Job Ndugai: Ipo haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Ipo haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Swali toka kwa Mwanahabari Huru: Je -Waliompiga Lissu risasi wameshapatikaka?

-CCTV ulishawai kuhoji nani amezitoa?

-Lissu alipigwa risasi akiwa Jimboni au kazini Hapo Dodoma?

Ukiwa kiongozi Ushabiki ni mbaya

=====================

Spika wa Bunge Bw.Job Ndugai amesema atasimamisha Mshahara na Malipo yote ya Mbunge wa Singida Mashariki Mhe.Tundu Lisu kuanzia mwezi huu kutokana ana Ofisi yake kutokuwa na Taarifa sahihi ya mahali alipo kwasasa na anachokifanya huko. Hii ina maana Lissu hatalipwa mshahara tena kuanzia sasa hadi pale Spika atakapojisikia.

#MyTake:
Hawa ndio wale Balozi Masilingi alisena wameumizwa sana na shambulio la Lissu. Yani waliumizwa sana lakini hawajahangaika kujua aliyeng'oa camera za CCTV. Waliumizwa sana wakaondoa ulinzi siku ya shamvulio la Lissu. Wakaumizwa sana lakini wakamnyima hela za matibabu ili afe, lakini Mungu akamuokoa kwa neema. Sasa wameumizwa sana wameamua kumsimamishia mshahara. Hivi bado tunahangaika kutafuta waliomshambulia Lissu kwa risasi?
 
po haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Swala toka kwa Mwanahabari Huru: Je waliompiga Lissu risasi wameshapatikaka? CCTV ulishawai kuhoji nani amezitoa Lissu alipigwa risasi akiwa Jimboni au kazini Hapo Dodoma? Ukiwa kiongozi Ushabiki nimbaya
Nasikia aliandaliwa risala, sijui alipelekewa? Au ilihifadhiwa kwenye Hansard.
Akishamaliza kipimo chake cha kumbukumbu na uvumilivu wa kusafiri na kukaa bila ya kutegemea msaada wa vifaa, ataruhusiwa kurudi.
 
Ipo haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Swali toka kwa Mwanahabari Huru: Je -Waliompiga Lissu risasi wameshapatikaka?

-CCTV ulishawai kuhoji nani amezitoa?

-Lissu alipigwa risasi akiwa Jimboni au kazini Hapo Dodoma?

Ukiwa kiongozi Ushabiki ni mbaya
Kwani aliwahi kuwa na ripoti yoyote ya daktari wa Lisu?!.......... Mnara wa babeli
 
Kauli za Magu zimekuwa mifano halisi katka kujibu maswali anayoulizwa pindi Lissu akiwa anahojiwa

Kauli za Magu zimekuwa zikiwapa wakati mgumu mabalozi na watu wengine wanapojaribu kumtetea pale Lissu akiweka mambo hadharani

Kama kuna kitu wasiojulikana walikosea basi ni kumshambulia mwanasheria na zaidi ni mwanasiasa na inabidi mjuute maana ye anapigana na maadui anaowafahamu ndio maana tunasikia kila aina ya vilio
 
Mmechelewesha sana huo uamuzi Ndugai fanyeni haraka. Kama kuna mzigo kwenye akaunti yake nao uchukueni kabisa kufidia, hawezekani tunalipa kodi halafu mnawapa watu kirahisi tu
 
Mpaka Muda huu ilitakiwa Katibu Mkuu wa Bunge ajiuzulu Kama aliendelea kumlipa Mtu Mshahara wakati hayupo eneo la Kazi Na Hakuna taarifa yoyote ya kimaandishi ya kutokuwepo kazini Na Sasa hivi anaonekana anazurura Kwenye Channel Za Kimataifa anachafua Nchi
 
Mpaka Muda huu ilitakiwa Katibu Mkuu wa Bunge ajiuzulu Kama aliendelea kumlipa Mtu Mshahara wakati hayupo eneo la Kazi Na Hakuna taarifa yoyote ya kimaandishi ya kutokuwepo kazini Na Sasa hivi anaonekana anazurura Kwenye Channel Za Kimataifa anachafua Nchi
Mkuu mbona huyu bwana anaogopwa sana....si waamke siku moja wafute kila kitu yaishe!!!! maana kila siku hakuna habari zaidi yake............
 
Back
Top Bottom