mzalendokweli20021
Member
- Feb 25, 2021
- 11
- 9
Siku ya Alhamis ya tarehe 28 ya mwezi wa kwanza mwaka 2021, wadau wa Riadha Tanzania na Taifa kwa ujumla walipokea kwa furaha kazi nzuri yenye kutanguliza maslahi ya taifa mbele iliofanywa na kamati maalum ilioteuliwa na Baraza la Michezo Tanzania BMT kwa maelekezo ya Wizara ya Michezo. Kamati hii ilikua na wajumbe waliotumikia taifa hili kwa uzalendo na uadilifu wa hali ya juu kwa nafasi mbali mbali. Dkt Jonas Tiboroha ambae alikua mwenyekiti na SSP Lwambo ni sehemu ya wajumbe wanaounda kamati hii.
Bila kujali sura ya mtu, cheo chake wala mfungamano wake wa kisiasa, Kamati hii iliwaengua baadhi ya wagombea wa nafasi mbali mbali za uongozi wa juu wa chama cha Riadha ikiwa ni pamoja na aliekua Raisi wa chama hicho na Mkuu wa mkoa wa Simiyu ndugu Anthony Mtaka, pamoja na makamu wake Ndugu William Kalage. Habari za kuaminika nilizopata zinasisitiza kwamba kuenguliwa kwa bwana Mtaka na Makamu wake, pamoja na baadhi ya wagombea waliokua sehemu ya iliokua kamati tendaji iliomaliza muda wake, kulitokana na ukiukwaji mkubwa wa katiba uliotendeka kipindi cha uongozi wao.
Taarifa za ndani zinaeleza kuwa, kamati ilipokea maelekezo maalum toka kwa serikali kupitia wizara ya michezo kuhakikisha kwamba hakuna ubabaishaji utakaofanyika katika zoezi zima la uchaguzi na kupata viongozi wenye weledi na wanaokidhi matakwa ya katiba ya chama hicho kama yanavyoainishwa katika katiba mpya ya chama ya mwaka 2020. Kwa kiasi kikubwa kamati hii ilifanya kazi nzuri ya kuwatathmini wagombea wote na kuengua wale wasiofaa, lakini kasoro kubwa iko kwa alieshinda kiti cha makamu wa Rais wa chama hicho ndugu John Gilbert Bayo, na aliekua mshindi wa nafasi ya mjumbe mwakilishi wa kanda ya pwani ndugu Robert Kalyahe.
Wawili hawa wametia doa katika kazi iliotukuka iliofanywa na kamati ya uchaguzi, lakini baada ya kugundua kasoro aliokua nayo ambayo ilimnyima sifa ya kua kwenye nafasi aliochaguliwa, ndugu Robert Kalyahe kwa uungwana na ili kulinda heshima yake, heshima ya kamati na chama cha riadha kwa ujumla, aliamua kujiudhuru nafasi hiyo week chache baada ya kuchaguliwa.
Kizungumkuti hata hivyo kimebaki kwa makamu wa Rais Ndugu John Gilbert Bayo, ambae pia ni mwenyekiti wa taasisi ijulikanayo kama Tanzania Race Organisers. Nafasi anayoshika ndugu huyu inapaswa kushikwa na mtu mwenye angalau elimu ya Diploma, lakini taarifa za ndani kabisa za uhakika nilizonazo zinaeleza kwamba ndugu John Gilbert Bayo hajawahi kusoma elimu kwa kiwango cha Diploma au zaidi ya hapo sio tu Tanzania bali hata mahala pengine popote duniani.
Taarifa zinazidi kueleza kwamba, ndugu John Gilbert Bayo amewasilisha kivuli cha cheti cha mtoto wake wa kiume aitwaje Gilbert John Bayo ambae alisoma maswala ya ugavi nchini jirani ya Kenya. Inasemekana Ndugu John Gilbert Bayo, si wakati wa usaili wala sasa, hajawah kuwasilisha nakala halisi ya copy alioambatanisha kwenye form yake ya maombi.
Tukumbuke kwamba Dr John Magufuli alipoingia madarakani, uongozi wake ulianza na tumbua tumbua ya wote wenye vyeti feki, lakini takribani miaka sita baadae Dr Tiboroha anahusika katika kuingiza madarakani kwenye nafasi nyeti katika michezo, mtu mwenye vyeti feki. Utamaduni wa vyeti feki ni utamaduni ambao watanzania tulishaga usahau. Wagombea wote, akiwamo Kanali mstaafu wa Jeshi la wananchi ndugu Juma Ikangaa walikaguliwa vyeti vyao wakati wa usaili lakini sio Bwana Bayo.
