salimkabora
JF-Expert Member
- Nov 10, 2012
- 2,441
- 651
Kwa hili la katiba mpya Jk amethibitisha ujeshi wake kwa kusimama na matakwa ya wananchi kuliko kukumbatia itikadi za vyama vya siasa ambazo zimelitumbukiza taifa katika majanga mengi ya kutisha ikiwa ni pamoja na ufisadi, uporwaji rasilimali, ukumbatiaji wenye nacho, nk. Hapa Jk amewatoka majambazi yote yaliyokuwa yanamtia ujinga na kumfunga mdomo asisimamie taifa ipasavyo na badala yake kufata mkondo wa magenge yaliyojipanga kivyama ili kupata nguvu ya pamoja za uporaji. Hapa JK ameonyesha rangi yake ya kweli ya ujeshi kusimama na nchi yake mda wote badala ya kusombwa na mkondo wa waangamiza nchi. Nyerere ni baba wa uhuru na jk ni baba wa taifa jipya. Aliyebezwa na kudharauliwa na kutukanwa hatimaye ameibuka kuwa shujaa. Mwana jf hebu tiririka hapa chini kuhusu Jk kuruhusu mivyama ya kisiasa kufa na kuwang'oa meno wanasiasa na kubakia mapengo matupu. N sema hili ni la JK kwa maana alikuwa na mabavu ya kutosha kulikwamisha nyuma ya pazia na kwa kuwa kaliacha kama lilivyo ni wazi mafuta yamejitenga na maji.