikijiamulia kubadilisha matumizi ya ardhi bila kuzingatia ushauri wa kitaalamu kutakalika hapa Tz?basi tuseme magufuli kajiamulia kupitisha barabara pale Tanesco kwa nini mnamuona ana wazimu.
 
Thamani ya barabara haiwezi linganishwa na jengo lolote lile hapa mjini. Kama hili jengo lipo ndani ya hifadhi ya barabara basi libomolewe na Magufuli yupo sahihi kabisa. Lazima sheria ziheshimiwe vinginevyo ipo siku tutasema tusiwafunge matariji kwasababu wakifungwa uchumi wa nchi utayumba.

1) Hivi mnajua ni hasara kiasi gani taifa linapata kwa magari kukaa foleni hapo barabarani?
2) Hivi mnajua wananchi wanateseka na kupoteza muda mwingi wa kuzalisha kwa kukaa foleni barabarani
3) hivi unajua ubungo ndio lango kuu la kuingia jijini?
Jengo hili linathamani ndogo sana ukilinganisha na hasara taifa linalopata na mateso kwa raia kutokana na foleni na msongamano wa magari. Magufuli kazi buti ondoa uchafu huo wa Tanesco.
 
Nakumbuka msemo wa kikwetu usemao "...Ukimsifu mgema tembo hulitia maji...! Magufuli amesema yale majumba ya shirika la umeme yanayoleta mandhari ya aina yake hapa jijini yaliyojengwa kwa mabilioni ya shilingi ni lazima yavunjwe eti yamejengwa kwenye sehemu iliyohifadhiwa kwa ajili ya kupita barabara.

Huyu mtu kama hana wazimu atakuwa na kitu gani hivi anafikiria hela iliyotumika ni hela ya serikali, ? Au ya shirika la umeme ,akili za watu wengine zinakuwa za ajabu ajabu ,anachotaka ni kuwapa tanesco eneo jingine wajenge upya ,kwa maana kwa dau hilo hela ingine itapatikana na wajanja kupata chao.

Mtu huyu alikuwa wapi wakati majumba hayo yakijengwa ?Serikali ilikuwa wapi ?
Tanescobuild.jpg
Unaenda kuvunja mijumba hiyo kwenye nchi ambayo uchumi wake ni wa kubahatisha au wakuu mnataka na kutafuta njia mbadala ya kufanya ufisadi,

Sio kwa majumba yaliyojengwa kwa fedha ya wananchi.Tena majumba yenyewe yanajionyesha ni ya bei au gharama kubwa sana. Unaweza kufanya quantity survey hapo au just estimation ni shilingi ngapi za kiTanzania zilitumika.
Inawezekana CCM wapo kwenye mikakati ya kuipa shida serikali itakayokuja badala yao.

Akivunja hili jengo nitamwona punguani!
Kuna tatizo gani hiyo barabara ikikwepeswa? Kama ana ubavu Ajenge ipite chini au juu. kama ni lazima ipite hapo.

Huyu jamaa ana wazimu sio kidogo, hao wazembe wa serikali waliopitisha ujenzi wa hilo jengo wako wapi? Wamechukuliwa hatua gani?

Au kwakuwa hayo majengo yamejengwa na kodi ya mwananchi basi inakuwa ni rahisi kuyavunja? Akavunje nyumba zake huko chato na dar..hili swala ni zito sana,badala ya serikali kufikiria maendeleo ya kujenga flyover eti wao wanafikiria kuvunja! Nasema siku atakapoamua kuvunja lile jengo kwa huo wazifa wake wa muda,atakuja kujutia maisha yake yote..I mean it.

Hifadhi ya Barabara ni kwa sababu ya public services and utilities ikiwema; umeme, maji, simu, internet, mobile toilets, e.t.c. Jengo la TANESCO ni public services kwa maana kwamba wameamua badala ya kuweka nguzo za umeme waweke sehemu ya ofisi yao ili kurahisisha public service, sasa mzee Pombe atuambia anataka kuondoa public service and utilities ili public ipate wapi huduma?