Taarifa ya kukosa sifa kwa bwana Bayo ipo mezani mwa Dr Tiboroha, lakini kwanini Dr Tiboroha mtu mwenye sifa ya uadilifu hata aliondoka kwenye safu ya uongozi wa timu ya Yanga SC ili kulinda heshima yake na kuepukana na uongozi wa ubabaishaji lakini leo anapata kigugumizi kuchukua hatua zile alizokua ameanza kuchukua dhidi ya ndugu Kalyahe kabla hajajiudhuru?
Kwanini mtu kama SSP Lwambo anapata kigugumizi dhidhi ya ndugu Bayo? Kwanini mtu mwenye ushawishi miongoni mwa wajumbe wa mkutano mkuu wa chama cha riadha Ndugu Mtakwa ameweza kuenguliwa lakini imeshindikana kwa bwana Bayo? jibu ni watu wawili waliopo nyuma ya Bwana John Gilbert Bayo nao si wengine bali ni Bi Neema alieko BMT na ndugu Filbert Bayi mwenyekiti wa TOC.
Je hawa wawili kwanini wanamlinda ndugu Bayo hali wakijua hana sifa? Neema na Bayi inasemekana ndio waliopiga simu kwa Dr Tiboroha kumshawishi asikague vyeti vya Bayo wakati wa usaili na hatimae kupitishwa bila kukaguliwa vyeti vyake, je Bayi amemshawishi vipi Dr Tiboroha?. Ukiacha kua hawa watatu (Bayi, Bayo na Neema) ni watu wa kabila moja, kuna nini zaidi nyuma ya pazia hata wawe interested kupanga safu za uongozi wa taasisi zote zinazohusiana na mchezo wa riadha Tanzania? swali hili, hasa kuhusu maslahi ya Filbert Bayi kwenye mchezo wa riadha nitalijibu kwenye makala nyingine.
Kwasasa ninamuacha Dr Tiboroha kuona kama kweli anao ujasiri, na moral conviction ya kutosha kuchukua hatua katika swala hili kwakua ninajua bado majina ya uongozi mpya hayajawasilishwa serikalini, na ninajua, hata wadau wa Riadha wapige kelele vipi, John Gilbert Bayo haendi mahali, Dr Tiboroha ataendelea kufunga masikio yake kwakua hawezi kua tayari kumkwaza ndugu Filbert Bayi.
Acha tuone.
Bila kujali sura ya mtu, cheo chake wala mfungamano wake wa kisiasa, Kamati hii iliwaengua baadhi ya wagombea wa nafasi mbali mbali za uongozi wa juu wa chama cha Riadha ikiwa ni pamoja na aliekua Raisi wa chama hicho na Mkuu wa mkoa wa Simiyu ndugu Anthony Mtaka, pamoja na makamu wake Ndugu William Kalage. Habari za kuaminika nilizopata zinasisitiza kwamba kuenguliwa kwa bwana Mtaka na Makamu wake, pamoja na baadhi ya wagombea waliokua sehemu ya iliokua kamati tendaji iliomaliza muda wake, kulitokana na ukiukwaji mkubwa wa katiba uliotendeka kipindi cha uongozi wao.
Taarifa za ndani zinaeleza kuwa, kamati ilipokea maelekezo maalum toka kwa serikali kupitia wizara ya michezo kuhakikisha kwamba hakuna ubabaishaji utakaofanyika katika zoezi zima la uchaguzi na kupata viongozi wenye weledi na wanaokidhi matakwa ya katiba ya chama hicho kama yanavyoainishwa katika katiba mpya ya chama ya mwaka 2020. Kwa kiasi kikubwa kamati hii ilifanya kazi nzuri ya kuwatathmini wagombea wote na kuengua wale wasiofaa, lakini kasoro kubwa iko kwa alieshinda kiti cha makamu wa Rais wa chama hicho ndugu John Gilbert Bayo, na aliekua mshindi wa nafasi ya mjumbe mwakilishi wa kanda ya pwani ndugu Robert Kalyahe.
