JK's 8 Days Iringa Tour

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,873
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

nembo.jpg

PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania.
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Fax: 255-22-2113425
E-mail: press@ikulu.go.tz



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali imetenga sh bilioni 31 kwa kipindi cha mwaka huu wa fedha (2008/09) kwa ajili ya ruzuku ya mbolea ili kuwezesha upatikanaji wa uhakika zaidi wa bidhaa hiyo katika jitihada za kuwaondolea makali wakulima nchini na kuwawezesha kuongeza uzalishaji.

Hayo yameelezwa leo (Ijumaa, Agosti Mosi, 200 asubuhi na Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati anazungumza na wananchi wa eneo la Ifunda katika siku yake ya kwanza ya ziara ya siku nane mkoani Iringa.

Rais Kikwete amesema kuwa kiasi hicho cha ruzuku ni ongezeko la kiasi cha mara nne tokea Serikali yake ilipoingia madarakani Desemba, mwaka 2005

“Tuliahidi kuongeza fedha kwenye mfuko wa mbolea; wakati tunaingia madarakani ilikuwa ni Sh bilioni 7 tukaongeza ikafika Sh bilioni 21, mwaka huu tumeongeza hadi Sh bilioni 31”, Rais amesema

Hata hivyo, Rais Kikwete amewaambia wananchi wa Ifunda kwamba upatikanaji wa uhakika wa mbolea nchini utawezekana tu kwa kuongeza uzalishaji mbolea katika kiwanda cha mbolea cha Minjingu na kujengwa kwa kiwanda kipya Mtwara.

“Tunafanya jitihada ya kuongeza upatikanaji wa mbolea zaidi kwa kuongeza uzalishaji katika kiwanda cha mbolea cha Mijingu, ambako uzalishaji kwa sasa ni tani laki moja kwa mwaka; tunataka zifikie laki tatu. Jitihada zingine ni kujenga kiwanda cha mbolea kwa kutumia gesi asilia Mtwara. Tunategemea baada ya miaka mitatu tutakuwa tumetatua tatizo la mbolea”, Rais ameongeza

Serikali itakuwa inaongeza ruzuku pale inapobidi lakini pia ameonya kuwa unafuu huo wa kuongeza ruzuku unaweza usionekane kutokana na kupanda kwa bei ya mbolea duniani.

Asubuhi hii, Rais pia amewasiliamia na kusikiliza matatizo yao wananchi katika miji ya Nyololo, Makambako, na Njombe. Rais pia atakagua Shule ya Wasichana ya Anna Makinda na kisha kuelekea Mlangali, Ludewa ambako atapokea taarifa ya wilaya.

Mwisho

Imetolewa na:
Premi Kibanga
IRINGA
01 Agosti, 2008




NB: Press Release attached.
 

Attachments

  • 080801 Taarifa ya Ziara ya Rais Iringa.pdf
    105.3 KB · Views: 111
Siku nane katika mkoa mmja? May be jamaa ashaanza kampeni za uchaguzi 2010 bila sisi kujua. Chadema inabidi wawe macho maana jamaa safari hii atabeba zaidi 80 % kama wasipoangalia. Vijijini huko hawajui mambo ya Richmonduli, EPA n.k. wao watakachoona rais yuko karibu nao period.
 
Siku nane katika mkoa mmja? May be jamaa ashaanza kampeni za uchaguzi 2010 bila sisi kujua. Chadema inabidi wawe macho maana jamaa safari hii atabeba zaidi 80 % kama wasipoangalia. Vijijini huko hawajui mambo ya Richmonduli, EPA n.k. wao watakachoona rais yuko karibu nao period.

Unahoji siku nane wakati kamaliza siku tisa Tanga wiki iliyopita.
 
Iringa ni moja ya mikoa mikubwa kijiografia na pia ina wilaya nyingi nadhani kama anatumia siku moja moja kwa kila wilaya ni sawa.
 
