pamoja na mazuri ambayo yalitokana na jkt, lakini si vyema kukataa au kujifanya vipofu kwa yale mabaya yaliyotokea jkt.
tunakataa kujifunza utoro lakini tunajisifu kujongo, tunakataa kujifunza uongo lakini tunajisifu kudanganya uanamichezo wetu na tunaita mbinu za medani, tunakataa kujifunza kuita watu malaya, wezi nk lakini tunajikumbusha kwa mapenzi nyimbo za mchakamchaka,
tunaita wadada zetu wapenda shushu lakini tunasahau sulba ambazo baadhi ya wadada walizipata ili kuwalazimisha kutoa "vitu" na kwa wale waliogangamala tunasahau vidonda vya kisaikolojia ambavyo walivipata.
nasema tena jkt ilikuwa na mazuri yake lakini kama nikiambiwa irudi leo ningependa isije kama ile niliyopitia mimi bali iwe na mabadiliko muhimu.
Kafara,
Sidhani kama kuna mtu hapa anatetea yote ya JKT. Kuna mambo mengi sana ambayo hayakuwa sawa na ndio maana ilikufa. Kwa uzalishaji ule, ilitakiwa kabisa JKT ijitegemee lakini wajanja wakaanza kuiba nk.
Nikiangalia faida na hasara zake, nakuta faida nyingi zaidi na ndio maana kama uchumi unaruhusu mimi ningependa JKT iendelee na nitakuwa tayari kuwaona watoto wangu wanaenda JKT.
Hizi institutions zote zinakuwa na matatizo yake na ndio maana neno CHANGE ni muhimu sana katika muda wote wa uhai wa mwanadamu.