JK na AMERICAN SUBPRIME MORTGAGES

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835


HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, 31 JANUARI, 2008


Ndugu Wananchi;
Jambo la pili ninalopenda kulizungumzia ni matatizo yanayoukabili uchumi wa dunia hivi sasa..........Tatizo lingine kubwa linaloukabili uchumi wa dunia sasa linatokana na matatizo yanayoukabili uchumi wa Marekani. Uchumi wa taifa hilo ambao ndiyo mkubwa kuliko wowote duniani umekuwa unapita kwenye misukosuko kwa miezi kadhaa na katika wiki chache zilizopita hali ikawa ngumu zaidi. Kasi ya ukuaji wa uchumi imepungua na thamani ya dola imeshuka. Serikali ya nchi hiyo imeanza kuchukua hatua za kukabiliana na matatizo hayo. Lakini, kwa kuwa uchumi wa Marekani ndiyo uchumi mkubwa kuliko wowote duniani na uchumi wa nchi nyingi duniani una uhusiano nao, matatizo ya uchumi wa nchi hiyo huathiri nchi nyingi. Na sisi Tanzania hivyo hivyo.

Nimeelekeza wachumi wetu wafanye uchambuzi wa kina juu ya athari hizo na kushauri hatua za kuchukua kupunguza makali yake. Moja ya jambo ambalo liko wazi ni lile la kushuka kwa thamani ya dola ya Kimarekani. Sisi tunaweka sehemu kubwa ya akiba yetu ya fedha za kigeni katika dola za Kimarekani. Ni dhahiri kwamba kushuka kwa thamani ya dola za Kimarekani kunatupunguzia uwezo wetu wa kuagiza bidhaa nchi za nje.





Once again mzee wa Pamba aka JK akisaidiwa na maspeech writers wake anataka kulink shida za waTanzania za maji machafu, na huduma mbovu za jamii kwa SUBPRIME MORTAGES MELTDOWN IN THE USA na hiyo RECESSION inayosadikiwa huko.

Maswali kwa JK:


CREDIT CRUNCH YA USA INAHUSIANA VIPI NA WATANZANIA KUKOSA BARA BARA ZA MAANA?
(mfano bara bara ya Kagera haipitiki wiki ya pili sasa)

DSC06074.jpg



US RECESSION INAHUSIANA VIPI NA WATANZANIA AMBAO WAMEOPT KUTUMIA BANDARI YA MOMBASA BADALA YA DAR?
Bandari yetu imejaa urasimu kuliko ya Mombasa na hali inafanya kuwa mbaya na TRA ambao serikali yako umetumia mamilioni kuwasomesha lakini hawajui tofauti ya TV na MONITOR YA COMPUTER)
os17.jpg




SUBPRIME MORTGAGES INAHUSIANA VIPI NA HAWA WAZEE KUKOSA MAFAO YAO?
(wazee wa Jumuiya hawajalipwa mafao yao mpaka leo)

march7-1.jpg




JK UNAPOSEMA KUWA UMEWAAGIZA WACHUMI WAKO WAFANYE UCHAMBUZI WA KINA WA HIYO RECESSION AMBAYO IPO KAMA VILE HAIPO NA MAMBO YA CREDIT CRUNCHS SIKUELWEI
(Je huyu jamaa atakuelewa unachosema?)
os11-1.jpg



MHESHIMIWA RAIS HUNA HAJA YA KUWAPA MAAGIZO HAO WATU BALI HIYO NI KAZI YAO NA WALITAKIWA WASHA PREDICT GLOBAL ECONOMY ITAKAVYOKUWA IN 2008


KAZI YA RAIS KAZI YAKO SIYO KUDELEGATE HAO WASHAURI WAKO KUHUSU GLOBAL ECONMIC TRENDS

HIYO NI KATIKA JOB DESCRIPTION YAO NA ILITAKIWA HIZO RIPOTI TAYARI WALISHAZIWAKILISHA KWAKO.

THE SAME KAMA GW BUSH NA OF COURSE BERNAKE NA PAULSON KILA KUKICHA WANAASHUSHA HIZO INTEREST RATES

MHESHIMIWA UKITAKA NIANZE KUKUTAKE SERIOUS PUNGUZA BARAZA LA MAWAZIRI TOKA 60 NITAKUONA UNA NIA YA KUTUOKOA KIUCHIMU NA SIYO KUJA NA SPEECH AMBAZO JAMAA ZAKO WANA CUT AND PASTE ARTICLES TOKA GAZETI LA ECONOMIST


(Je huoni hatuna umuhimu wa haya ma VX? Je unajua hayo ma VX 60 yangejenga kilomita ngapi kule Mafia?


