John Magufuli ni mweupe kwelikweli, sijui huo urais aliwaza nini kugombea!

Ondoa Mahaba yako ili uweze kuuona utendaji wa Magufuli

Ww ndio uondoe mahaba yako kwa magufuli ili uuone uozo wa magufuli. 90% ya niliyosema yapo kwenye report ya CAG ambaye ni mteule wa rais. So niliyocomment serikali ya kikwete inayafahamu fika na kwa sbb zao binafsi wameyakalia.

Kwenye mustakabali wa nchi ni nzr wote tukawa objective.
 
CCM usanii umewaponza
Mnasema mawaziri wakuu hawakuleta maendeleo lakini hamsemi waziri wenu mkuu ataletaje maendeleo, mnasema kitu kimefanyika kwenye awamu ya mkapa na awamu ya kikwete lakini hapo hapo mnasema mawaziri wakuu na mshauri wa raisi kwa awamu zote hizo ni mafisadi na waliwarudisha nyuma
Kwa nini tu msiseme ukweli kuwa sera zenu zina matatizo? Hakuna atayeweza kutukwamua kiuchumi ndani ya sera zenu ameshindwa sumaye na mkapa, ameshindwa mwinyi , ameshindwa kikwete na pinda ...hakuna atayeweza full stop!!


Sasa mmkalia uongo tu, na unafiki wa kushangaa elimu bure hadi chuo kikuu wakati mkishangilia elimu bure hadi form four!!!! Hivi kati ya wanafunzi wanaomaliza form four wanafunzi wanaokwenda form five nchi nzima ni wangapi na wangapi wanaenda vyuoni, kama mtu anaweza kufanya elimu bure hadi form four anashindwa nini kuifanya bure hadi chuo kikuu??

Ati mtakamata mafisadi, kwani kinachowafanya msiwakamate sasa hivi nini? Mahakama hizihizi mbona zilimfunga Yona na Mramba? Mbona Hao mafisadi mmnaokula nao sahani moja mnawanadi kwenye ubunge??

Lowasa sio fisadi, kama angekuwa fisadi mngekuwa mmeshamsweka jela alipo hamia ukawa kwa jinsi mbavyomchukia

Tunataka mabadiliko ya sera na katiba, hayo ndiyo mabadiliko ya kweli na yeyote anayetusapoti kwa hilo tunamsapoti hatutaki mabadiliko ya sura kumtoa kikwete na kumuweka magufuli wakati kila kitu kipo palepale!

Sera za kuiweka nchi kwenye umaskini, ufisadi, mikopo na kuomba omba mwisho keshokutwa!!!!

I cant agree more mkuu.

Hv mkapa kwa mfano lets b very honest, unakuwa na waziri mkuu mzigo unakaa naye miaka kumi na kumsifu kwamba ni mtendaji. Ghafla anahama chama unaanza kumponda then unataka tukuamini kweli? Tunaweza kuwa malofa lakini si kwa kiwango hicho mzee!
 
Ndio tayari kasha kuwa Rais sasa, anaijenga Tanzania ya wanyonge.

mafisadi hayana rangi
 
Kiukweli ni bora Kikwete 'dhaifu' kuliko Magufuli mkurupukaji.
Huyu jamaa akipewa nchi hata mwezi mmoja tu atasababisha vita.
Tuchukulie mfano wa mgogoro wa ziwa Nyasa kati yetu na Malawi Magufuli ndio angekuwa rais ingekuwaje?
Tuache ushabiki,Magufuli hafai kuwa rais.
Yaliyonenwaaa sasaa
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya manager, boss na Leader. Hii nchi inahitaji leader.
 
Dikteta haimanishi kufanya maamuzi kabla ya kufanya uchambuzi wa kutosha.

Tofauti kati ya Mgufuli na Lowasa ni kwamba Lowasa anaongea jambo baada ya kulifanyia analysis lkn Magufuli Anaongea ndipo anafanya analysis.
Mkuu uliyaona mapema haya...
 
Mkuu kuna makaburi mengine ni lazima tu yafukuliwe mara kwa mara ili tusisahau yaliyojiri mbali mbali kuhusu huyu dhalimu dikteta uchwara.

Haha Mkuu unefukua kaburi..huu Uzi ni valid sana aisee..jamaa aliniona mbali..too bad mtoa mada alim"Kaanga" Dr Fenela..no wonder akakatwa kwenye ubunge EAC..!
 
Kasi kwenye kufanya lipi lenye maslahi kwa Watanzania. Kudharau katiba, Bunge, mahakama, sheria za nchi, wizi wa kuchota pesa hazina bila idhini ya Bunge!?

Bado Magufuli anastahili pongezi kubwa, amekwenda kwa kasi ambayo haijawahi kutokea.
 
Kasi kwenye kufanya lipi lenye maslahi kwa Watanzania. Kudharau katiba, Bunge, mahakama, sheria za nchi, wizi wa kuchota pesa hazina bila idhini ya Bunge!?
Umesikia fisiem kuunga mkono juhudi za rahisi wa kunyonga wanyonge wamejenga kiwanda cha kununua wabunge, madiwani wa upinzani?

Pia ulisikia amewajengea watoto wa wanyonge hosteli aka makaburi?

Link Hosteli za Magufuli chuoni UDSM zimeanza kubomoka. Nini chanzo? Watoto wetu watapona?

Link 2. Hosteli za Magufuli chuoni UDSM zimeanza kubomoka. Nini chanzo? Watoto wetu watapona?

