mwanaizaya
Senior Member
- Apr 26, 2008
- 133
- 1
JK: Wafanyabiashara chanzo cha ufisadi
Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, amepasua ukweli mbele ya wenye viwanda, akisema kuwa, rushwa kubwa nchini zina mkono wa baadhi ya wafanyabiashara.
Kutokana na hali hiyo, Rais alilitaka Shirikisho la Wenye Viwanda nchini (CTI), kushirikiana na serikali kupambana na rushwa nchini.
Akizungumza juzi usiku wakati wa utoaji wa Tuzo bora ya Rais kwa Wazalishaji Bora, Rais Kikwete alisema, hakuna biashara inayoweza kudumu katika mazingira ya rushwa na ukiukaji wa sheria.
Rais Kikwete ambaye alizungumza mbele ya wenye viwanda akiwemo Mwenyekiti wa CTI, Reginald Mengi, alisema, wakati mwingine katika kutafuta upendeleo wa ushindani ni wafanyabiashara ndio wanaochochea rushwa.
Alisema, kama wafanyabiashara wataamua kuacha kupenda upendeleo na upindishaji sheria, basi rushwa kubwa zitakoma.
"Lakini, pia na wenyewe mjitazame katika shughuli zenu. Na nyie mnalalamikiwa kwa rushwa katika ajira na kupata shughuli ya kufanya kama vile kupata uwakala, wahusika kuomba na kupokea rushwa," alisema Rais Kikwete.
Rais alisema: "Kama mwombaji ni msichana, basi huombwa penzi ndipo apate kazi au shughuli."
Alisema, imezoeleka kusemwa kwamba, rushwa ni adui wa haki; na akasisitiza kuwa sheria za nchi ziheshimiwe katika mienendo ya biashara na wafanyabiashara.
Alisema kuwa, serikali inatambua na kuridhishwa na mchango mkubwa wa sekta binafsi na umuhimu wa sekta ya viwanda katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya taifa.
Alisema, serikali inajivunia uamuzi wake wa kuifanya sekta binafsi kuwa injini ya ukuaji uchumi, kwani imeonyesha mafanikio ambayo ni kufanya ukuaji wa haraka wa Pato la Taifa kwa wastani wa asilimia sita kwa mwaka katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Rais aliongeza kuwa, mchango wa sekta ya viwanda katika pato hilo umeongezeka kutoka asilimia 17.2 mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 18.4 mwaka 2007, lakini akasema bado haridhishwi na mchango wa sekta hiyo katika pato la taifa.
"Vile vile, pamoja na kwamba mchango wa Pato la Taifa umeongezeka katika mauzo ya nje kutoka asilimia 5.3 mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 8.3 mwaka 2007, mchango huo ni mdogo mno ukilinganisha na uwezo wa sekta hii," alisema Rais Kikwete.
Rais alisema kuwa ni vema pia watu wakachangamkia soko katika Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), na kuongeza: "Leo mkulima wa machungwa kule Muheza, anaweza kupakia machungwa yake katika Fuso na kupeleka Mombasa tu, tofauti na kwamba apeleke Marekani itakuwa ni matatizo, mambo ya kupakia. Sisi tumefungua mipaka, fanyeni biashara."
Rais alikabidhi tuzo mbalimbali kwa viwanda katika sekta tofauti huku Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ikiibuka mshindi wa jumla
Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, amepasua ukweli mbele ya wenye viwanda, akisema kuwa, rushwa kubwa nchini zina mkono wa baadhi ya wafanyabiashara.
Kutokana na hali hiyo, Rais alilitaka Shirikisho la Wenye Viwanda nchini (CTI), kushirikiana na serikali kupambana na rushwa nchini.
Akizungumza juzi usiku wakati wa utoaji wa Tuzo bora ya Rais kwa Wazalishaji Bora, Rais Kikwete alisema, hakuna biashara inayoweza kudumu katika mazingira ya rushwa na ukiukaji wa sheria.
Rais Kikwete ambaye alizungumza mbele ya wenye viwanda akiwemo Mwenyekiti wa CTI, Reginald Mengi, alisema, wakati mwingine katika kutafuta upendeleo wa ushindani ni wafanyabiashara ndio wanaochochea rushwa.
Alisema, kama wafanyabiashara wataamua kuacha kupenda upendeleo na upindishaji sheria, basi rushwa kubwa zitakoma.
"Lakini, pia na wenyewe mjitazame katika shughuli zenu. Na nyie mnalalamikiwa kwa rushwa katika ajira na kupata shughuli ya kufanya kama vile kupata uwakala, wahusika kuomba na kupokea rushwa," alisema Rais Kikwete.
Rais alisema: "Kama mwombaji ni msichana, basi huombwa penzi ndipo apate kazi au shughuli."
Alisema, imezoeleka kusemwa kwamba, rushwa ni adui wa haki; na akasisitiza kuwa sheria za nchi ziheshimiwe katika mienendo ya biashara na wafanyabiashara.
Alisema kuwa, serikali inatambua na kuridhishwa na mchango mkubwa wa sekta binafsi na umuhimu wa sekta ya viwanda katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya taifa.
Alisema, serikali inajivunia uamuzi wake wa kuifanya sekta binafsi kuwa injini ya ukuaji uchumi, kwani imeonyesha mafanikio ambayo ni kufanya ukuaji wa haraka wa Pato la Taifa kwa wastani wa asilimia sita kwa mwaka katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Rais aliongeza kuwa, mchango wa sekta ya viwanda katika pato hilo umeongezeka kutoka asilimia 17.2 mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 18.4 mwaka 2007, lakini akasema bado haridhishwi na mchango wa sekta hiyo katika pato la taifa.
"Vile vile, pamoja na kwamba mchango wa Pato la Taifa umeongezeka katika mauzo ya nje kutoka asilimia 5.3 mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 8.3 mwaka 2007, mchango huo ni mdogo mno ukilinganisha na uwezo wa sekta hii," alisema Rais Kikwete.
Rais alisema kuwa ni vema pia watu wakachangamkia soko katika Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), na kuongeza: "Leo mkulima wa machungwa kule Muheza, anaweza kupakia machungwa yake katika Fuso na kupeleka Mombasa tu, tofauti na kwamba apeleke Marekani itakuwa ni matatizo, mambo ya kupakia. Sisi tumefungua mipaka, fanyeni biashara."
Rais alikabidhi tuzo mbalimbali kwa viwanda katika sekta tofauti huku Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ikiibuka mshindi wa jumla