Nimekuelewa kwa kina ila jibu langu limekupita.
Huwezi kusema sheria imevunjwa wakati kwa kujengwa Jumba hilo ,bia ya shaka yeyote ile hizo landmark za zinjia au hiyo master plan ilikuwepo kabla ya jumba hilo au sio ? Kama ni hivyo majengo hayo ni lazima yapitie katika idara kwa kupasishwa na kama kuna kizingiti chochote kile ,ujengaji huwa hauruhusiwi ,kumbuka tu aliejenga hapo si mwananchi anaekaa karibu na mipaka ya njia badala ya kuona kwa muda mrefu barabara haijajengwa akaamua kujenga,pengine na alama za upitishaji njia akazing'oa,majumba hayo yamejengwa kwa baraka zote za serikali iliopo madarakani,iweje leo hukohumo ndani ya serikali azuke mtu aseme ni lazima majumba hayo yavunjwe? Hivi serikali yeti ina uwezo gani wa kuyafanya hayo yote ?

Huyu jamaa anatakiwa ku focus attention yake kwenye kujenga barabara. Badala yake sasa ana focus attention yake yote kwenye kubomoa majengo ambayo yamekuwepo hapo kwa zaidi ya miaka kumi sasa. Huu ni wenda wazimu!

Nakubaliana kwamba ni uendawazimu kubomoa majumba ya gharama kubwa kama lile la Tanesco Ubungo, eti kwa sababu tunataka barabara inyooke. Hata kama majumba hayo yanamilikiwa na watu binafsi, ni hasara kwa taifa kwani yakijengwa mengine gharama za ujenzi zitaongezeka na sisi wananchi tuta-suffer. Mengi ya haya majengo yaliidhinishwa na Serikali hii hii.

Huku kukurupuka kwa Magufuli na mawaziri wengine wa aina yake, kunadhoofisha uchumi wetu. Hivi Baraza la Mawaziri halijadili mambo kama haya ambayo yanaweza kuongeza gharama kwa taifa?

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mustapha Mkullo ana jukumu la kuhakikisha mipango ya Serikali inatekelezwa kwa namna ya kutokuongeza mzigo usio wa lazima kwa walipa kodi. Tunaomba uwadhibiti wenda wazimu kama Magufuli.

Muuliza hii hoja ungeuliza swali ungejibiwa vizuri sana na kupata elimu ya bure, kwa kifupi

1. Thamani ya barabara itakayopita pale hata iwe ni lane moja thamani yake ni kubwa dynamically mara nyingi sana zaidi ya any standing structures!

2. Ukifocus miaka 50 au 100 ijayo we need six lanes or 8 lanes highways....

Ningekueleza in details whay that building is chaos! siyo Magufuli ni wataalamu, tatizo kubwa ni kuwa masterplan za mji zinachakachuliwa kila siku na siasa inatawala na wanasiasa hao ni kama nyie!

mwanafunzi wa certificate NIT au diploma ya civil engineering DIT, MIST au Arsuha tech wanajua vyema kabisa , achilia mbali watu wa degree ya kwanza mlimani au URP ardhi institut

This is common practise even in developed world especially USA where they have even specialised contractors for demolition!

Try to search in your google you will be amazed

Guys learn to look things in different direction hii ni aibu kubwa !! STOP!
 
Thamani ya barabara haiwezi linganishwa na jengo lolote lile hapa mjini. Kama hili jengo lipo ndani ya hifadhi ya barabara basi libomolewe na Magufuli yupo sahihi kabisa. Lazima sheria ziheshimiwe vinginevyo ipo siku tutasema tusiwafunge matariji kwasababu wakifungwa uchumi wa nchi utayumba.

1) Hivi mnajua ni hasara kiasi gani taifa linapata kwa magari kukaa foleni hapo barabarani?
2) Hivi mnajua wananchi wanateseka na kupoteza muda mwingi wa kuzalisha kwa kukaa foleni barabarani
3) hivi unajua ubungo ndio lango kuu la kuingia jijini?
Jengo hili linathamani ndogo sana ukilinganisha na hasara taifa linalopata na mateso kwa raia kutokana na foleni na msongamano wa magari. Magufuli kazi buti ondoa uchafu huo wa Tanesco.