Wawili hawa wametia doa katika kazi iliotukuka iliofanywa na kamati ya uchaguzi, lakini baada ya kugundua kasoro aliokua nayo ambayo ilimnyima sifa ya kua kwenye nafasi aliochaguliwa, ndugu Robert Kalyahe kwa uungwana na ili kulinda heshima yake, heshima ya kamati na chama cha riadha kwa ujumla, aliamua kujiudhuru nafasi hiyo week chache baada ya kuchaguliwa.
Kizungumkuti hata hivyo kimebaki kwa makamu wa Rais Ndugu John Gilbert Bayo, ambae pia ni mwenyekiti wa taasisi ijulikanayo kama Tanzania Race Organisers. Nafasi anayoshika ndugu huyu inapaswa kushikwa na mtu mwenye angalau elimu ya Diploma, lakini taarifa za ndani kabisa za uhakika nilizonazo zinaeleza kwamba ndugu John Gilbert Bayo hajawahi kusoma elimu kwa kiwango cha Diploma au zaidi ya hapo sio tu Tanzania bali hata mahala pengine popote duniani.
Taarifa zinazidi kueleza kwamba, ndugu John Gilbert Bayo amewasilisha kivuli cha cheti cha mtoto wake wa kiume aitwaje Gilbert John Bayo ambae alisoma maswala ya ugavi nchini jirani ya Kenya. Inasemekana Ndugu John Gilbert Bayo, si wakati wa usaili wala sasa, hajawah kuwasilisha nakala halisi ya copy alioambatanisha kwenye form yake ya maombi.
Tukumbuke kwamba Dr John Magufuli alipoingia madarakani, uongozi wake ulianza na tumbua tumbua ya wote wenye vyeti feki, lakini takribani miaka sita baadae Dr Tiboroha anahusika katika kuingiza madarakani kwenye nafasi nyeti katika michezo, mtu mwenye vyeti feki. Utamaduni wa vyeti feki ni utamaduni ambao watanzania tulishaga usahau. Wagombea wote, akiwamo Kanali mstaafu wa Jeshi la wananchi ndugu Juma Ikangaa walikaguliwa vyeti vyao wakati wa usaili lakini sio Bwana Bayo.
Taarifa ya kukosa sifa kwa bwana Bayo ipo mezani mwa Dr Tiboroha, lakini kwanini Dr Tiboroha mtu mwenye sifa ya uadilifu hata aliondoka kwenye safu ya uongozi wa timu ya Yanga SC ili kulinda heshima yake na kuepukana na uongozi wa ubabaishaji lakini leo anapata kigugumizi kuchukua hatua zile alizokua ameanza kuchukua dhidi ya ndugu Kalyahe kabla hajajiudhuru?
Kwanini mtu kama SSP Lwambo anapata kigugumizi dhidhi ya ndugu Bayo? Kwanini mtu mwenye ushawishi miongoni mwa wajumbe wa mkutano mkuu wa chama cha riadha Ndugu Mtakwa ameweza kuenguliwa lakini imeshindikana kwa bwana Bayo? jibu ni watu wawili waliopo nyuma ya Bwana John Gilbert Bayo nao si wengine bali ni Bi Neema alieko BMT na ndugu Filbert Bayi mwenyekiti wa TOC.
Je hawa wawili kwanini wanamlinda ndugu Bayo hali wakijua hana sifa? Neema na Bayi inasemekana ndio waliopiga simu kwa Dr Tiboroha kumshawishi asikague vyeti vya Bayo wakati wa usaili na hatimae kupitishwa bila kukaguliwa vyeti vyake, je Bayi amemshawishi vipi Dr Tiboroha?. Ukiacha kua hawa watatu (Bayi, Bayo na Neema) ni watu wa kabila moja, kuna nini zaidi nyuma ya pazia hata wawe interested kupanga safu za uongozi wa taasisi zote zinazohusiana na mchezo wa riadha Tanzania? swali hili, hasa kuhusu maslahi ya Filbert Bayi kwenye mchezo wa riadha nitalijibu kwenye makala nyingine.
Kwasasa ninamuacha Dr Tiboroha kuona kama kweli anao ujasiri, na moral conviction ya kutosha kuchukua hatua katika swala hili kwakua ninajua bado majina ya uongozi mpya hayajawasilishwa serikalini, na ninajua, hata wadau wa Riadha wapige kelele vipi, John Gilbert Bayo haendi mahali, Dr Tiboroha ataendelea kufunga masikio yake kwakua hawezi kua tayari kumkwaza ndugu Filbert Bayi.
Acha tuone.