Joe anachotaka kufanya ni kutaka kwendana na soko la sasa coz ukiangalia na kuchunguza nymbo nyingi za sasa hazina ujumbe kama za zaman¤
Mfano nyimbo kama za G NAKO Na NIKI WA 2 ( weusi kwa ujumla )
Huu utafiti uliufanyia ?KWA TAARIFA YAKO WAPENDA MZIKI WENGI NI WALE TULIOKIMBIA UMANDE NA NI WASOMI WACHACHE SANA WANAHUDHURIA SHOW NA KUWANUFAISHA WASANII.
True ...sio yeye tu " hata yule nick wa pili ..sijui ndio anaimba nini upuuzi mtupuHuyu jamaa anapenda hip pop na uwezo wa ku flow anao mzuri si mbaya.shida kubwa amekosa akili ya kutunga wimbo ukawa na maana yaani ukaeleweka anaongelea nini
Ana tofauti kubwa na fid q ambaye anaonekana kuwa ni mtu mwenye akili anatulia anapoimba na ana falsafa.jo makini ukisikiliza nyimbo zake maneno mengine ni ya kipuuzi ili mradi akamilishe vina.
Nmemsikia anasema
"....akate gogo
Akalie kigogo...."
Na mengine mengine mengi ya kipuuzi ili verse iishie na GO. nyimbo zake nyingi ana flow nzuri lakini anakosa akili ya kutunga mistari yenye madini kama wengine hasa fid q. Najua watu wa R Chuga hapa watakuja kutoa povu sana.
Mi nmesema ninachokiona.jo makini hana akili au umakini wa kutunga mistari yenye akili au madini.analazimisha vina.