JK zungumzia haya kwenye hotuba yako ya mwisho wa mwezi July

kapotolo

JF-Expert Member
Sep 19, 2010
3,727
2,213
Mwisho wa mwezi July umekaribia, kama utaratibu ulivyo rais huwa analihutubia taifa ingawa siku hizi hujifanya yuko busy na kukwepa.

Naomba nimkumbushe kuwa kuna mambo mengi ya msingi ambayo unatakiwa kuyatolea ufafanuzi kwa kuwa watanzania yanatuchanganya. Kwa hiyo kwenye hotuba yako, pamoja na mambo mengine utakayoyaeleza, ujumuishe na haya.

1. utueleze kuhusu matatizo ya umeme na ufumbuzi wake. Chonde chonde naomba usituambie wewe sio wingu ukanyeshe mtera, maneno haya huwa yanatuudhi sana. Tunataka kusikia ufumbuzi wa haraka wa tatizo la umeme, hali ikiendelea hivi hata wewe utashindwa kusafiri nje, serikali itakosa mapato.

2. utueleze kuhusu hatima ya Ngeleja na Malima, watu wanawaomba wawajibike wao wametia pamba masikioni, wewe kama mwajiri wao unatuambia nini? Mimi siamini kama tatizo sio wao, hata huyo Jairo ni mbuzi wa kafara, naamini ule mchango wa pesa za "kuwarushwa" wabunge ulikuwa na baraka zao.

3. ule mpango wenu wa kupunguza bei za mafuta umefia wapi, mbona bei hazishuki, tatizo ni nini? mmewapandishia watu mafuta ya taa huku mkijua wale watoto mliowatelekeza kwenye shule za kata wanasomea vibatali ambavyo vinatumia mafuta ya taa. walimu hawana na sasa mnawaondolea hata uwezo wa kujisomea wenyewe, angalieni hilo bomu litawalipukia. Naomba ufafanuzi.

4. Pia naomba uzungumzie juu ya kuzidi kupanda kwa bei za bidhaa na kushuka kila siku kwa thamani ya shilingi, mmeshindwa kudhibiti?

5. La mwisho tuambie mafanikio uliyoyapata kwenye ziara zako tano za mwisho nje ya nchi, na ziara hizo zimeligharimu taifa kiasi gani.

Najua utakuwa na mengi ya kutueleza lakini haya yangu matano naomba uyatolee ufafanuzi, kwani yananikera, naamini kuna watanzania wengi pia yanawakera.

Naomba kuwasilisha
 
Hivi huyu jamaa bado anatoaga hotuba za mwisho wa mwezi? Ya mwisho ilikuwa lini vile?
 
Mwisho wa mwezi July umekaribia, kama utaratibu ulivyo rais huwa analihutubia taifa ingawa siku hizi hujifanya yuko busy na kukwepa. Naomba nimkumbushe kuwa kuna mambo mengi ya msingi ambayo unatakiwa kuyatolea ufafanuzi kwa kuwa watanzania yanatuchanganya. Kwa hiyo kwenye hotuba yako, pamoja na mambo mengine utakayoyaeleza, ujumuishe na haya.1. utueleze kuhusu matatizo ya umeme na ufumbuzi wake. Chonde chonde naomba usituambie wewe sio wingu ukanyeshe mtera, maneno haya huwa yanatuudhi sana. Tunataka kusikia ufumbuzi wa haraka wa tatizo la umeme, hali ikiendelea hivi hata wewe utashindwa kusafiri nje, serikali itakosa mapato.2. utueleze kuhusu hatima ya Ngeleja na Malima, watu wanawaomba wawajibike wao wametia pamba masikioni, wewe kama mwajiri wao unatuambia nini? Mimi siamini kama tatizo sio wao, hata huyo Jairo ni mbuzi wa kafara, naamini ule mchango wa pesa za "kuwarushwa" wabunge ulikuwa na baraka zao.3. ule mpango wenu wa kupunguza bei za mafuta umefia wapi, mbona bei hazishuki, tatizo ni nini? mmewapandishia watu mafuta ya taa huku mkijua wale watoto mliowatelekeza kwenye shule za kata wanasomea vibatali ambavyo vinatumia mafuta ya taa. walimu hawana na sasa mnawaondolea hata uwezo wa kujisomea wenyewe, angalieni hilo bomu litawalipukia. Naomba ufafanuzi.4. Pia naomba uzungumzie juu ya kuzidi kupanda kwa bei za bidhaa na kushuka kila siku kwa thamani ya shilingi, mmeshindwa kudhibiti?5. La mwisho tuambie mafanikio uliyoyapata kwenye ziara zako tano za mwisho nje ya nchi, na ziara hizo zimeligharimu taifa kiasi gani.Najua utakuwa na mengi ya kutueleza lakini haya yangu matano naomba uyatolee ufafanuzi, kwani yananikera, naamini kuna watanzania wengi pia yanawakera.Naomba kuwasilisha
Mkuu maswali ni ya msingi sana ukweli ni hizo ndizo baadhi ya changamoto nyingi zinazowabili watz ambayo kiongozi wa nchi alipaswa kuyatolea majawabu miaka sita iliyopita!! Nasikitika tu kuwa raisi hakuchaguliwa na sehemu kubwa ya watatz wanaokabiliana na changamoto hizo...kwa hiyo hakuna wa kuyajibu hayo. Nikukumbushe kuwa hivi karibuni mkuu alinukulia kusema hizo changamoto alizikuta...so expect nothing.
 
