Elections 2010 JK: Vyombo vya Habari visaidie kutibu majeraha ya Uchaguzi

Nicky82

JF-Expert Member
Mar 14, 2009
941
64
Wakuu,
Nimemsikia JK akitoa kauli hii jana wakati akihutubia kwenye hafla ya kutangazwa pale Karimjee na leo kwenye sherehe ya kuapishwa pale uwanja wa uhuru.

Na kuna mahali kwenye hotuba ya leo amesema ziko hoja za kidini zilizotolewa majukwaani na wanasiasa ambazo zimeleta mpasuko hivyo akavisihi vyombo vya habari visaidie kutibu majeraha na mpasuko huo.

Wote tunakumbuka hizi hoja kuhusu udini na ukabila zilishikiwa bango na kufanywa mtaji wa ccm majukwaani. Sasa hii ina maana JK anakiri ule ulikuwa ni mkakati wa kampeni au na je vyombo vya habari vitawezaje kuziba ufa huu,

Nawakilisha
.
 
Wakuu,
Nimemsikia JK akitoa kauli hii jana wakati akihutubia kwenye hafla ya kutangazwa pale Karimjee na leo kwenye sherehe ya kuapishwa pale uwanja wa uhuru.

Na kuna mahali kwenye hotuba ya leo amesema ziko hoja za kidini zilizotolewa majukwaani na wanasiasa ambazo zimeleta mpasuko hivyo akavisihi vyombo vya habari visaidie kutibu majeraha na mpasuko huo.

Wote tunakumbuka hizi hoja kuhusu udini na ukabila zilishikiwa bango na kufanywa mtaji wa ccm majukwaani. Sasa hii ina maana JK anakiri ule ulikuwa ni mkakati wa kampeni au na je vyombo vya habari vitawezaje kuziba ufa huu,

Nawakilisha
.
Mimi mpaka leo sijakielewa vizuri hicho kinachoitwa udini hasa kipo wapi!
Uduni ninaoweza kusema kama mfano ni waraka ulioletwa hapa jamvini unaowataka watu wa dini fulani wachague viongozi wa dini fulani..basi
Otherwise sijaona shida hiyo kuwa ni kubwa sana katika jamii ya kitanzania, ila inatumiwa tu na baadhi ya watu kujitafutia umaarufu majukwaani!
 
Majeraha yamesababishwa na yeye mwenyewe Kikwete, alifanya hivyo 2005 kuwajeruhi wana CCM wenzake, na mwaka huu kazitumia kumjeruhi Dr Slaa, sasa analoloma nini ? Huyu mtu ni mnafiki na elements zote za udikteta. Lakini ajuwe kuwa kipindi hiki ni kigumu kwake sana kuliko wakati wowote katika maisha yake, amekiporomosha chama chake, ameibaka demokrasia ,amevuruga uchaguzi,ametoa ahadi zisizotekelezeka, afya anazidi kudorora, mieleka kwa sana huko ikulu na zaidi sana dhamira yake inamshitaki.
 
Ivi JK ana amani ya mwili na roho following the election results?
 
Wakuu,
Nimemsikia JK akitoa kauli hii jana wakati akihutubia kwenye hafla ya kutangazwa pale Karimjee na leo kwenye sherehe ya kuapishwa pale uwanja wa uhuru.

Na kuna mahali kwenye hotuba ya leo amesema ziko hoja za kidini zilizotolewa majukwaani na wanasiasa ambazo zimeleta mpasuko hivyo akavisihi vyombo vya habari visaidie kutibu majeraha na mpasuko huo.

Wote tunakumbuka hizi hoja kuhusu udini na ukabila zilishikiwa bango na kufanywa mtaji wa ccm majukwaani. Sasa hii ina maana JK anakiri ule ulikuwa ni mkakati wa kampeni au na je vyombo vya habari vitawezaje kuziba ufa huu,

Nawakilisha
.



Majeraha kayaleta yeye, sasa anavipa vyombo vya habari kazi ya kutibu majeraha? ingekuwe vyema yeye kuyatibu kwa kukubali luwa kura zilichakachuliwa.
 
Back
Top Bottom