Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,347
- 6,471
JK kuzuia/ kuchelewesha huduma kwenye majimbo ya upinzani
Kama JK alivyowaambiwa wabunge wa Chadema wakati akizindua Bunge la 10 la Jamhuri ya Muungano kuwa ndiye Rais na watatoka, watarudi kwake yaani serikalini kutaka msaada.
Katiba inasema:
Ibara ya 13
(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya Mamlaka ya Nchi
(5) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara hii neno kubagua maana yake ni kutimiza haja, haki au mahitaji mengineyo kwa watu mbalimbali kwa kuzingatia utaifa wao, kabila, pahala walipotokea, maoni yao ya kisiasa, rangi, dini, jinsia au hali yao ya maisha kwa namna ambayo watu wa aina Fulani wanafanywa au kuhesabiwa kuwa dhaifu au duni na kuwekewa vikwazo au masharti ya vipingamizi ambapo watu wa aina nyingine wanatendewa tofauti au wanapewa fursa au faida iliyoko nje ya masharti au sifa za lazima, isipokuwa kwamba neno kubagua halifafanuliwa kwa namna ambayo itazuia serikali kuchukua hatua za makusudi zenye lengo la kurekebisha matatizo mahususi katika jamii
[Maswali ya Msingi: Hivi JK atakapotoa maagizo kwa viongozi wa maeneo ambayo wananchi wamewachagua wabunge wa Chadema ambao walitoka nje ya ukumbi wa Bunge wakati JK akihutubia, sio wote akiwemo JK watakuwa wamevunja katiba? Kuwanyima wananchi huduma au maendeleo kwa sababu ya kuwa na maoni tofauti ya kisiasa, sio kuminya demokrasia huko? Hili likitokea na kuthibitishwa basi, JK apitishiwe azimio la kuondolea madarakani ndani ya Bunge]
Kama JK alivyowaambiwa wabunge wa Chadema wakati akizindua Bunge la 10 la Jamhuri ya Muungano kuwa ndiye Rais na watatoka, watarudi kwake yaani serikalini kutaka msaada.
Katiba inasema:
Ibara ya 13
(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya Mamlaka ya Nchi
(5) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara hii neno kubagua maana yake ni kutimiza haja, haki au mahitaji mengineyo kwa watu mbalimbali kwa kuzingatia utaifa wao, kabila, pahala walipotokea, maoni yao ya kisiasa, rangi, dini, jinsia au hali yao ya maisha kwa namna ambayo watu wa aina Fulani wanafanywa au kuhesabiwa kuwa dhaifu au duni na kuwekewa vikwazo au masharti ya vipingamizi ambapo watu wa aina nyingine wanatendewa tofauti au wanapewa fursa au faida iliyoko nje ya masharti au sifa za lazima, isipokuwa kwamba neno kubagua halifafanuliwa kwa namna ambayo itazuia serikali kuchukua hatua za makusudi zenye lengo la kurekebisha matatizo mahususi katika jamii
[Maswali ya Msingi: Hivi JK atakapotoa maagizo kwa viongozi wa maeneo ambayo wananchi wamewachagua wabunge wa Chadema ambao walitoka nje ya ukumbi wa Bunge wakati JK akihutubia, sio wote akiwemo JK watakuwa wamevunja katiba? Kuwanyima wananchi huduma au maendeleo kwa sababu ya kuwa na maoni tofauti ya kisiasa, sio kuminya demokrasia huko? Hili likitokea na kuthibitishwa basi, JK apitishiwe azimio la kuondolea madarakani ndani ya Bunge]