Jogoo ashikiliwa polisi kwa kumuua mmiliki wake

Johnny Sins

JF-Expert Member
Nov 4, 2019
2,538
3,826
Mtu mmoja ameuawa na Jogoo wake aliyekuwa amefungwa kisu mguuni kwa ajili ya mchezo uliopigwa marufuku wa kupambanisha jogoo Kusini mwa India.

Mmiliki wa jogoo alichomwa kisu usawa wa kati ya tumbo na nyonga wakati kuku huyo akijaribu kutoroka. Mwanaume huyo alipoteza maisha akiwa njiani kuelekea hospitali kwasababu ya kupoteza damu nyingi.

Polisi hivi sasa wanawatafuta watu wengine 15 waliohusika kwenye tukio hilo, ambalo lilifanyika kwenye kijiji cha Lothunur jimbo la Telangana wiki hii.

Kuku huyo alishikiliwa katika kituo cha polisi kabla ya kupelekwa shambani.

Polisi wamesema mnyama huyo alikuwa akitayarishwa kwa ajili ya kushiriki mpambano alipojaribu kutoroka.

Mmiliki alijaribu kumkamata lakini alichomwa na kisu hicho chenye urefu wa sentimita 7 kilichokuwa kimefungwa kwenye mguu wa kuku huyo wakati wa purukushani hizo.

Wale waliohusika katika tukio hilo wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya kutokusudia, kujihusisha na mchezo haramu wa kamari na kuhodhi mchezo wa kupiganisha kuku, shirika la habari la Ufaransa limeripoti.

Afisa polisi katika eneo hilo B Jeevan amesema kuku huyo atapelekwa mahakamani kwa ajili ya ushahidi, kwa mujibu wa gazeti la The New Indian Express.

Mchezo wa kuwapambanisha jogoo ulipigwa marufuku India mwaka 1960, lakini mchezo huo bado ni maarufu vijijini kama Telangana wengi hasa katika matamasha ya jamii ya Hindu wa Sankranti.

Si mara ya kwanza kwa mmiliki wa kuku kuuawa na jogoo wake.

Mwaka jana mwanaume mmoja huko Andhra Pradesh aliaga dunia baada ya kukatwa shingoni na kiwembe kilichokuwa kimefungwa kwenye mguu wa jogoo.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la CNN, mmiliki alikuwa akimchukua jogoo wake tayari kwa mpambano wa jogoo wakati tukio hilo lilipotokea.

CHANZO- BBC SWAHILI
 
Hapa sasa ndo unaamia kati ya trump na bin laden.sababu kama simba itashinda match mbili au moja na nusu tayari anakuwa na uhakika. Kinachofuatia ni ACT Wazalendo sasa kupeleka jina JF Kujua nani alitembea naye.
 
BBC Hawawezi kumuita Jogoo 'Mnyama'.
Habari hii itakuwa ni ya kusadikika au tena umeongeza Chumvi kunako Togwa.
 
BBC Hawawezi kumuita Jogoo 'Mnyama'.
Habari hii itakuwa ni ya kusadikika au tena umeongeza Chumvi kunako Togwa.

Mkuu nimeiona hii habari hata Al Jazeera wameweka
IMG_5978.jpg
 
Back
Top Bottom