G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,874
Naomba nieleweke kuwa ni kweli pasipo shaka kabisa John Magufuli mgombea urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia CCM ana upeo mdogo sana wa kuchanganua mambo! Hajui kitu kinachoitwa kanuni za utawala bora!
Jana nimemsikia akisema eti yule mtu mwenye ghorofa aliyezuia bomba la maji lisipite angekuwa yeye ndiye mwenye mamlaka angemvunjia kwa nguvu! Huyu ndiye mtu anayepigiwa chapuo kuwa rais wa nchi!
Bomba unataka upitishe kwenye nyumba ya mtu kimabavu tu eti kwa kuwa una mamlaka? Nini maana ya mahakama? Hujui na wala huitambui hadhi ya mahakama? Ama kweli sasa naanza kuwaelewa Kikwete na Pinda kwanini walikuwa wanamzima hadharani! Huyu
mtu anaweza kusababisha taifa lenye migogoro mikubwa nje na ndani!
Juzi nilifanya mahojiano na waziri Fenela Mkangala kaniambia kuwa Magufuli alikuwa akipewa fedha kidogo za bajeti kwenye kikao cha mawaziri kulikuwa hakukaliki! Alitaka awe yeye kwanza na anadiriki kusema wizara ya fulani haina maana hizo hela nipeni mimi! Hata hivyo bado miradi mingi haina ubora, kwa nini?
Lipo jambo lingine la 'mahakama ya mafisadi' sijui ataipa tafsiri gani kwenye mfumo wa mahakama! Au anataka kuunda mahakama ya kijeshi? Maana lazima iwe ndani ya mfumo wa kimahakama. Yote tisa kwani mahakama zilizopo zimezidiwa mpaka kuanzishwa mahakama (sijui ya kijeshi? ) Magufuli hajui kuwa kabla ya kumfunga mtu kuna kesi? Hajui kuwa kuna kushinda na kushindwa mahakamani? Ukipeleka mtuhumiwa mahakamani then akashinda utashinikiza afungwe eti kwa kuwa ni lazima umfunge?
Kesi ni lazima iamuliwe na hukumu ikitoka imetoka unashinda au umeshindwa! Labda ukate rufaa!!
Akiwa Chato juzi nikamsikia akisema "nitakutia ndani" sijui alikuwa anamwambia nani? Unamtiaje mtu ndani hujampeleka mahakamani?
Kwa kweli kuwa na kiongozi anayekurupuka hovyohovyo kama Magufuli! Hapana!
.............................
Alipokuwa Arusha alisema hadharani kuwa kiwanda cha Tanelec kimefungwa na kingeweza kuzalisha viatu bora kabisa vya ngazi. Akaomba apewe kura ili akifungue akiwa rais! Masikini kiwanda chenyewe kinazalisha vifaa vya hali ya juu kabisa vya umeme e. g Transfoma!
Leo nimefanya utafiti kuhusu lile bomba alilosema jana kumbe nalo lilishatandazwa siku nyingi ila hela ya kumalizia kazi imekosekana hali iliyowafanya wachina wasitishe kufanya kazi!
Leo akiwa Mbezi mwisho waziri Mkangara kashindwa kumuandalia mkutano kutokana na mwitikio hafifu wa watu. Cha ajabu hiyo imekuwa ajenda kwenye mikutano iliyofuata! Anamchanachana waziri wake hadharani akimuita mzembe! Sijui alitaka hao watu awatapike?
Jana nimemsikia akisema eti yule mtu mwenye ghorofa aliyezuia bomba la maji lisipite angekuwa yeye ndiye mwenye mamlaka angemvunjia kwa nguvu! Huyu ndiye mtu anayepigiwa chapuo kuwa rais wa nchi!
Bomba unataka upitishe kwenye nyumba ya mtu kimabavu tu eti kwa kuwa una mamlaka? Nini maana ya mahakama? Hujui na wala huitambui hadhi ya mahakama? Ama kweli sasa naanza kuwaelewa Kikwete na Pinda kwanini walikuwa wanamzima hadharani! Huyu
mtu anaweza kusababisha taifa lenye migogoro mikubwa nje na ndani!
Juzi nilifanya mahojiano na waziri Fenela Mkangala kaniambia kuwa Magufuli alikuwa akipewa fedha kidogo za bajeti kwenye kikao cha mawaziri kulikuwa hakukaliki! Alitaka awe yeye kwanza na anadiriki kusema wizara ya fulani haina maana hizo hela nipeni mimi! Hata hivyo bado miradi mingi haina ubora, kwa nini?
Lipo jambo lingine la 'mahakama ya mafisadi' sijui ataipa tafsiri gani kwenye mfumo wa mahakama! Au anataka kuunda mahakama ya kijeshi? Maana lazima iwe ndani ya mfumo wa kimahakama. Yote tisa kwani mahakama zilizopo zimezidiwa mpaka kuanzishwa mahakama (sijui ya kijeshi? ) Magufuli hajui kuwa kabla ya kumfunga mtu kuna kesi? Hajui kuwa kuna kushinda na kushindwa mahakamani? Ukipeleka mtuhumiwa mahakamani then akashinda utashinikiza afungwe eti kwa kuwa ni lazima umfunge?
Kesi ni lazima iamuliwe na hukumu ikitoka imetoka unashinda au umeshindwa! Labda ukate rufaa!!
Akiwa Chato juzi nikamsikia akisema "nitakutia ndani" sijui alikuwa anamwambia nani? Unamtiaje mtu ndani hujampeleka mahakamani?
Kwa kweli kuwa na kiongozi anayekurupuka hovyohovyo kama Magufuli! Hapana!
.............................
Alipokuwa Arusha alisema hadharani kuwa kiwanda cha Tanelec kimefungwa na kingeweza kuzalisha viatu bora kabisa vya ngazi. Akaomba apewe kura ili akifungue akiwa rais! Masikini kiwanda chenyewe kinazalisha vifaa vya hali ya juu kabisa vya umeme e. g Transfoma!
Leo nimefanya utafiti kuhusu lile bomba alilosema jana kumbe nalo lilishatandazwa siku nyingi ila hela ya kumalizia kazi imekosekana hali iliyowafanya wachina wasitishe kufanya kazi!
Leo akiwa Mbezi mwisho waziri Mkangara kashindwa kumuandalia mkutano kutokana na mwitikio hafifu wa watu. Cha ajabu hiyo imekuwa ajenda kwenye mikutano iliyofuata! Anamchanachana waziri wake hadharani akimuita mzembe! Sijui alitaka hao watu awatapike?