ST2.jpg

st1.jpg

(Baraza lako la mawaziri ni 60 NA kila waziri kapewa gari dizaini hii ambalo si chini ya milioni 60 sasa hebu justify hili nalo)


 
GT,

Hayo mashangingi sii tu kwa mawaziri pekee! Kila Wizara au Idara ya Serikali ina Wakurugenzi watano au zaidi na kila Mkurugenzi hupewa shangingi na dereva kumtoa Osterbay kumleta Ofsini! Pia Majaji wote hupewa haya mashangingi! Wakuu wa Vyuo, na taasisi zote za serikali.
Pia Wakuu wote wa Mikoa, RAS Wote, Wakurugenzi na Wakuu wote wa Wilaya hupewa haya mashangingi! Tunaongea kama mashangingi kama 5,000 au zaidi.

Gharama kubwa sii hii ya kununua Mil. 60 au 70 (Bila VAT)- ila matengenezo na mafuta. Mfano Lita moja shangingi hutumia km 5 na toka Dar to Arusha na kurudi ni ni 1400 km- hizi ni lita 280 * 1500 ni shilingi 420,000. Bado service na tairi. Sasa Waziri akiwa na trip za mikoani 30 kwa mwaka mafuta tu ni 15,000,000. Kwa hiyo hii gari kwa miaka mitano mafuta ni 75,000,000! Bado spare parts na bado kumlipa dereva!

Ndo maana tukisema Tz ni maskini wakati Viongozi wanatanua hivi- is this a fair presetation?

Yet majority ya Watz wanateseka bila barabara Kigoma?

Is this fair?
 
Thank you GT,

Well done, Nimeipenda sana hii na moja kwa moja inaingia kwenye kitabu changu cha kumbukumbu. Huyu JK anahitaji kwanza apelekwe shule kwa muda wakati ili afundishwe hata kwa lazima kitu cha kufanya.

MUNGU ibariki JF!
 
Angalia vizuri hiyo picha ya barabara palipokwama magari huko Kagera; angalia pembezoni mwa barabara hiyo.

Unapomwambia mtu atokae nchi za jangwa kama Misri, Israel na kwingineko duniani kuwa kuna watu wanakaribia kufa njaa katika nchi kama hii, inaonekana kama wananchi wake na viongozi wao wana laana.
 
JK msanii tuu na atasema chochote ili mradi awafurahishe au alaumu wengine kwa matatizo yake,sasa anakuja kutuambia njaa zetu ni credit crunch za wall street hapo wapi na wapi mjomba mbona tunafanyana watoto? sasa hivi anatuambia akiba kubwa yetu iko kwenye $$ anyway ningekuwa mshauri wake ningefanya wanachofanya Benki kuu zote ... balance btn $$$ & gold maana hivi vitu viko indirect kimoja kikipanda kingine kinashuka and vice versa ndio maana sasa $$$ iko all time low na gold iko all time high lakini aache usanii kulink wall street na matatizo yetu yanayotokana na ufisadi.
 
GT, Thank you Bruv!!

Amazing factual recollections, amazing evidence of thinking slackness on part of our leaders, pictorial perspective evident to our leaders' inactions.

GT, you have presented solid arguments. I am really proud of you being a member here despite of our minor differences expectedly of any beings.

Simply, GREAT! BRAVO!


SteveD.
 
GT udumu, na wale ambao wanapenda kusema kuwa unaleta udaku waseme sasa.

Lakini kwa kweli JK kuhusisha mortgage crunch iliyopo marekani kuathiri uchumi wa Tanzania? Give me a break. Angejua kuwa ni wahuni tu ndio walikuwa wanawatapeli watu kuwapa mikopo hewa, na sasa FBI wanakula nao sahani moja raisi mzaima kapata kisingizio AIBU.

Au ndiyo mazoezi ya speech za kumsomea Goerge Kichaka ... naona wanafanya warm up!
 
Jamani, mnataka raisi wetu aseme hadharani kuwa yeye ndiye ameshindwa kuongoza nchi kuiondoa kwenye matatizo hayo? Je atakuwa "mwanasiasa wa Tanzania aliyebobea" kweli?
 
