green29
JF-Expert Member
- Jul 4, 2007
- 311
- 41
JKT ilianzisha na Israel na hata sasa wanafufua JKT kwa kuwashirikisha.
Mzee Madela wa madilu point yako katika thread ya Ubalozi wa israel imenikumbusha kitu muhimu sana kuhusu jeshi la kujenga Taifa JKT na ule utaratibu wa vijana wote kupitia huko. Sisi wengine hatukubahatika kupitia huko japo wakati mwingine tunadandiaga stori za huko kwa style ya Brazameni.
Sina hakika kama mada kama hii imeshawahi kujadiliwa lakini ningeomba tutoe maoni na mchango wetu labda wahusika wanaweza kupata points flani hapa ili iwapo kutakuwa na sababu ya Kurudisha JKT basi iwe na manufaa kwa Taifa.
Nyakati zinabadilika na mahitaji pia huwa yanabadilika. Inawezekana kabisa sababu za kuwa na JKT miaka hiyo hazitoshi tena kuhalalisha kurudisha hili jeshi.
Je makusudi ya kuanzisha JKT miaka hiyo yalikuwa ni yapi? Nilisikia kuwa JKT ilifutwa sababu ya gharama kuwa kubwa. Hii ilinifanya nijue kuwa JKT haikulenga kuzalisha mali bali kuwafundisha vijana kuzalisha mali; au inawezekana ililenga kuzalisha mali lakini ikashindwa kufikia malengo. Swali kubwa ni kuwa JKT inataka irudishwe kwa makusudi mapya au hayohayo ya mwanzo? JKT ikirudishwa itawezaje kuisadia nchi yetu na vijana kwa ujumla?
Nilikuwa naongea na kijana mmoja toka Ghsna akaniambia huko kwao wana utaratibu wa Kufanya kazi kwa mwaka mmoja kuchangia maendeleo ya jamii mara baada ya kumaliza masomo ya sekondari, vyuo vya ufundi, afya, au chuo kikuu. Ni kama kazi za kujitolea lakini wanakuwa wanalipwa posho flani kuwawezesha kujikimu. Na hii wamelenga kufikisha huduma za elimu, na afya maeneo amabayo bado hayajafikiwa.
Kwa Tanzania hivi karibuni wameanzisha mtindo wa kuwapa mafunzo ya mwezi mmoja vijana waliomaliza kidato cha sita kisha wanawapeleka kufundisha sekondari kwenye maeneo ya vijijini ambayo hayana walimu wa kutosha. Mpango huu kwa kiasi flani "umesaidia" kupunguza tatizo la walimu japo kwa mtazamo mwingine umeonekana ni mpango unaoshusha kiwango cha elimu.
NI kweli kuna maeneo ya nchi yetu yana hali mbaya sana ukizingatia hakuna incentives kwa wataalam mbalimbali kuishi na kufanya kazi huko. Nakumbuka mwaka juzi wakati wanaajiri wataalam wa afya kwenye BENJAMIN MKAPA HIV/AIDS FOUNDATION, walisema mpango wao umelenga kupeleka wataalamu wa afya kwenye wilaya zenye mazingira magumu na ukosefu wa wataalamu.
Cases nilizozitoa hapo juu zinanifanya nione kuwa JKT inaweza kutumika sio kwa kujifunza gwaride tu lakini pia kutoa mchango wa maendeleo kwenye sehemu za nchi yetu na kwa watanzania wenzetu waishio maeneo ambayo wataalamu wetu wanashindwa kufanya kazi. Serikali inaweza kufanya trade off kwa kugharamia elimu ya juu na kisha badala ya kulipa madeni watu wakafanya kazi ya kujitolea kwa vipindi maalum kupitia JKT. Kuna watu wengi wanapomaliza masomo wanakaa zaidi yamwaka mmoja wakitafuts kazi. Humu wamo madaktari, walimu, manesi, engineers, wanasheria, watu wa ustawi wa jamii, architects, n.k. Na wanapotafuta kazi wanaambiwa wawe na ujuzi.
Kwa maoni yangu zoezi hili litasaidia kupunguza tatizo la wataalamu kwenye maeneo yenye mazingira magumu na pia litawajengea uwezo (uzoefu) wataalam wapya maana itakuwa ni kama internship ilivyo kwa madaktari na wanasheria. Kwa upande mwingine serikali inaweza kuendelea kuwasomesha watanzania bure katika Elimu ya juu kwa makubaliano na kujua kuwa baada ya kuhitimu mtu atawajibika kujitolea kwa mwaka mmoja.
Serikali inaweza kuwalipa wataalam hawa posho za kujikimu kwa kipindi chote cha kujitolea kwa mtindo ambao wizara ya Elimu inafanya kwa walimu wa leseni.
It sounds like siasa ya ujamaa na kujitegemea lakini Ni mtazamo wangu, nakaribisha mitazamo tofauti kwa lengo la kujenga nchi yetu.