"Tuliahidi kuongeza fedha kwenye mfuko wa mbolea; wakati tunaingia madarakani ilikuwa ni Sh bilioni 7 tukaongeza ikafika Sh bilioni 21, mwaka huu tumeongeza hadi Sh bilioni 31", Rais amesema




Inasemekana wafanya biashara wame-abandon biashara ya ku-ship TUMBAKU maana biashara ya mbolea (kwa ajili ya tumbaku) inalipa zaidi. Habari hizi zilitolewa kwenye TV mwezi jana.


Hofu yangu kubwa ni hapo Kikwete atakapoamua kugombea urais kwa mara nyingine which is very likely. Siku tutakapopata hizo fununu, tayari tutakuwa tumeshachelewa - jamaa atashinda uchaguzi tu. Tutashuhudia twist zisizo na mfano hapa Bongo. Makundi mengine humo sisiem hayatakuwa na ubavu hata wagangamae vipi!




.
 
Siku nane katika mkoa mmja? May be jamaa ashaanza kampeni za uchaguzi 2010 bila sisi kujua. Chadema inabidi wawe macho maana jamaa safari hii atabeba zaidi 80 % kama wasipoangalia. Vijijini huko hawajui mambo ya Richmonduli, EPA n.k. wao watakachoona rais yuko karibu nao period.

Naam wala hujakosea. Inaelekea huu ni mwanzo wa kampeni za 2010 na pia kuondoa malalamiko kwamba msanii anafanya ziara nje ya nchi zaidi kuliko ndani ya nchi. Alianza ziara yake Singida, akaenda Tanga sasa yuko Iringa. Inaelekea hii ziara ni ya Tanzania nzima ambayo anaweza kuikamilisha mapema mwaka ujao.
 
Siku nane katika mkoa mmja? May be jamaa ashaanza kampeni za uchaguzi 2010 bila sisi kujua. Chadema inabidi wawe macho maana jamaa safari hii atabeba zaidi 80 % kama wasipoangalia. Vijijini huko hawajui mambo ya Richmonduli, EPA n.k. wao watakachoona rais yuko karibu nao period.

Cant win! akienda nje ziara zimezidi, akitembelea mikoa kampeni. Kazi kweli kweli
 
Iringa ni moja ya mikoa mikubwa kijiografia na pia ina wilaya nyingi nadhani kama anatumia siku moja moja kwa kila wilaya ni sawa.
wao wanajua kupost tu,hawajui kama mkoa huu uko kwenye mkakati wa kugawanywa na kutoa mkoa mwingine. mzee Mwinyi alisema binadamu ni watu wa ajabu sana wakiwa na njaa tabu na wakishika ni kelele.

Rais akienda Marekani mnalalamika kuwa ni anapenda kusafiri hawezi kuijua nchi yake vizuri, akiamua kutembea nchi yake nayo ni matatizo tu.
kama Mbowe hatembei matawi yake na kupeleka ruzuku mnataka na JK asitembelee mikoa yake?
 
Siku nane katika mkoa mmja? May be jamaa ashaanza kampeni za uchaguzi 2010 bila sisi kujua. Chadema inabidi wawe macho maana jamaa safari hii atabeba zaidi 80 % kama wasipoangalia. Vijijini huko hawajui mambo ya Richmonduli, EPA n.k. wao watakachoona rais yuko karibu nao period.
Kwanini usiseme Cuf au Chausta? wewe chama ni chadema tu, hujui kama ni NGO hadi marehemu Wangwe anafariki anajua na amekufa na kinyongo akiona anaongoza chama ambacho ni NGO ya wachagga.
 
Cant win! akienda nje ziara zimezidi, akitembelea mikoa kampeni. Kazi kweli kweli

Sasa hivi matatizo yetu makubwa ni ufisadi ulioshamiri ambao msanii anajitahidi kufanya kila njia ili kukwepa kuzungumzia chochote kuhusiana na hilo na pia kuhusiana na mikataba ya madini isiyo na maslahi kwa Tanzania ikiwemo kujimilikisha Kiwira katika mazingira ya kifisadi. Pesa zilizoibwa kutoka BoT zinadaiwa kuwa ni kati ya shilingi 133 bilioni na 1 Trillioni na sasa hivi wafadhili wamekataa kutoa shilingi bilioni 812 mpaka waone hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi ya wahusika wote wa EPA. Kwa maneno mengine basi wizi wa BoT unaukosesha uchumi wa Tanzania kati ya shilingi 945 bilioni na 1.812 Trillioni. Hizi ni pesa nyingi sana. Badala ya msanii kulipa hili la EPA kipaumbele kushughulikia hili ili kuwaridhisha Watanzania na wafadhili yeye anafanya ziara ambazo kwa sasa hivi hazina kupaumbele chochote ukilinganisha na ufisadi mkubwa unawaongezea ugumu wa maisha Watanzania kila kona ya nchi yetu.
 