Siku hizi hakuna mtu anasikilizaga mipasho ya JK na yeye analijua hilo wewee!
 
Sasa nyie ndiyo mnataka kumkimbiza kabisaa.... Hilo la kwanza alisha litolea ufafanuzi akipohojiwa na BiBithii hivi karibuni, yeye si wingu.
 
''Si... si... si... sihutubii, tehe tehe! Mwisho wa mwezi huu labda nitakuwa pluto''
 
Jamani! Jamani naomba mniache! Mwezi huu kwanza nina dharula ya kwenda kwa Mtarika kusuruhisha mgogoro huu. Si mnajua watanzania jinsi wanavyotuamini, hasa mimi kumbuka nilivyomaliza ya Kenya. Siji kuhutubia mwezi huu ''Akili ya kuambiwa changanya na yako''.
 
mh rais dr Jakaya Kikwete ana mambo mengi ya kuzungumzia u nani mpaka umwambie rais ajibu maswali yako, kwani uongo yeye ni mvua unafikiri atajazaje maji mtera? Mipango thabitii inahitaji muda sali mvua inyeshe. Hela inashuka thamani kutokana na mtikisiko wa uchumi. Kingine ngeleja ajiuzulu kisa umeme ?? We vipi mke haachwi kwa kosa moja mpeni nafasi.
Mwisho wa mwezi July umekaribia, kama utaratibu ulivyo rais huwa analihutubia taifa ingawa siku hizi hujifanya yuko busy na kukwepa. Naomba nimkumbushe kuwa kuna mambo mengi ya msingi ambayo unatakiwa kuyatolea ufafanuzi kwa kuwa watanzania yanatuchanganya. Kwa hiyo kwenye hotuba yako, pamoja na mambo mengine utakayoyaeleza, ujumuishe na haya. 1. utueleze kuhusu matatizo ya umeme na ufumbuzi wake. Chonde chonde naomba usituambie wewe sio wingu ukanyeshe mtera, maneno haya huwa yanatuudhi sana. Tunataka kusikia ufumbuzi wa haraka wa tatizo la umeme, hali ikiendelea hivi hata wewe utashindwa kusafiri nje, serikali itakosa mapato. 2. utueleze kuhusu hatima ya Ngeleja na Malima, watu wanawaomba wawajibike wao wametia pamba masikioni, wewe kama mwajiri wao unatuambia nini? Mimi siamini kama tatizo sio wao, hata huyo Jairo ni mbuzi wa kafara, naamini ule mchango wa pesa za "kuwarushwa" wabunge ulikuwa na baraka zao. 3. ule mpango wenu wa kupunguza bei za mafuta umefia wapi, mbona bei hazishuki, tatizo ni nini? mmewapandishia watu mafuta ya taa huku mkijua wale watoto mliowatelekeza kwenye shule za kata wanasomea vibatali ambavyo vinatumia mafuta ya taa. walimu hawana na sasa mnawaondolea hata uwezo wa kujisomea wenyewe, angalieni hilo bomu litawalipukia. Naomba ufafanuzi. 4. Pia naomba uzungumzie juu ya kuzidi kupanda kwa bei za bidhaa na kushuka kila siku kwa thamani ya shilingi, mmeshindwa kudhibiti? 5. La mwisho tuambie mafanikio uliyoyapata kwenye ziara zako tano za mwisho nje ya nchi, na ziara hizo zimeligharimu taifa kiasi gani. Najua utakuwa na mengi ya kutueleza lakini haya yangu matano naomba uyatolee ufafanuzi, kwani yananikera, naamini kuna watanzania wengi pia yanawakera. Naomba kuwasilisha
 
looo!! mtoa mada unataka Jakaya Kikwete aseme nini tena...?

Macho ya Rais yana kutu haoni vema, shida ya umeme huwa anasikia lakini haamini kuwa kuna watu wameacha kazi zao kwaajili ya ukosefu wa umeme.

Mtazamo wake ni maji tuuu ndio chanzo cha nishati, it is hard to believe kuwa Mkuu wa Nchi anasema "Serikali ya Tanzania (au yeye binafsi) haitengenezi mawingu ya mvua ili yalete maji na kujaza mabwawa".