Link3. Zitto: Tuliambiwa hostel za UDSM zimejengwa kwa bil 10 ila ripoti ya CAG inasema zimejengwa kwa bil 54. Uwongo! Uwongo!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mafisiem yanapongeza tu Mkuu! Yanachojali haya mafisiem ni matumbo yao Mkuu na si maslahi ya Tanzania na Watanzania.

Umesikia fisiem kuunga juhudi za rahisi wa kunyonga wanyonge wamejenga kiwanda cha kununua wabunge, madiwani wa upinzani?

Pia ulisikia amewajengea watoto wa wanyonge hosteli aka makaburi?

Link Hosteli za Magufuli chuoni UDSM zimeanza kubomoka. Nini chanzo? Watoto wetu watapona?

Link Zitto: Tuliambiwa hostel za UDSM zimejengwa kwa bil 10 ila ripoti ya CAG inasema zimejengwa kwa bil 54. Uwongo! Uwongo!
 
Naomba nieleweke kuwa ni kweli pasipo shaka kabisa John Magufuli mgombea urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia CCM ana upeo mdogo sana wa kuchanganua mambo! Hajui kitu kinachoitwa kanuni za utawala bora!

Jana nimemsikia akisema eti yule mtu mwenye ghorofa aliyezuia bomba la maji lisipite angekuwa yeye ndiye mwenye mamlaka angemvunjia kwa nguvu! Huyu ndiye mtu anayepigiwa chapuo kuwa rais wa nchi!

Bomba unataka upitishe kwenye nyumba ya mtu kimabavu tu eti kwa kuwa una mamlaka? Nini maana ya mahakama? Hujui na wala huitambui hadhi ya mahakama? Ama kweli sasa naanza kuwaelewa Kikwete na Pinda kwanini walikuwa wanamzima hadharani! Huyu
mtu anaweza kusababisha taifa lenye migogoro mikubwa nje na ndani!

Juzi nilifanya mahojiano na waziri Fenela Mkangala kaniambia kuwa Magufuli alikuwa akipewa fedha kidogo za bajeti kwenye kikao cha mawaziri kulikuwa hakukaliki! Alitaka awe yeye kwanza na anadiriki kusema wizara ya fulani haina maana hizo hela nipeni mimi! Hata hivyo bado miradi mingi haina ubora, kwa nini?

Lipo jambo lingine la 'mahakama ya mafisadi' sijui ataipa tafsiri gani kwenye mfumo wa mahakama! Au anataka kuunda mahakama ya kijeshi? Maana lazima iwe ndani ya mfumo wa kimahakama. Yote tisa kwani mahakama zilizopo zimezidiwa mpaka kuanzishwa mahakama (sijui ya kijeshi? ) Magufuli hajui kuwa kabla ya kumfunga mtu kuna kesi? Hajui kuwa kuna kushinda na kushindwa mahakamani? Ukipeleka mtuhumiwa mahakamani then akashinda utashinikiza afungwe eti kwa kuwa ni lazima umfunge?

Kesi ni lazima iamuliwe na hukumu ikitoka imetoka unashinda au umeshindwa! Labda ukate rufaa!!

Akiwa Chato juzi nikamsikia akisema "nitakutia ndani" sijui alikuwa anamwambia nani? Unamtiaje mtu ndani hujampeleka mahakamani?

Kwa kweli kuwa na kiongozi anayekurupuka hovyohovyo kama Magufuli! Hapana!

.............................
Alipokuwa Arusha alisema hadharani kuwa kiwanda cha Tanelec kimefungwa na kingeweza kuzalisha viatu bora kabisa vya ngazi. Akaomba apewe kura ili akifungue akiwa rais! Masikini kiwanda chenyewe kinazalisha vifaa vya hali ya juu kabisa vya umeme e. g Transfoma!

Leo nimefanya utafiti kuhusu lile bomba alilosema jana kumbe nalo lilishatandazwa siku nyingi ila hela ya kumalizia kazi imekosekana hali iliyowafanya wachina wasitishe kufanya kazi!

Leo akiwa Mbezi mwisho waziri Mkangara kashindwa kumuandalia mkutano kutokana na mwitikio hafifu wa watu. Cha ajabu hiyo imekuwa ajenda kwenye mikutano iliyofuata! Anamchanachana waziri wake hadharani akimuita mzembe! Sijui alitaka hao watu awatapike?
Maandishi hayafutiki...
 
Chief, watu wengi wanaofanya naye kazi wizara ya ujenzi wako perplexed na hii desperate move ya CCM kumsimamisha huyu jamaa kuwania urais. wanasema jamaa anaweza akawageuka hata wateuzi wake - and according to them CCM is likely kufia mikononi mwa Magufuli hata kama wakibahatika kupenya kwenye uchaguzi huu (a very unlikely situation of course).

wanadai jamaa si kiongozi kabisa, amekaa kiunyampara na u-foreman zaidi!
It pretty much looks like they were right!
 
Sumaye is a total failure, wala usimnukuu yule. Ameongoza serikali kama waziri mkuu for ten good yrs, yet anasema ndani ya miaka 54 serikali ya CCm haijafanya kitu, while he has been part of it for more than 20yrs...FUTSEKE!!
I hope you remember Magufuli also has been part of the governments (20 years), which he blames everyday for our current miseries.
 
32 Reactions
Reply
Back
Top Bottom