nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]JUMAMOSI, NOVEMBA 17, 2012 08:33 NA ELIYA MBONEA, KILIMANJARO
RAIS Jakaya Kikwete amesema ameshangazwa na utekelezaji wa miradi mikubwa katika awamu yake kwa muda mfupi, ikiwamo ujenzi wa madaraja makubwa ya Kigamboni, Malagarasi na Kilombero.
Rais aliyasema kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) juzi, alipozungumza na viongozi wa dini mkoani Arusha.
Kwa kweli hata mimi, wakati mwingine nashangazwa na mambo mengi tuliyoweza kuyatekeleza katika muda mfupi.
Hivi sasa tunajenga madaraja matatu Kigamboni urefu wa mita 680, daraja la Malagarasi kilomita 2.75 na Kilombero urefu wa mita 510, alisema Rais Kikwete na kuongeza:
Imekuwa ni miujiza ya Mwenyezi Mungu chukulia mfano ujenzi wa madaraja makubwa nchini kwenye Mito ya Mara, Rufiji, Kilombero, Malagarasi na Kigamboni yalikuwa katika mpango wa pili wa miaka mitano tangu mwaka 1969, lakini hayakuweza kutekelezwa, alisema.
Alisema wakati awamu ya Mwalimu Julius Nyerere, lilijengwa daraja moja tu kati ya hayo matano.
Alisema lilijengwa daraja la Kirumi ambalo liko mto Mara, wakati daraja la pili ni la Mto Rufiji lilijengwa na Rais wa zamani Benjamin Mkapa.
Akizungumzia suala la amani, Rais Kikwete aliwahimiza viongozi wa dini kuendelea kuiombea nchi ili amani na utulivu uliopo uendelee.
Nawaombeni jambo moja kubwa, tuendelee kuombea amani na utulivu. Amani ikivurugika hakuna atakayekwenda kanisani, msikitini wala shambani. Amani na utulivu ndio kila kitu, alisema Rais Kikwete.
Viongozi wa dini walioongoza maombi uwanjani hapo ni Askofu wa Kanisa la Anglikani Dayosisi ya Mount Kilimanjaro (DMK), Stanley Hotay, Askofu Dk. Leonard Majura Mwizarubi wa Kanisa la EAGT.
Wengine ni Kaimu Sheikh wa mkoa wa Arusha, Sheikh Abdilrahman Salim, Askofu Paul Akyoo Dayosisi ya Meru (KKKT) na Askofu Eliud Isangya wa Kanisa la International Evangelism Church.
Katika mazungumzo na maombi yao, kwa nyakati tofauti viongozi hao walisema wanatambua fika mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais Kikwete, na yameleta ustawi zaidi kwa wananchi wa Tanzania.
RAIS Jakaya Kikwete amesema ameshangazwa na utekelezaji wa miradi mikubwa katika awamu yake kwa muda mfupi, ikiwamo ujenzi wa madaraja makubwa ya Kigamboni, Malagarasi na Kilombero.
Rais aliyasema kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) juzi, alipozungumza na viongozi wa dini mkoani Arusha.
Kwa kweli hata mimi, wakati mwingine nashangazwa na mambo mengi tuliyoweza kuyatekeleza katika muda mfupi.
Hivi sasa tunajenga madaraja matatu Kigamboni urefu wa mita 680, daraja la Malagarasi kilomita 2.75 na Kilombero urefu wa mita 510, alisema Rais Kikwete na kuongeza:
Imekuwa ni miujiza ya Mwenyezi Mungu chukulia mfano ujenzi wa madaraja makubwa nchini kwenye Mito ya Mara, Rufiji, Kilombero, Malagarasi na Kigamboni yalikuwa katika mpango wa pili wa miaka mitano tangu mwaka 1969, lakini hayakuweza kutekelezwa, alisema.
Alisema wakati awamu ya Mwalimu Julius Nyerere, lilijengwa daraja moja tu kati ya hayo matano.
Alisema lilijengwa daraja la Kirumi ambalo liko mto Mara, wakati daraja la pili ni la Mto Rufiji lilijengwa na Rais wa zamani Benjamin Mkapa.
Akizungumzia suala la amani, Rais Kikwete aliwahimiza viongozi wa dini kuendelea kuiombea nchi ili amani na utulivu uliopo uendelee.
Nawaombeni jambo moja kubwa, tuendelee kuombea amani na utulivu. Amani ikivurugika hakuna atakayekwenda kanisani, msikitini wala shambani. Amani na utulivu ndio kila kitu, alisema Rais Kikwete.
Viongozi wa dini walioongoza maombi uwanjani hapo ni Askofu wa Kanisa la Anglikani Dayosisi ya Mount Kilimanjaro (DMK), Stanley Hotay, Askofu Dk. Leonard Majura Mwizarubi wa Kanisa la EAGT.
Wengine ni Kaimu Sheikh wa mkoa wa Arusha, Sheikh Abdilrahman Salim, Askofu Paul Akyoo Dayosisi ya Meru (KKKT) na Askofu Eliud Isangya wa Kanisa la International Evangelism Church.
Katika mazungumzo na maombi yao, kwa nyakati tofauti viongozi hao walisema wanatambua fika mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais Kikwete, na yameleta ustawi zaidi kwa wananchi wa Tanzania.