Joe Biden: Urusi ikiivamia Ukraine isahau kuhusu bomba la mafuta

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,805
4,484
1644313742101.png

Picha: Kushoto Rais wa Marekani Joe Biden. Kulia rais wa Urusi Vladmir Putin

Rais wa Marekani Joe Biden ameapa kufunga bomba muhimu la gesi la Urusi kuelekea Ujerumani iwapo Moscow itaivamia Ukraine.

Akizungumza baada ya mazungumzo na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz mjini Washington, Biden amesema Marekani "itamaliza" bomba la Nord Stream 2.

Mazungumzo yao yamekuja wakati Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akiwa amekutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin huko Moscow na kuelezea matumaini kwamba vita vinaweza kuepukwa.

Kwa sasa Urusi ina zaidi ya wanajeshi 100,000 waliokusanyika kwenye mipaka ya Ukraine.

Katika wiki za hivi karibuni, Moscow imetaka muungano wa kijeshi wa nchi za Magharibi NATO kupiga marufuku Ukraine kuwa mwanachama, na kwamba kundi hilo lipunguze idadi ya wanajeshi wake mashariki mwa Ulaya.

Mvutano kati ya Urusi, Ukraine na nchi za Magharibi unakuja karibu miaka minane baada ya Urusi kuiteka rasi ya Crimea kusini mwa Ukraine na kuunga mkono uasi katika eneo la mashariki la Donbas.
 
View attachment 2112467
Picha: Kushoto Rais wa Marekani Joe Biden. Kulia rais wa Urusi Vladmir Putin

Rais wa Marekani Joe Biden ameapa kufunga bomba muhimu la gesi la Urusi kuelekea Ujerumani iwapo Moscow itaivamia Ukraine...

Marekani imekuwa kama mbwa koko tu siku hizi. Mpaka aibu, yaani wamekuwa na ghubu kama zote.

Afghanistan wameondoka kwa aibu sasa kwa Putin wataona jua kweli haya majinga?
 
Ulaya haina jeuri dhidi ya Putin. Gesi yao asilimia kubwa inatoka Urusi. Marekani anabwaka tu ila madhara ya ukosefu wa gesi itawahusu wazungu ulaya kwa kiasi kikubwa.

EU hawezi ku survive bila Urusi. Ndo maana Macron imebidi atumwe aongee na mkubwa.

Marekani haina hela tena ya kufadhili vita husuani baada ya aibu kule Afghanistan na janga hili la Korona, hata EU hawapo tayari kwa vita.

Putin anachukua turufu mapeeeeeema. Maana amewatishia na wametishika kweli
 
Back
Top Bottom