Joaquim Chissano: Siwezi kuzungumza Kiswahili kama mnavyodhani

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
613
1,775
"Ahsante sana kwa kukumbusha watu kuwa nilizungumza kwa Kiswahili kule Umoja wa Afrika, na ile ilikuwa tu kuwakumbusha watu kwamba Kiswahili ilikuwa ni lugha rasmi ya Umoja wa Afrika kipindi kile na watu wakaamini kuwa nilikuwa nafahamu Kiswahili vizuri. Lakini si kweli kwamba nafahamu Kiswahili kwa kiasi hicho, na kwahiyo siwezi kutoa hotuba yangu kwa Kiswahili. Niruhusu nizungumze Kiingereza."

Rais Mstaafu wa Msumbiji Joaquim Chissano amezungumza hayo leo Julai 14, 2022 katika Kongamano la Pili la kumuenzi aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa.

Kwa miaka mingi imekuwa ikiaminika kuwa Chissano anazungumza vizuri Kiswahili. Na watu wengi wanaounga mkono mafanikio ya Kiswahili wamekuwa wakitoa mfano wa Chissano na hotuba yake ya mwaka 2004 ambayo, kwa mujibu wake leo, si kama ambavyo tumekuwa tukiamini.

Kwa kumbukumbu: Julai 6, 2004, Mzee Joaquim Chissano ambaye wakati huo alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), aliamua kutumia lugha ya Kiswahili kutoa hotuba yake muhimu ya kuaga kiti akimuachia kijiti cha uenyekiti Rais wa Nigeria wa wakati huo, Olusegun Obasanjo.

joaquim-chissano-1.jpg

Joaquim Alberto Chissano ni mwanasiasa ambaye alikuwa Rais wa pili wa Msumbiji, kuanzia 1986 hadi 2005. Anasifiwa kwa kuibadilisha Msumbiji iliyokumbwa na vita kuwa mojawapo ya nchi za Afrika zenye demokrasia yenye mafanikio makubwa.
 
Watoto wa siku hizi huko shule mnaenda kusomea ujinga mtupu.
Kwa hapa wewe unaonekana mjinga kuliko mie nilieuliza swali.

Jf ina great thinkers kibao, nikategemea nitajibiwa na mmoja kati yao bahati mbaya umejibu wewe.

Moja ya faida za hii jf ni kutoana tongotongo cha ajabu kuna ujuaji usio na faida.

Kama hujui kausha si lazima kujibu au kukejeli.
 
week argument, poor reasoning....

Angesema anaweza kusoma speech lakini kuongea na kujibizana hawezi angeeleweka

Anashindwaje kutoa speech wakati alishawahi kutoa speech ?

Waafrika tunakunywa maziwa ya ng'ombe, mbuzi, kondoo tukiwa vichanga, ambayo hayana Ferrous Oxide ya kukuza ubongo. Tunadumaa akili.
 
week argument, poor reasoning....

angesema anaweza kusoma speech lakini kuongea na kujibizana hawezi angeeleweka

anashindwaje kutoa speech wakati alishawahi kutoa speech ????

Waafrika tunakunywa maziwa ya ng'ombe, mbuzi, kondoo tukiwa vichanga, ambayo hayana Ferrous Oxide ya kukuza ubongo. Tunadumaa akili.




.
Speech za marais wengi huandikiwa na mwandishi wa hotuba za rais ikulu kulingana na hoja anayoitaka, hivyo yeye huisoma tu.
Chissano hajasema hakijui kabisa kiswahili, anakijua kiasi kwani aliishi Tanzania na pia msumbiji kaskazini kuna kiswahili.
 
Back
Top Bottom