Jamani, mnataka raisi wetu aseme hadharani kuwa yeye ndiye ameshindwa kuongoza nchi kuiondoa kwenye matatizo hayo? Je atakuwa "mwanasiasa wa Tanzania aliyebobea" kweli?

Kichuguu,
... kamwe hatutegemei yeye kutaja hilo. Ila tungelitegemea Rais huyu awe mfano bora Africa na Ulimwenguni kote kwa kuonyesha vitendo na si kusema tuu! Ni rais ambaye ameingia kwenye ngwee yake na kukuta madhambi kibao, lakini pia madhambi na utomvu wa nidhamu kibao umetendeka katika kipindi kifupi alichokuwa Rais.

Inaction yake ya kutosafisha utomvu huu na udhalim alioukuta na unaoendelea kutendeka ndiyo kunatupelekea sisi kusema haya, ama kweli, kama usemavyo, yakifanyika tunayopenda badala ya 'tunayotarajia', huyo atakuwa siyo 'mwanasiasa aliyebobea'!!!

SteveD.
 
My reaction from the speech of Mr President J.Kikwete. Kwanza kabisa I am so please to get this chance to provides answers from Mr president speech.

First, Mfumo mbovu ndani ya wizara ya mambo ya ndani kupitia kitengo chake cha uhamiaji kimesababisha madhara haya yote ya uhamiaji ndani ya Tanzania. Mipaka yetu iko wazi pasipo ulinzi wa aina yoyote, wakati viongozi wetu wanazidisha zogo kuhusu wahamiaji hawa wanaingiaje. Swala la rushwa ndani ya uhamiaji limesababisha watu wengi kuishi kinyume ndani ya nchi. Hii ni pamoja na vigogo wapya wa TTCL ambao wameanza kazi pasipo vibali, vile vile raia wengi wa bara la Asia wameweza kuishi ndani ya nchi pasipo vibali halali vya kuishi. Swali langu ni nini kinafanyika kuenforce kwa raia hawa wangi waishio miji mikuu ya Tanzania? Awali ya hayo nampongeza muheshiwa rahisi kwa kugusa swala la wakimbizi ndani ya nchi.

second issue, World economy is intergrated in global manner as Mr President elaborated, however kuongezeka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia hakuna effect kubwa sana katika nchi ambazo sitegemezi katika mafuta. Ni uweleo wangu kwamba Tanzania economy is relied on Agricalture for more than 50%, na wakulima hawa majority wanatumia jembe la pilau au mkono basi kuongezeka kwa bei ya mafuta hakuna much effect in our economy. Tanzania use mafuta sana kwenye cormercial uses and not business uses. So increases of gas price will affect individual people more than whole economy. Hii inadhihirisha ni kiasi gani wachumi wa muheshimiwa raisi wana focus more kwenye factor za uchumi wa marekani than their own economy.

Tatu, swala la kusema uchumi wa marekani umekwenda chini, na uchumi wa marekani unaffiliate na world economy it's misinterplation of the real meaning. America economy inaaminika umekubwa na tatizo la subprime mortagage. Mortgage ina contribute about 47% of the total US economy, less than 5% of home owner are not capable to make their month payments, which cause this crisis to landers. Go to the point ya USA economy, uchumi wa marekani bado una contribute about 43% of the world market. Majority of index in the world are still bring more return, that includes S&P 500, Nikkei index, Russell 2000 and many others are still bring giantic returns, so all MR JK said is full of CNN and MSNBC lies. Kushuka kwa dolla kumeongeza nchi nyingi duniani kuinvest katika US market. Vile vile uchumi wa Tanzania ni mdogo sana kuweza kuathirika kwa kushuka kwa dolla, sababu hakuna vitu vingi tunavyouza kwenye soko la dunia, the different side ni kwamba consumer in Tanzania are benefit more from goods coming from USA.

Swala la Bank Kuu, muheshimiwa Raisi J. Kikwete ameshindwa kuzungumza lolote la maana kuhusu bank kuu, alichoweza kuelezea ni kuwataka watu wafumbie macho kuhusu swala zima la Bank Kuu. Muheshimiwa ameshindwa kujibu tuhuma za US embassy kuitaka serikali ya Tanzania kumuomba Balali awe deported kutoka US kurudi Tanzania ili aface Justice. Vile vile muheshimiwa ajazungumzia lolote kuhusu why report ya Enerst & Young hajawekwa public so every Tanzania could benefit from analysis.

Last, muheshimiwa ameonyesha kutufundisha watanzania kufikiria kuhusu nini tufanye pindi muheshimiwa G.W. Bush atakapofika. Ni haki ya watanzania kuwa na freedom of speech pasipo vizingiti vyovyote, vile vile ni haki ya watanzania kusema lolote kwa muheshimiwa rais wa marekani bila kuvunja mipaka ya kisheria. Hii iwe ni kumuomba muheshimiwa G. Bush kusitisha misaada kwa Tanzania au iwe ni kumuomba kuongeza scholarship kwa watanzania. Imefika muda muheshimiwa ache kutupangia nini wananchi tufanye.

Mwisho, speech ya muheshimiwa bado haijazungumzia lolote, kuhusu ni mbinu gani mbadala zitakazo wasaidia wadau wa Tanzania, ni vugu vugu gani analotumia kuzuia Rushwa ndani ya serikali yake. Ni kwanini anazidi kuwafunika mawaziri ambao wamekula rushwa na kuitia Tanzania katika Billion of dollar loss.
 
Asante sana mtanzania kwa uchungu uliokuwa nao, tuko pamoja baba
Nadhani watanzania wamepigwa sindano ya Ganzi, ebu angalia hiyo mifano michache iliyoorodheshwa hapo juu, na uangalie tabu zinavyotupata, lakini bado tu utakuta 2010 barabara zinapitika kwa miezi miwili watu wanapewa Vijitishert, na Kanga, na 500/Tsh, then wanasahau haya Matatizo yote jamani
Hivi tuanzie wapi kuelimisha jamii kuhusu huu uchafu wa Serikali hii jamani
Watanzania amkeni jamani, tunaibiwa jamani tukiwa macho, na Maela yanahamishiwa Mabenki ya Nje huko, jamani jamani, amkeniiiiiiiiiiii!!!

MABUBU YA KISEMA NA VIZIWI WAKISIKIA,KUTAKUA KAMA KENYA
 
GT,

Hii kali sana, yaani jamaa badala ya kuja na ubunifu wa kutatua matatizo yetu, wao kazi kuangalia taarifa za habari ili wapate ya kuandika kwenye hotuba?

Bila mawazo mapya na mabadiliko (change) hapo wananchi wataendelea kufungwa magoli tu.

Hiyo ardhi inaelekea ina rutuba kweli kweli lakini bado wananchi wetu wanasumbuka hata kupata vyakula. Tuna safari ndefu kweli kweli.

Wengine tukiomba hata kazi ya kuwa katibu kata na kwenda kuleta mabadiliko, hawataki, eti mpaka uwe kijana mpaka ndani ya mwili.
 
I am waiting for his next hotuba

---baada ya ile ya Bungeni kuhusiana na EPA, sasa karudi kule kule kwenye subprime mortgages kama chanzo cha ulalahoi wa Watanzania akiwa kwenye hiyo controversial ziara yake mkoani Mbeya!
 
''Nimeelekeza wachumi wetu wafanye uchambuzi wa kina juu ya athari hizo na kushauri hatua za kuchukua kupunguza makali yake''.

...Miezi tisa baada ya kuwapa maelekezo hayo,wamekuja na mapendekezo gani?
See for yourself.


The chairman of the African Union has appealed against any cut in aid following the global financial crisis.

Jakaya Kikwete, who is also president of Tanzania, said his country and other developing states were "deeply concerned" about the crisis.

"Skyrocketing oil and food prices" were also a worry, he said.

Experts say Africa is relatively sheltered from the global financial crisis, but there could be an impact on investment, remittances and aid.

"Our appeal to our development partners is that they should not cut aid to the developing countries," Mr Kikwete said.

"Tanzania and other developing countries are deeply concerned with the current financial crisis coupled with skyrocketing oil and food prices."

But he also hoped that the global economic meltdown would not ultimately affect aid.

"Our expectation is that the financial crisis in Europe and America, and now the huge sums of money that are being spent to bail out the banks, would not impact negatively on development assistance to Africa," he said.

Mr Kikwete added that his country was looking at ways to soften the impact of the crisis.

"This situation has plunged many people in various parts of the world into economic misery," he said.


"On our part in Tanzania, we are watching the situation and see what we can do to mitigate the possible effects of the problem."


Déjà vu!
Bado tunaangalia.
Seriously?
 


HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, 31 JANUARI, 2008








Once again mzee wa Pamba aka JK akisaidiwa na maspeech writers wake anataka kulink shida za waTanzania za maji machafu, na huduma mbovu za jamii kwa SUBPRIME MORTAGES MELTDOWN IN THE USA na hiyo RECESSION inayosadikiwa huko.

Maswali kwa JK:


CREDIT CRUNCH YA USA INAHUSIANA VIPI NA WATANZANIA KUKOSA BARA BARA ZA MAANA?
(mfano bara bara ya Kagera haipitiki wiki ya pili sasa)

DSC06074.jpg



US RECESSION INAHUSIANA VIPI NA WATANZANIA AMBAO WAMEOPT KUTUMIA BANDARI YA MOMBASA BADALA YA DAR?
Bandari yetu imejaa urasimu kuliko ya Mombasa na hali inafanya kuwa mbaya na TRA ambao serikali yako umetumia mamilioni kuwasomesha lakini hawajui tofauti ya TV na MONITOR YA COMPUTER)
os17.jpg




SUBPRIME MORTGAGES INAHUSIANA VIPI NA HAWA WAZEE KUKOSA MAFAO YAO?
(wazee wa Jumuiya hawajalipwa mafao yao mpaka leo)

march7-1.jpg




JK UNAPOSEMA KUWA UMEWAAGIZA WACHUMI WAKO WAFANYE UCHAMBUZI WA KINA WA HIYO RECESSION AMBAYO IPO KAMA VILE HAIPO NA MAMBO YA CREDIT CRUNCHS SIKUELWEI
(Je huyu jamaa atakuelewa unachosema?)
os11-1.jpg



MHESHIMIWA RAIS HUNA HAJA YA KUWAPA MAAGIZO HAO WATU BALI HIYO NI KAZI YAO NA WALITAKIWA WASHA PREDICT GLOBAL ECONOMY ITAKAVYOKUWA IN 2008


KAZI YA RAIS KAZI YAKO SIYO KUDELEGATE HAO WASHAURI WAKO KUHUSU GLOBAL ECONMIC TRENDS

HIYO NI KATIKA JOB DESCRIPTION YAO NA ILITAKIWA HIZO RIPOTI TAYARI WALISHAZIWAKILISHA KWAKO.

THE SAME KAMA GW BUSH NA OF COURSE BERNAKE NA PAULSON KILA KUKICHA WANAASHUSHA HIZO INTEREST RATES

MHESHIMIWA UKITAKA NIANZE KUKUTAKE SERIOUS PUNGUZA BARAZA LA MAWAZIRI TOKA 60 NITAKUONA UNA NIA YA KUTUOKOA KIUCHIMU NA SIYO KUJA NA SPEECH AMBAZO JAMAA ZAKO WANA CUT AND PASTE ARTICLES TOKA GAZETI LA ECONOMIST


(Je huoni hatuna umuhimu wa haya ma VX? Je unajua hayo ma VX 60 yangejenga kilomita ngapi kule Mafia?


ST2.jpg

st1.jpg

(Baraza lako la mawaziri ni 60 NA kila waziri kapewa gari dizaini hii ambalo si chini ya milioni 60 sasa hebu justify hili nalo)



Mwenye wivu na ajinyonge, Tanzania ni mfano wa kuigwa!!
 
Mwenye wivu na ajinyonge, Tanzania ni mfano wa kuigwa!!

Teh teh teh
hiyo ilikuwa mwaka 2008 saizi 2009 ,imepiga hatuwa yafaa kuigwa.

Harafu ukiangalia na hiyo thread utaguduwa mwanzo watu wengi walikuw pamoja kuutafuta mwarobaini wa matatizo yetu,lakini baadaye wenda wakaguduwa kuna wezetu wana hoja za siri ,kwi kwi kwi kwi
 
Teh teh teh
hiyo ilikuwa mwaka 2008 saizi 2009 ,imepiga hatuwa yafaa kuigwa.

Harafu ukiangalia na hiyo thread utaguduwa mwanzo watu wengi walikuw pamoja kuutafuta mwarobaini wa matatizo yetu,lakini baadaye wenda wakaguduwa kuna wezetu wana hoja za siri ,kwi kwi kwi kwi


nani kakuongopoea kuwa tuko poamoja? hatupo pamoja humu
kwi kwi kwi kwi
 
Back
Top Bottom