kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,213
Kikwete akisema sasa namuamini, Matukio yafuatayo ingawa yalitikisa Nchi, lakini yalikuwa upepo tu na yamepita.
1. Waligoma waalimu na madaktari, watu wakafa wanafunzi wakakosa masomo, hata bila madai yao kushughulikiwa ukawa upepo tu na ukapita.
2. Akakamatwa Ulimboka, akateswa na kukaribia kutolewa uhai, wanaharakati na watanzania wakaja juu, kova akaendesha movie yake, kumbe nao ulikuwa upepo tu na umepita.
3. Wakauawa watu maeneo mbali mbali na polisi kama Arusha, Morogoro na kule Iringa ambapo mwandishi Daudi Mwangosi (RIP) aliuawa na polisi, watu wakapiga makelele sana, wengine wakatishia kuwashitaki viongozi wakuu wa jeshi la polisi The Hague, he.. nao ukawa upepo, umepita, tumemsahau Mwangosi na maisha yanaendelea.
4. Balali, akiwa shahidi mkuu wa wizi ya babilioni kwenye account ya EPA, akatoweka na kwenda kufariki Marekani katika mazingira ya kutatanisha, ingawa mpaka sasa kuna mtu anatweet akijifanya ni Balali lakini labda alikufa. Utata wa kifo chake ulikuwa gumzo kubwa nchini, lakini gumzo hilo lilikuwa upepo tu nao ukapita.
5. Wabungwe wakaomba rushwa, wakajiingiza kwenye biashara na shirika wanalolisimamia, ikaundwa tume ya kuchunguza, kumbe tume yenyewe ilikuwa ni ya kupitisha upepo, wamesafishwa na upepo umepita.
6.Naamini na mtakuja kuniambia, sakata la mabilioni ya Uswiswi ni upepo tu nao utapita.
Najua yapo mengine lakini haya ni moja ya matukio ambayo mwisho wake ulikuwa kama upepo na ukapita, miti ikasimama, maisha yanaendelea.
Watanzania tumekuwa wepesi wa kuacha na kusahau mambo makubwa haraka na kirahisi, nadhani JK anawajua watanzania ndio maana ana uhakika tukio lolote hata liwe kubwa kiasi gani, litasemwa na mwishowe litasahaulika. Alishasema kelele za mlangoooooooo......!!! Ukitaka kulaaaaa............!!! W/end njema.
1. Waligoma waalimu na madaktari, watu wakafa wanafunzi wakakosa masomo, hata bila madai yao kushughulikiwa ukawa upepo tu na ukapita.
2. Akakamatwa Ulimboka, akateswa na kukaribia kutolewa uhai, wanaharakati na watanzania wakaja juu, kova akaendesha movie yake, kumbe nao ulikuwa upepo tu na umepita.
3. Wakauawa watu maeneo mbali mbali na polisi kama Arusha, Morogoro na kule Iringa ambapo mwandishi Daudi Mwangosi (RIP) aliuawa na polisi, watu wakapiga makelele sana, wengine wakatishia kuwashitaki viongozi wakuu wa jeshi la polisi The Hague, he.. nao ukawa upepo, umepita, tumemsahau Mwangosi na maisha yanaendelea.
4. Balali, akiwa shahidi mkuu wa wizi ya babilioni kwenye account ya EPA, akatoweka na kwenda kufariki Marekani katika mazingira ya kutatanisha, ingawa mpaka sasa kuna mtu anatweet akijifanya ni Balali lakini labda alikufa. Utata wa kifo chake ulikuwa gumzo kubwa nchini, lakini gumzo hilo lilikuwa upepo tu nao ukapita.
5. Wabungwe wakaomba rushwa, wakajiingiza kwenye biashara na shirika wanalolisimamia, ikaundwa tume ya kuchunguza, kumbe tume yenyewe ilikuwa ni ya kupitisha upepo, wamesafishwa na upepo umepita.
6.Naamini na mtakuja kuniambia, sakata la mabilioni ya Uswiswi ni upepo tu nao utapita.
Najua yapo mengine lakini haya ni moja ya matukio ambayo mwisho wake ulikuwa kama upepo na ukapita, miti ikasimama, maisha yanaendelea.
Watanzania tumekuwa wepesi wa kuacha na kusahau mambo makubwa haraka na kirahisi, nadhani JK anawajua watanzania ndio maana ana uhakika tukio lolote hata liwe kubwa kiasi gani, litasemwa na mwishowe litasahaulika. Alishasema kelele za mlangoooooooo......!!! Ukitaka kulaaaaa............!!! W/end njema.