Huo mtazamo ndio mwisho wa kufikiri kwake na msaada wake kwetu!

no comment for july's speech.
 
Sasa nyie ndiyo mnataka kumkimbiza kabisaa.... Hilo la kwanza alisha litolea ufafanuzi akipohojiwa na BiBithii hivi karibuni, yeye si wingu.
Hata mimi nashangaa sijui mnataka aongee nini Dr. Jakaya!
Dr. wewe zunguka tuu angani upewe uprofessar kabisaa!
 
mh rais dr Jakaya Kikwete ana mambo mengi ya kuzungumzia u nani mpaka umwambie rais ajibu maswali yako, kwani uongo yeye ni mvua unafikiri atajazaje maji mtera? Mipango thabitii inahitaji muda sali mvua inyeshe. Hela inashuka thamani kutokana na mtikisiko wa uchumi. Kingine ngeleja ajiuzulu kisa umeme ?? We vipi mke haachwi kwa kosa moja mpeni nafasi.
kweli bana umeeleweka sana tuu!
Mkwe,re anamambo mengi yakufanya si isue ndogo kama hizi za umeme na mfumuko wa bei!
 
Hayo kweli mkuu ni mambo ya msingi sana.
Lakini huyu kiranja mkuu hata akiamua kuyaongelea
unadhani kutakuwa na jipya? mimi binafsi huwa akianza
kuhutubia tu huwa nakosa raha na huwa simwelewi kabisa.
Mkuu wa kaya wa kuchekacheka tuu hata kwenye mambo
serious, kiukweli anaboa sana huyu................
 
JK asihangaike kutafuta maelezo magumu juu ya matatizo yanayolikabili taifa sasa hivi. ataumiza kichwa bure. Yeye aseme tu kwamba matatizo yote yanayolikabili taifa hivi sasa yanasababishwa na vyama vya Upinzani. Mgawo wa umeme, rushwa bungeni, kupanda bei ya mafuta, ufisadi n.k vyote vimesababishwa na wapinzani. Baada ya hapo aendelee na ziara zake nchi za nje
 
Mwisho wa mwezi July umekaribia, kama utaratibu ulivyo rais huwa analihutubia taifa ingawa siku hizi hujifanya yuko busy na kukwepa.

Naomba nimkumbushe kuwa kuna mambo mengi ya msingi ambayo unatakiwa kuyatolea ufafanuzi kwa kuwa watanzania yanatuchanganya. Kwa hiyo kwenye hotuba yako, pamoja na mambo mengine utakayoyaeleza, ujumuishe na haya.

1. utueleze kuhusu matatizo ya umeme na ufumbuzi wake. Chonde chonde naomba usituambie wewe sio wingu ukanyeshe mtera, maneno haya huwa yanatuudhi sana. Tunataka kusikia ufumbuzi wa haraka wa tatizo la umeme, hali ikiendelea hivi hata wewe utashindwa kusafiri nje, serikali itakosa mapato.

2. utueleze kuhusu hatima ya Ngeleja na Malima, watu wanawaomba wawajibike wao wametia pamba masikioni, wewe kama mwajiri wao unatuambia nini? Mimi siamini kama tatizo sio wao, hata huyo Jairo ni mbuzi wa kafara, naamini ule mchango wa pesa za "kuwarushwa" wabunge ulikuwa na baraka zao.

3. ule mpango wenu wa kupunguza bei za mafuta umefia wapi, mbona bei hazishuki, tatizo ni nini? mmewapandishia watu mafuta ya taa huku mkijua wale watoto mliowatelekeza kwenye shule za kata wanasomea vibatali ambavyo vinatumia mafuta ya taa. walimu hawana na sasa mnawaondolea hata uwezo wa kujisomea wenyewe, angalieni hilo bomu litawalipukia. Naomba ufafanuzi.

4. Pia naomba uzungumzie juu ya kuzidi kupanda kwa bei za bidhaa na kushuka kila siku kwa thamani ya shilingi, mmeshindwa kudhibiti?

5. La mwisho tuambie mafanikio uliyoyapata kwenye ziara zako tano za mwisho nje ya nchi, na ziara hizo zimeligharimu taifa kiasi gani.

Najua utakuwa na mengi ya kutueleza lakini haya yangu matano naomba uyatolee ufafanuzi, kwani yananikera, naamini kuna watanzania wengi pia yanawakera.

Naomba kuwasilisha

Nina amini hata kusikia na hata akikusikia ata ku-perceive kwamba wewe ni mchochezi hutaki nchi itawalike
 
Umemshauri vizuri lakini alivyo na roho yakutojali wananchi nina imani ataishia kukutukana mpaka utakoma mwenyewe
 
Back
Top Bottom