- Thread starter
- #61
Ohh wamekwisha anza!!!...mnyonge mnyongeni haki yake mpeni...nadhani kauli ya JK kila mwenye masikio alisikia na kila mwenye akili timamu alitafsiri kwa upeo wa akili yake . sasa nashangazwa na watu timamu walio makini kulishwa maneno na kutaka jamii iamini kile wanachokiamini wao..ni busara kila mtu apewe nafasi achuje pumba na mchele ni upi. si busara kutaka wote wafanane mitazamo juu ya kauli ya JK coz kila mtu anajua kutafsiri kilichosemwa hivyo si HAKI kumshawishi mtu asimpe kura mgombea yeyote (hata JK) kwa kuwa tu yeye binafsi hakufurahishwa na kitu fulani au kauli fulani (kama mjadala huu ulivyo). nakumbuka alisema yuko radhi kuzikosa kura za wafanyakazi na Mgaya akasema JK kazikataa kura za wafanyakazi...nasi sote tumeingia kwenye malumbano juu ya kauli hizi za JK na Mgaya...kwanini tusitumie busara zetu kuamua mambo?(mf kumpa au kumnyima kura mgombea)...kama hatuwezi basi ijulikane kabisa kuwa hapa kuna namna fulani ya kampeni dhidi ya JK na chama chake..iwekwe wazi ili wachangiaji wajue mada hizi zinatumika kupigia debe chama fulani coz nimeona watu wanachangia kwa ku-base judgement zao kwenye tafsiri moja tu ya kauli ile ( tafsiri ya Mgaya) wakti ambapo kabla mgaya hajazungumza mtazamo huo haukuwepo je ndio kusema watu hawakuelewa kama alivyoelewa mgaya toka mwanzo mpaka alipozungumza? hii inanipa hofu kuwa kuna mengi tutajikuta tunaamua kwa kusikia flani kasema basi nasi tunachukua mtazamo huo kama wetu na kujikuta tunaafanya maamuzi yasiyo sahihi...tubadilike kila mtu awe na mtazamo wake juu ya jambo husika kwa kulifanyia uchunguzi wa kina na ndipo ufanye uamuzi.
So,kila mtu achague kiongozi amtakaye kwa kumsikiliza na kushawishika na sera zake na si kwa kuambiwa na mtu mwingine kama wengine wanavyojaribu kuwaambia wafanyakazi wasimpe kura JK...all in all, maisha yako si ya mwenzako so waweza kushawishi kundi fulani lisimpe kura na mwishowe wakampa nadhani itauma zaidi kwani kura huwa ni siri so huwezi jua, pia unaweza kushawishika kumbe aliekushawishi hana shida kama zako..(ofkoz hatulingani hata kama wote tuna shida)... kila mtu atumie haki yake ya kuchagua kiongozi amtakaye yeye na si kuchagua kwa kuwa wanaJF wachache wameamua huo ndio uwe msimamo wa JF na wafanyakazi walio JF.
Sio wafanyakazi wote wenye kuweza kunyambua kila linalosemwa na sio wote wanaweza kukotoa hesabu za kisanii za serikali hivyo hapa JF watu hatumpigii debe Dr Slaa Professa Lipumba au JK bali tunajaribu kuchambua kila mmoja anasema nini ili mwenye macho afumbuke asiyenayo aendelee kukaa tu kwenye kiza.