GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
JK Sahani Moja na Upinzani Hotuba ya Agosti
Watanzania tuna utamaduni wa kushangaa mazuri na kufurahia mabaya kwa kutazama tu anayeyasema ni nani na wakati gani bila kuzingatia anayoyasema yana tija au ni porojo tu za jukwaa kujisafishia mkate wake.
Mpaka leo huwa najiuliza alitoa wapi ujasiri na undumilakuwili ule Mzee wangu Ben katika kampeni za mwisho za CCM pale jangwani 2010 alipoamua bayana kuwatukana wapinzani ati ni wanafiki wakubwa kwa kuhoji serikali imefanya nini kama vile hawana macho.
Ni mwaka tu sasa unakatika hata kauli hii ya Mzee Ben bado haijafutika katika masikio yetu alipoibuka ghafla kutoka Nairobi katika usuluhishi wa ghasia za baada ya Uchaguzi Nchini Kenya ambapo alirejea huku ujio wake ukitanda wingu zito la kashfa ambazo si mahala pake kuzizungumza maana si mintarafu ya makala nayokusudia leo.
Namtazama Mzee Ben kama kioo na chagizo muhimu katika kusaidia kutanzua mkwamo wa kiuchumi Nchini lakini kwa hili nasema hapana tena iliyoshiba huku nikisukumwa sasa na matokeo ya utitiri wa kauli za wanasiasa wenye njaa ambao nao wametumbukia katika mkumbo huu wa kuukebehi upinzani akiwemo mjomba wangu Mzee wa Viwango na Spidi.
Inawezekanaje katika Nchi hii ambayo leo tunaadhimisha miaka hamsini ya Uhuru hali ya miundo mbinu na huduma za kijamii ni duni kuliko maelezo ya kawaida huku tukiendelea kujinasibu kwa nyimbo nyingi nzuuri za kisiwa cha amani na tuna rasilimali nyingi, ambazo kamwe hatujui zinamsaidia nani?
Wenye kuyaona haya mapema wengi wanaishia kutiwa tonge mdomoni na wengine kulambishwa asali na kuusahau shubiri hii ya ukali wa maisha unaowakabili watanzania.
Sishangai Rafiki yangu Mjomba aliyejitahidi kwa kutunga Beti zenye mantiki na ukosoaji wa hali ya juu kwa uozo huu wa serikali na yeye leo tayari domo limejaa zege maneno hayatoki tena baada ya kupewa ulaji na Adui yake Mkubwa mpango wa Malaria ambaye hata pale katika tamasha kubwa la malaria hakumwalika lakini baada ya kelele za wanahabari wakamkumbuka na leo haemi kitu tena zaidi ya kushabikia ujinga.
Akianzia kule TCRA, baadaye Zain na sasa katika dawa butu za Maralia.Kama haitoshi kila ukifunua mdomo kuwaambia watanzania tudai haki yetu kwa nguvu ya Umma maana mazungumzo yameshindikana baadhi ya wenzetu wenye msongo wa mawazo na ufinyu wa fikara bado watakwambia nyie mmezoea vurugu tu hebu iacheni serikali ifanye kazi.
Ashkum si matusi, kazi gani hiyo ambayo bado wanataka kuifanya na wameshindwa kuimaliza katika kipindi cha miaka hamsini isiyokuwa na tija ya kuridhisha, narudia tena tija ya kuridhisha au ni wizi tu na udangayifu kwa umma.
Hakuna sababu tena ya mtanzania kusimama akipinga maandamano ya CDM, hii ndio njia sahihi iliyobakia kuonyesha nini hasa tunahitaji na si porojo na hotuba ndeefu ambazo kila siku zinaediwa kisha copy na paste.
Msingi wa hoja yangu ni hapa kuna fununu kwamba baada ya kimya kirefu Mkuu wa Nchi anajipanga kutoa Hotuba Mwisho wa mwezi huu ikiwa ni sehemu ya kureview na kupoza makali kwa hekaheka nyingi zilizolikumba Bunge la serikali yake kipindi hiki.
Na pengine kutoa mkono wa Iddi kwa waumini wa Dini ya Kiislam.Linalotarajiwa hapa ni mkuu wa Nchi kuzungumza tena kwa ukali huku akijinasibu kwa kuvaa usiriasi usioonekana katika matendo yake zaidi ya kufanya maigizo hayo katika luninga.
Hii haitoshi kwa kuwavaa wapinzani na kusimanga juhudi zao muhimu kabisa za kushinikiza mabadiliko, tunataka kuona huduma za uhakika kwa watanzania wa leo na kwa hakika tunawajibika kuendelea kulipigia hili kelele kupitia Nguvu ya Umma hadi kieleweke.
ADIOS
Ahadi za Bwana Mkubwa hizi hapa: KWA OMBI MAALUM ndani ya Thread
JF Senior Expert Member
Join Date : 22nd October 2009
Location : Mtimbwani
Posts : 500
Rep Power : 23
[h=2]
AHADI - ALIITOA AKIWA WAPI...
- Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora
- Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini
- Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga
- Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga
- Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma
- Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini
- Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma
- Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera
- Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera
- Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini
- Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
- Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera
- Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera
- Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera
- Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya
- Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera
- Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
- Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza
- Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza
- Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita
- Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba
- Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro
- Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini
- Kujenga bandari Kasanga – Rukwa
- Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
- Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya
- Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga
- Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa
- Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro
- Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini
- Kuboresha barabara za Igunga - Tabora
- Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu
- Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini
- Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara
- Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa - Musoma
- Kulinda haki za walemavu - Makete
- Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini
- Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha
- Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
- Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora
- Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini
- Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma
- Kuwafidia wanakijiji ng'ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido
- Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
- Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini
- Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma
- Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido
- Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
- Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara
- Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini
- Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini
- Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa
- Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa
- Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa
- Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi -Ifunda
- Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara
- Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa
- Ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii - Kibandamaiti Mjini Zanzibar
- Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa - Kibandamaiti mjini Zanzibar
- Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti
- Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma
- Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma
- kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma
- Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma
- Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
- Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara
- Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha
- Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa - Kibaha
- Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda - Kibaha