SteveD,

haya sasa ndugu yangu uliyeko makambako tupe yanayojiri huko...... kuhusu ziara ya JK.....lol
 
Kwani JK ameshawahi kukaa Ikulu more than a week???

Akimaliza local trips ni overseas. I pray tuna watu makini wanaojua kugovern maana ......
 
Mmmmm JF nanyi mna vijimambo. Mdogo wangu Jakaya akienda safari za ulaya na America mnamsema kwamba hawajali Watanzania na mnamwita Vasco Da Gama, sasa ameamua kuwatembelea wananchi na kujua matatizo yao mnaanza kusema ameanza kampeni za 2010. Sasa afanye lipi liwe jema jamani?.
 
anapita kila mkoa kuuliza matatizo ya wananchi.....and then what?

maanke sijasikia kuattua tatizo la mwananchi hata siku moja ......yeye kazi ni kufile up tu hayo matatizo tu.
 
Iringa siku nane, Mbeya vipi?

Inaelekea hataki tena kufanya ziara zaidi ya mkoa mmoja hivyo kila baada ya kuzuru mkoa mmoja inabidi arudi Dar na baada ya muda kuendelea na ziara katika mkoa mwingine au akiweza basi ajipangie kitrip mmoja cha nje ya nchi. Kama sikosei anatakiwa kuwa US mwezi huu kwa mwaliko wa kichaka, hivyo basi labda baada ya Iringa atakuwa anajiandaa na katrip kangine kwenda kumuaga 'rafiki' yake na anaweza pia kuongeza katrip ili apitie Paris kwenda 'kuangaliwa' afya yake.
 
Naam wala hujakosea. Inaelekea huu ni mwanzo wa kampeni za 2010 na pia kuondoa malalamiko kwamba msanii anafanya ziara nje ya nchi zaidi kuliko ndani ya nchi. Alianza ziara yake Singida, akaenda Tanga sasa yuko Iringa. Inaelekea hii ziara ni ya Tanzania nzima ambayo anaweza kuikamilisha mapema mwaka ujao.

Umesahau kutaja Songea ... alikoshindwa kuvuka kwenda nsumbiji
 
Inaelekea hataki tena kufanya ziara zaidi ya mkoa mmoja hivyo kila baada ya kuzuru mkoa mmoja inabidi arudi Dar na baada ya muda kuendelea na ziara katika mkoa mwingine au akiweza basi ajipangie kitrip mmoja cha nje ya nchi. Kama sikosei anatakiwa kuwa US mwezi huu kwa mwaliko wa kichaka, hivyo basi labda baada ya Iringa atakuwa anajiandaa na katrip kangine kwenda kumuaga 'rafiki' yake na anaweza pia kuongeza katrip ili apitie Paris kwenda 'kuangaliwa' afya yake.

Mkuu hauko mbali na ukweli,Baada ya ziara ya Iringa Mkuu anakwenda US,kwa ziara ya siku Nne kwa mualiko wa Serikali ya Marekani,atakwenda DC na baadaye New York.Ataongozana na Mawaziri 5.
 
Shida ni kwamba anapangiwa nini akione huko mikoani. Ziara hizi mbali ya gharama manufaa yake kwa Mwananchi wa kawaida ni kidogo sana. Shule zinabaki hazina madarasa, madawati, Walimu,... zahanati hazina madawa, waganga,... barabara zinachongwa mle atakamopita tu,..
 
Hivi wabunge wa huko wako Dodoma au wako na Muungwana? Na kama wako na muungwana je posho zao za kule dodoma wanalamba? na je kama wako na Jk wanalipwa posho pia kwa safari hizo? Nisaidieni hapa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom