Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,786
- 1,710
Na Mwandishi wetu
Raia Mwema
Septemba 15-21 (Ukurasa wa Tatu)
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Kigoma, Moudline Castico, aliyedaiwa kupigania chama hicho kutomteua mgombea ubunge anayehusishwa na kashfa za mauaji ya albino na ujambazi, amehamishiwa makao makuu ya CCM, mjini Dodoma, Raia Mwema limebaini.
Taarifa za uhakika zinasema kuwa Castico alipewa barua ya uhamisho saa sita za usiku siku ambayo mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete alifika Kigoma kwa ajili ya kampeni.
Katika moja ya matoleo ya gazeti hili, hasa baada ya kuhitimishwa mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, Dodoma uliopitisha wagombea ubunge na udiwani, liliripoti kupitishwa mgombea ubunge mwenye kashfa ya mauaji ya albino na ujambazi katika Jimbo la Muhambwe, Kibondo (Jamal Tamim)
Katika habari hiyo, gazeti hili liliripoti habari za ndani kuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Kigoma ndiye aliyeongoza hoja za kumpinga mgombea huyo, akirejea mazingira halisi ya Jimbo anakogombea Jamal Tamim.
Kwa mujibu wa habari hiyo ya ndani ya NEC-CCM, Katibu huyo alilazimika kutoa maelezo kwa nini mgombea husika asipitishwe. Anadaiwa kutoa maelezo hayo wakati wa mikutano wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kibondo na ya Mkoa wa Kigoma.
Katika mkutano wa mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, anadaiwa kuwasilisha ripoti iliyochambua madhambi ya mgombea husika.
Hata hivyo katika mkutano huo wa NEC , mjumbe mmoja kutoka Kigoma anatajwa kumtetea Jamal Tamim (ambaye ana asili ya kiasia) ambaye anaungwa mkono na wafanyabiashara wakubwa mkoani Kigoma (kwa motisha gani????) ambao maadili yao yana utata. Pia mgombea huyo anaungwa mkono na mfanyabiashara na mwanasiasa maarufu mkoani Tabora ambaye ni mjumbe wa NEC [Rostam Aziz (asili ya kiasia na mfanyabiashara pia)].
Ikiwa imepita miezi takriban miwili sasa, taarifa za hivi karibuni kutoka Kigoma zinabainisha kuwa kile kinachoelezwa kuwa ni 'fitina' za kundi la wafanyabiashara; hasa wenye utata kimaadili, limepambanua kutumia ushawishi wa 'mtandao' kumng'oa katibu huyo Kigoma.
Baada ya kupewa barua ya uhamisho, Katibu huyo anadaiwa kutengenezewa zengwe jingine kwamba alijaribu kubadilisha majina ya wagombea saba wa udiwani, Jimbo la Kigoma mjini akikwaruzana na mgombea ubunge, Peter Serukamba.
Habari kutoka ndani ya CCM Kigoma zinadai kuwa Katibu huyo aling'olewa kutokana na kujaribu kusaidia kuleta vurugu kwa kushawishi kamati za maadili na kamati za siasa kuwaengua na kuwapa alama za chini wagombea walioongoza kwenye kura za maoni. Anadaiwa kudhamiria kuwaengua wagombea zaba wa udiwani Manispaa ya Kigoma Ujiji na kuwaweka washindi wa pili na tatu katika kata za watu hao waliokusudiwa kuenguliwa.
Hata hivyo gazeti hili liliwasiliana na Katibu huyo ambaye alithibitisha kuhamishwa kutoka Kigoma hadi Dodoma lakini akipinga madai mengine dhidi yake.
"Sio ajabu kuhamishwa, ni masuala ya kazi. Kuhusu kujaribu kupangua madiwani hilo ni suala la vikao si la kwangu .... sio suala la mtu binafsi. Wanaosema hivyo hawajui chama kinaongozwa vipit.
"Wananisema kwa sababu wanajua mimi ni mwanasiasa na kiongozi bora, ninayesimamia kazi kikamilifu. Simwogopi mtu yeyote wala sifanyi siasa za makundi. Namwogopa Mungu tu. Nimeonyesha uwezo wangu wa kazi Kigoma na kwingine na ndiyo maana nabadilishwa kazi kutokana na utendaji mzuri. Na kwa sababu wananihusisha kwenye mambo yao kwa nia wanazozijua hiyo inazidi kunijenga kiuongozi maana yake kuna mambo ya msingi nayasimamia bila kujali siasa za makundi,
"Ukiona wanakuandama au kukujadili kila wanapokutana ujue una thamani fulani ya kiuongozi ambayo labda wao hawana," alijibu Katibu huyo wa zamani wa Kigoma katika mazungumzo yake na mwandishi wa gazeti hili.
Lakini wakati majibu ya kigogo huyo yakiwa hayo, taarifa zaidi kutoka Kigoma zinaeleza kuwa kiongozi huyo alikuwa akimpigania mbunge (Kijiko) aliyemaliza muda wake katika Jimbo la Muhambwe ambalo CCM imemteua Jamal Tamim anayetuhumiwa kwa mauaji ya maalbino na matukio ya ujambazi.
Inadaiwa kuwa kiongozi huyo aliyehamishwa alikuwa akiungwa mkono na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, John Mongela, katika kuhakikisha mgombea ubunge mwenye kashfa za mauaji ya maalbino na ujambazi hagombei kwa tiketi ya CCM ili kunusuru ushindi wa chama hicho.
Lakini wakati mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya na kiongozi huyo aliyehamishwa wakitajwa wakati wa kura za maoni kuhakikisha Jamal Tamim hachaguliwi, Mwenyekiti wa CCM Kigoma, Azim Premji (mfanyabiashara pia mwenye asili ya kiasia) na mjumbe wa NEC-CCM, Muhsin Abdallah Sheni (mfanyabiashara tajiri mwenye asili ya kiasia na maadili yenye mashaka) walitajwa kumtetea Jamal Tamim (mwenye nguvu ya pesa zenye kutiliwa mashaka, mwenye asili ya kiasia pia) kwenye vikao mbalimbali kwa wakati huo.
Mgombea huyo anayetetewa na Premji pamoja na Muhsin Sheni huku akipingwa na Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya, kwa kuzingatia taarifa za Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Mkoa, anadaiwa pia kuwa amewafungulia mashtaka viongozi wa dini na kujikuta katika mgogoro mzito uliovuka mipaka kutoka kwa viongozi wa dini hadi wapiga kura.
Viongozi hao wamekuwa wakimtetea Jamal (muasia mwenzao, na mwenye pesa kama wao) ndani ya NEC kwa hoja kuw kama angekuwa anahusika na mauaji ya maalbino au matukio ya ujambazi, basi viongozi wa dola akiwemo Mkuu wa Mkoa, Simbakalia wangepaswa kumchukulia hatua lakini hawakufanya hivyo.
Lakini wakati hayo yakiendelea, taarifa kutoka jimbo anakogombea mtuhumiwa huyo zinabainisha kuwa mgombea husika amewashtaki Padre wa Kanisa Katoliki ambaye ni Paroko wa Parokia ya Mabamba, Padre Adrian Jimenez, pamoja na kiongozi wa kiislam Maalim wa Madrasa ya Mabamba kwa madai ya kumkashifu.
Tukio hilo la kufunguliwa kwa kesi hizo linatajwa kuibua mgogoro mkubwa kati ya mgombea huyo na viongozi wa dini, ikielezwa kuwa mgogoro huo sasa umevuka mipaka na wananchi wanaunga mkono viongozi wao wa dini.
Katika hatua nyingine, habari zaidi za uhamisho wa Katibu wa CCM Kigoma, Castico zinabainisha kuwa alipewa barua ya uhamisho kwenda kuripoti makao makuu ya CCM Dodoma saa sita usiku, siku ya mkutano wa kampeni ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete mkoani Kigoma.
Chanzo chetu cha habari kinaeleza kuwa kabla ya kikao cha NEC-CCM na hasa baada ya kupata taarifa ya mvutano uliokuwapo Kigoma, Jakaya Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa CCM Taifa aliwaita Dar es Salaam viongozi watatu wa CCM Kigoma ambao wanaingia kwenye kikao cha NEC-Taifa ili kuzungumzia mwenendo wa zilizokuwa kura za maoni ndani ya chama chao Kigoma. Viongozi hao waliokutana na Kikwete kwa wakati huo ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Kigoma, Azim Premji, Katibu wa Mkoa, Castico, na Mjumbe wa NEC, Muhsin Abdallah Sheni.
Raia mwema iliwasiliana na Mwenyekiti wa CCM Kigoma, Azim Premji kuhusu uhamisho wa katibu huyo na masuala mengine anayohusishwa kuyafanya na hatima ya CCM katika Jimbo la Muhambwe ambalo wanadaiwa kumteua mgombea ubunge mwenye elimu ya darasa la saba na mtuhumiwa wa mauaji ya maalbino ambaye alipendekezwa katika kura zaa maoni zilizoendeshwa na serikali kubaini wauaji na wauzaji wa viungo vya albino.
Katika majibu yake kuhusu uhamisho wa Katibu huyo, Premji alisema huo ni uhamisho wa kawaida na kwamba yeye si mtu wa kwanza kuhamishwa kituo cha kazi.
"Suala la kumhamisha kiongozi ni la kawaida, pengine imetokea anahitajika zaidi huko alikopelekwa lakini hakuna matatizo hapa." (!!!!!!!????????) Kampeni zinakwenda vizuri."
Alipoulizwa kuhusu mgombea mtuhumiwa wa mauaji ya maalbino na ujambazi, ambaye pia ameingia katika mgogoro na viongozi wa dini kwamba mazingira yanaweza kikinyima ushindi CCM, alisema hilo ni suala lake binafsi (Jamal) na si la chama. (!!!!!!!!!???????)
"Mgombea wa Muhambwa kuwa na matatizo na viongozi wa dini ni lake binafsi, chama hakinga mgogoro na tunaamini tutapata kura (my comment: kwa rushwa???) na viongozi wa dini kwa sababu ni watu wazima wanajua. Ni suala lake binafsi, haliwezi kuathiri kampeni" alisema.
Raia Mwema
Septemba 15-21 (Ukurasa wa Tatu)
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Kigoma, Moudline Castico, aliyedaiwa kupigania chama hicho kutomteua mgombea ubunge anayehusishwa na kashfa za mauaji ya albino na ujambazi, amehamishiwa makao makuu ya CCM, mjini Dodoma, Raia Mwema limebaini.
Taarifa za uhakika zinasema kuwa Castico alipewa barua ya uhamisho saa sita za usiku siku ambayo mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete alifika Kigoma kwa ajili ya kampeni.
Katika moja ya matoleo ya gazeti hili, hasa baada ya kuhitimishwa mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, Dodoma uliopitisha wagombea ubunge na udiwani, liliripoti kupitishwa mgombea ubunge mwenye kashfa ya mauaji ya albino na ujambazi katika Jimbo la Muhambwe, Kibondo (Jamal Tamim)
Katika habari hiyo, gazeti hili liliripoti habari za ndani kuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Kigoma ndiye aliyeongoza hoja za kumpinga mgombea huyo, akirejea mazingira halisi ya Jimbo anakogombea Jamal Tamim.
Kwa mujibu wa habari hiyo ya ndani ya NEC-CCM, Katibu huyo alilazimika kutoa maelezo kwa nini mgombea husika asipitishwe. Anadaiwa kutoa maelezo hayo wakati wa mikutano wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kibondo na ya Mkoa wa Kigoma.
Katika mkutano wa mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, anadaiwa kuwasilisha ripoti iliyochambua madhambi ya mgombea husika.
Hata hivyo katika mkutano huo wa NEC , mjumbe mmoja kutoka Kigoma anatajwa kumtetea Jamal Tamim (ambaye ana asili ya kiasia) ambaye anaungwa mkono na wafanyabiashara wakubwa mkoani Kigoma (kwa motisha gani????) ambao maadili yao yana utata. Pia mgombea huyo anaungwa mkono na mfanyabiashara na mwanasiasa maarufu mkoani Tabora ambaye ni mjumbe wa NEC [Rostam Aziz (asili ya kiasia na mfanyabiashara pia)].
Ikiwa imepita miezi takriban miwili sasa, taarifa za hivi karibuni kutoka Kigoma zinabainisha kuwa kile kinachoelezwa kuwa ni 'fitina' za kundi la wafanyabiashara; hasa wenye utata kimaadili, limepambanua kutumia ushawishi wa 'mtandao' kumng'oa katibu huyo Kigoma.
Baada ya kupewa barua ya uhamisho, Katibu huyo anadaiwa kutengenezewa zengwe jingine kwamba alijaribu kubadilisha majina ya wagombea saba wa udiwani, Jimbo la Kigoma mjini akikwaruzana na mgombea ubunge, Peter Serukamba.
Habari kutoka ndani ya CCM Kigoma zinadai kuwa Katibu huyo aling'olewa kutokana na kujaribu kusaidia kuleta vurugu kwa kushawishi kamati za maadili na kamati za siasa kuwaengua na kuwapa alama za chini wagombea walioongoza kwenye kura za maoni. Anadaiwa kudhamiria kuwaengua wagombea zaba wa udiwani Manispaa ya Kigoma Ujiji na kuwaweka washindi wa pili na tatu katika kata za watu hao waliokusudiwa kuenguliwa.
Hata hivyo gazeti hili liliwasiliana na Katibu huyo ambaye alithibitisha kuhamishwa kutoka Kigoma hadi Dodoma lakini akipinga madai mengine dhidi yake.
"Sio ajabu kuhamishwa, ni masuala ya kazi. Kuhusu kujaribu kupangua madiwani hilo ni suala la vikao si la kwangu .... sio suala la mtu binafsi. Wanaosema hivyo hawajui chama kinaongozwa vipit.
"Wananisema kwa sababu wanajua mimi ni mwanasiasa na kiongozi bora, ninayesimamia kazi kikamilifu. Simwogopi mtu yeyote wala sifanyi siasa za makundi. Namwogopa Mungu tu. Nimeonyesha uwezo wangu wa kazi Kigoma na kwingine na ndiyo maana nabadilishwa kazi kutokana na utendaji mzuri. Na kwa sababu wananihusisha kwenye mambo yao kwa nia wanazozijua hiyo inazidi kunijenga kiuongozi maana yake kuna mambo ya msingi nayasimamia bila kujali siasa za makundi,
"Ukiona wanakuandama au kukujadili kila wanapokutana ujue una thamani fulani ya kiuongozi ambayo labda wao hawana," alijibu Katibu huyo wa zamani wa Kigoma katika mazungumzo yake na mwandishi wa gazeti hili.
Lakini wakati majibu ya kigogo huyo yakiwa hayo, taarifa zaidi kutoka Kigoma zinaeleza kuwa kiongozi huyo alikuwa akimpigania mbunge (Kijiko) aliyemaliza muda wake katika Jimbo la Muhambwe ambalo CCM imemteua Jamal Tamim anayetuhumiwa kwa mauaji ya maalbino na matukio ya ujambazi.
Inadaiwa kuwa kiongozi huyo aliyehamishwa alikuwa akiungwa mkono na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, John Mongela, katika kuhakikisha mgombea ubunge mwenye kashfa za mauaji ya maalbino na ujambazi hagombei kwa tiketi ya CCM ili kunusuru ushindi wa chama hicho.
Lakini wakati mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya na kiongozi huyo aliyehamishwa wakitajwa wakati wa kura za maoni kuhakikisha Jamal Tamim hachaguliwi, Mwenyekiti wa CCM Kigoma, Azim Premji (mfanyabiashara pia mwenye asili ya kiasia) na mjumbe wa NEC-CCM, Muhsin Abdallah Sheni (mfanyabiashara tajiri mwenye asili ya kiasia na maadili yenye mashaka) walitajwa kumtetea Jamal Tamim (mwenye nguvu ya pesa zenye kutiliwa mashaka, mwenye asili ya kiasia pia) kwenye vikao mbalimbali kwa wakati huo.
Mgombea huyo anayetetewa na Premji pamoja na Muhsin Sheni huku akipingwa na Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya, kwa kuzingatia taarifa za Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Mkoa, anadaiwa pia kuwa amewafungulia mashtaka viongozi wa dini na kujikuta katika mgogoro mzito uliovuka mipaka kutoka kwa viongozi wa dini hadi wapiga kura.
Viongozi hao wamekuwa wakimtetea Jamal (muasia mwenzao, na mwenye pesa kama wao) ndani ya NEC kwa hoja kuw kama angekuwa anahusika na mauaji ya maalbino au matukio ya ujambazi, basi viongozi wa dola akiwemo Mkuu wa Mkoa, Simbakalia wangepaswa kumchukulia hatua lakini hawakufanya hivyo.
Lakini wakati hayo yakiendelea, taarifa kutoka jimbo anakogombea mtuhumiwa huyo zinabainisha kuwa mgombea husika amewashtaki Padre wa Kanisa Katoliki ambaye ni Paroko wa Parokia ya Mabamba, Padre Adrian Jimenez, pamoja na kiongozi wa kiislam Maalim wa Madrasa ya Mabamba kwa madai ya kumkashifu.
Tukio hilo la kufunguliwa kwa kesi hizo linatajwa kuibua mgogoro mkubwa kati ya mgombea huyo na viongozi wa dini, ikielezwa kuwa mgogoro huo sasa umevuka mipaka na wananchi wanaunga mkono viongozi wao wa dini.
Katika hatua nyingine, habari zaidi za uhamisho wa Katibu wa CCM Kigoma, Castico zinabainisha kuwa alipewa barua ya uhamisho kwenda kuripoti makao makuu ya CCM Dodoma saa sita usiku, siku ya mkutano wa kampeni ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete mkoani Kigoma.
Chanzo chetu cha habari kinaeleza kuwa kabla ya kikao cha NEC-CCM na hasa baada ya kupata taarifa ya mvutano uliokuwapo Kigoma, Jakaya Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa CCM Taifa aliwaita Dar es Salaam viongozi watatu wa CCM Kigoma ambao wanaingia kwenye kikao cha NEC-Taifa ili kuzungumzia mwenendo wa zilizokuwa kura za maoni ndani ya chama chao Kigoma. Viongozi hao waliokutana na Kikwete kwa wakati huo ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Kigoma, Azim Premji, Katibu wa Mkoa, Castico, na Mjumbe wa NEC, Muhsin Abdallah Sheni.
Raia mwema iliwasiliana na Mwenyekiti wa CCM Kigoma, Azim Premji kuhusu uhamisho wa katibu huyo na masuala mengine anayohusishwa kuyafanya na hatima ya CCM katika Jimbo la Muhambwe ambalo wanadaiwa kumteua mgombea ubunge mwenye elimu ya darasa la saba na mtuhumiwa wa mauaji ya maalbino ambaye alipendekezwa katika kura zaa maoni zilizoendeshwa na serikali kubaini wauaji na wauzaji wa viungo vya albino.
Katika majibu yake kuhusu uhamisho wa Katibu huyo, Premji alisema huo ni uhamisho wa kawaida na kwamba yeye si mtu wa kwanza kuhamishwa kituo cha kazi.
"Suala la kumhamisha kiongozi ni la kawaida, pengine imetokea anahitajika zaidi huko alikopelekwa lakini hakuna matatizo hapa." (!!!!!!!????????) Kampeni zinakwenda vizuri."
Alipoulizwa kuhusu mgombea mtuhumiwa wa mauaji ya maalbino na ujambazi, ambaye pia ameingia katika mgogoro na viongozi wa dini kwamba mazingira yanaweza kikinyima ushindi CCM, alisema hilo ni suala lake binafsi (Jamal) na si la chama. (!!!!!!!!!???????)
"Mgombea wa Muhambwa kuwa na matatizo na viongozi wa dini ni lake binafsi, chama hakinga mgogoro na tunaamini tutapata kura (my comment: kwa rushwa???) na viongozi wa dini kwa sababu ni watu wazima wanajua. Ni suala lake binafsi, haliwezi kuathiri kampeni" alisema.