Awali ya yote kwanza nilipongeze Gazeti la Mwananchi kwa kazi nzuri sana juu ya uchunguzi wa kina katika kujua chanzo cha kifo cha Shirika la Chuma nchini , binafsi nimesoma matoleo yote mawili yaani toleo la Jumatano , Januari 27 na toleo la pili Januari 28 , 2021. Shirika la Chuma lilianzishwa mwaka 1966 likiwa na lengo kubwa katika kusimamia rasilimali madini aina ya Chuma nchini .
Lakini kwa kukosa uzalendo Meneja Mkuu wa shirika hilo Bw. John Fissoo na aliyekuwa Mkurugenzi wa Fedha Bw. Makika Kasuga ndio waliofanya juhudi zote za kuliua shirika hilo la taifa kwa tamaa zao na maslahi binafsi kwa kujimilikisha mali za shirika ikiwa pamoja na kuuza vitega uchumi mbalimbali vya shirika hilo kama vile Nyumba za shirika , Viwanja vya shirika , Fedha mbalimbali za Shirika hilo.
Gazeti la mwanachi mmefanya kazi yenu nzuri lakini maajabu ni kwamba chombo cha serikali ambacho kina kazi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini hakijui chochote juu sakata hili ameulizwa mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU anasema hana kumbukumbu sahihi , yaani mkurugenzi mkuu unasema huna kumbukumbu juu ya jambo la maslahi ya taifa? upo hapo kwa faida ya nani? Kwa hali hiii hata TAKUKURU ni sehemu ya kutoa na kupokea rushwa wala rushwa wote.
Lakini kwa kukosa uzalendo Meneja Mkuu wa shirika hilo Bw. John Fissoo na aliyekuwa Mkurugenzi wa Fedha Bw. Makika Kasuga ndio waliofanya juhudi zote za kuliua shirika hilo la taifa kwa tamaa zao na maslahi binafsi kwa kujimilikisha mali za shirika ikiwa pamoja na kuuza vitega uchumi mbalimbali vya shirika hilo kama vile Nyumba za shirika , Viwanja vya shirika , Fedha mbalimbali za Shirika hilo.
Gazeti la mwanachi mmefanya kazi yenu nzuri lakini maajabu ni kwamba chombo cha serikali ambacho kina kazi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini hakijui chochote juu sakata hili ameulizwa mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU anasema hana kumbukumbu sahihi , yaani mkurugenzi mkuu unasema huna kumbukumbu juu ya jambo la maslahi ya taifa? upo hapo kwa faida ya nani? Kwa hali hiii hata TAKUKURU ni sehemu ya kutoa na kupokea rushwa wala rushwa wote.