Thanks brother!! kula tano!
 
Ndugu kuna watu wanavunjiwa nyumba bila ya kulipwa ,hio sio haki,watu wanauliza tulipokuwa tukijenga mlikuwa wapi.kwa maana hii wahusika wanaovunja vunja na kutoa vibali vya ujengaji hawana maispector wanaopita pita na kuangalia hali ya mazingira na plan za mji kama wapo watakuwa wanapokea rushwa,weka kando hayo.
Magufuli anataka kutoa kafara majumba hayo ili kuhalalisha uvunjaji wa nyumba za walala hoi bila ya kuwalipa kwa kigezo kama hicho kuwa hata majumba ya serikali yamevunjwa itakuwaje mengine yasivunjwe.

haki lazima iwe na ukomo,haki lazima izingatie sheria.
Basi mimi nina mpango wa kujenga hospitali kwenye mataa ya ubungo ili nisaidie abiria wa maeneo yale.vipi maoni yako kuhusu hili?
Usichukulie makosa na ufisadi uliofanywa na wazembe wachache ndio mwenendo wa maisha yetu.
 
Strategically, kama majengo hayo yamo ndani ya eneo la barabara ni lazima yabomolewe.

Kabla ya kumwona Magufuli hana akili ni lazima wote mnaopinga uamuzi wa Magufuli kujiuliza maswali.

Hivi ni nani aliyeamuru ujenzi wa majengo haya ya mabilioni bila kukaa chini na kupanga kila kitu kikamilifu??
Master plan ionyeshayo eneo la Barabara ilichorwa mwaka gani?
Kama Master plan ilikuwepo kabla ya ujenzi wa barabara ni kwa nini Tanesco iliendelea na ujenzi katika eneo la barbara? Ni kwa nini serikali haikuizuia Tanesci kujenga akatika eneo la barbara?

Eneo la Ubungo ni Entrence na Exit kuu ya jiji la Dar, kama kwa namna yeyote ile majengo hayo yamo ndani ya eneo la barabara ni lazima yabomolewe kupisha upanuzi wowote wa barabara uiliopangwa hapo awali. Comparatively thamani ya majengo hayo ni ndogo sana ukilinganisha na hasara itakayosababishwa ya kuzuia upanuzi wa barabara.


Kama kwa akili zenu mnamuona Magufuli ni Punguani kwa kushikiria msimamo wake wa kubomoa majengo yote yaliyomo katika eneo la barabara! Mnamuonaje na mtamwita jina gani mtu aliyeng'ang'ania kujenga majengo ya thamani kubwa katika eneo la barabara?

Kulikuwa na Busara gani kujenga majengo hayo ndani yana eneo la barabara??

Ni nani aliyekuwa Waziri wa wizara husika wakati wa ujenzi huo?? Na ninani aliyekuwa Bosi wa Tanesco wakati huo??

Serikali ya CCM ilikuwa wapi na mastar plan yake wakati Tanesco wakijenga katika eneo la barabara??

Kipimo na Ujinga,Upunguani Uhuni na Utovu wa Nidhanmu Tanzania ni nini??

Magufuli ni Punguani, aliyesimama kidete kujenga katika eneo la barabara tutamwitaje??

Madela; You are right...!

To see what is wrong and take action about it is to be right on what is wrong!

Magufuli hajafanya kosa lolote!

Labda mlalamikaji aombe kupunguziwa hukumu...lakini Magufuli hajakosea lolote..

Ukubwa wa gharama kwenye kutenda kosa ..hakufanyi kosa lisiwe kosa.... Magufuli yuko sahihi..

...Jumba lazima livunjwe huo ndio mtizamo sahihi....

Kama ni complain ya kuomba msamaha dhidi ya kosa hilo ni jambo lingine...na hiyo haifanyi Magufuli kuonekana kakosea ...bado yuko sahihi!!

Labda mlalamikaji aombe kupunguziwa hukumu...lakini Magufuli hajakosea lolote..!!
 
Back
Top Bottom