JK: Mgomo wa madaktari ulikuwa 'ngoma nzito'... Aeleza kilichomfanya asaini haraka haraka

Faiza Fox yuko wapi siku hizi, au yuko kwenye ban? Ningependa kusikia ana maoni gani naye kuhusu jambo hili.
 
Sisi ndo tumewatuma hao wabunge kutuwakilisha, iweje sisi maboss tudharauliwe??? Kuna haja ya Katiba ijayo kuwapa nguvu kubwa wananchi kufanya maamuzi mazito kama kutokuwa na imani naa Rais kuliko kuwapa nguvu hiyo wabunge mana ni vigumu Rais kuhonga wananchi wote.

Kama hali ingekuwa hivyo Rais asingewahonga wabunge kwa kupitisha sheria mbovu kwani angejua kuwa hata asipoipitisha wabunge wa CCM wasingeweza kufanya chochote.

Njia hii ya kibabaishaji aliyoitumia Rais kupunguza hasira za Bunge naitafsiri kama RUSHWA YA KITAASISI NA KUBWA ZAIDI KUTOKEA HAPA NCHINI. Je PCCB hii kauli kwa sheria zenu sio RUSHWA???Tunaomba muongozo wenu.
 
Huyu ndie kiongozi wa nchi, anawaogopa wabunge wa chama chake kuliko maslahi ya nchi. Tujiulize, kama ana woga wa aina hiyo amefanya /atafanya mangapi yasiyo na maslahi kwa taifa kwa ajili ya kuwaogopa CCM.

Dangerous statement!!! Sio kwamba ameacha, muelewe wapendwa wananchi anaendelea kuwaogopa!! Nimechoka
 
Kwa kauli hiyo, wabunge wa ccm wangekuwa makini wangevunja serikali. Ni kauli ya aibu kwanza kwa Rais Mwenyewe na Chama chake na pia ni kauli ya kuwazalilisha wabunge wa ccm.
 
Huyu ndie kiongozi wa nchi, anawaogopa wabunge wa chama chake kuliko maslahi ya nchi. Tujiulize, kama ana woga wa aina hiyo amefanya /atafanya mangapi yasiyo na maslahi kwa taifa kwa ajili ya kuwaogopa CCM. Dangerous statement!!! Sio kwamba ameacha, muelewe wapendwa wananchi anaendelea kuwaogopa!! Nimechoka
Kiongozi huna haja ya kuchoka kazi ndo inaanza, ni jukumu letu sisi tunaoelewa hali ya mambo kuwaelimisha wale wanaozawadia viongozi kura wakati wa uchaguzi. Ni sisi ndo wakuwaambia madhara ya kuwa na wabunge wa chama kimoja zaidi bungeni. Idadi ingekuwa sawa kwa sawa haya yasingetokea. Marekani, UK na kwingineko wamefika hapa walipofika sababu wafanya maamuzi ni 50% kwa 50% so Rais hana sababu ya kuogopa kundi fulani kama hapa kwetu.
 
Kwa kauli hiyo, wabunge wa ccm wangekuwa makini wangevunja serikali. Ni kauli ya aibu kwanza kwa Rais Mwenyewe na Chama chake na pia ni kauli ya kuwazalilisha wabunge wa ccm.
Rais ameweka bayana kuwa wabunge wa CCM ndio wanaoficha maovu ya nchi hii hali inayopelekea Rais kuwapa Respect ya uoga.
 
Yale majina waliompa huko Davoz sasa anayadhihirisha. Kumbe sisi hata hatumjui rais wetu. Wa nje ndiyo wanamjua vizuri.

Hii ndiyo hasara ya kuchaguwa mtu ajili ya baby face yake. In the end he starts behaving like one.
 

Faiza Fox yuko wapi siku hizi, au yuko kwenye ban? Ningependa kusikia ana maoni gani naye kuhusu jambo hili.

Faiza anampa mwanahawa tuisheni ili aende masomoni london school of economics!

Hata mie mwanamke nisingeweza kutoa jibu kama hilo. Ina maana hatuna Rais mwenye msimamo anayeweza kutumia akili yake kufanya maamuzi? kazi ipo hadi 2015. hii ni aibu na fedheha kubwa sana kwa tanzania. huyu angefaaa kuwa mkuu wa kitengo cha kucheza ngoma kuliko kuwa rais. Kama baba kama mwana...mwanahawa ameonyesha mfano jinsi baba alivyo
 
Hofu yangu ni kuwa atawaogopa wangapi?ataogopa mangapi? ataogopa mara ngapi? ataogopa lini? Rais wa namna hii hatufai kabisa. Tumemkabishi uongozi wa nchi halafu yeye anafanya kazi kwa hofu?

Rais anayewaogopa mafisadi, anamwogopa L....? Atatufikisha wapi? Je? tunaweza kupata katiba mpya chini ya rais mwenye hofu. Anaogopa chama chake. Atatufikisha wapi huyu jamani?

Mimi nimeogopa sana kwa sababu ya hilo la rais wetu kuwa mwoga. Kwa kweli tumwombe Mungu atuepushe na yale yote yanayomwogopesha rais wetu.
 
Jakaya Mrisho Kikwete ...A shameless Coward......

Sijui alipataje cheo jeshini.....mtu anaogopa hadi ujani...!!!...tukiingia vitani tukiwa na Amri Jeshi Mkuu KAMA huyu....tutachukuliwa woooote mateka!!...coward ...coward...mdebwedo!!
 
Baba wa Taifa alitueleza kuwa JK by then akiwa na around 45 years kuwa bado hajakomaa. Kikawaida mtu akifikisha umri kama huo anakuwa ameshakomaa. Sijui ni wapi hatukumuelewa yule mzee wa watu. Dah. alazwe mahali pema peponi, ila alitueleza huyu bado hajakomaa. Leo katudhihirishia mwenyewe kuwa bado hajakomaa. Na hajui kaz yake ktk utunzi wa sheria.​
 
Rais ameweka bayana kuwa wabunge wa CCM ndio wanaoficha maovu ya nchi hii hali inayopelekea Rais kuwapa Respect ya uoga.

Ndugu yangu Patriote,

Ndio maana ni kasema wabunge wa ccm wangekuwa na busara na umakini wa kuelewa nini maana ya alichokisema rais, serikali ingevunjika, maana yake ni kwamba yeye (rais) huwa hakubalini na mawazo yao kwa kuwa mara nyingi huwa hayana tija kwa taifa, lakini huwa anaogopa uwingi wao bungeni, sasa maana yake mawazo ya upinzani ndiyo yenye tija lakini akiungana nao hatadumu katika madaraka maana wapinzani ni wachache bungeni.

sasa kama rais hakubaliani nao kwa nini wako nae?, je hawaoni kwamba kauli hii kawazalilisha? na kama kawazalilisha je wanaikubali au wanachukua hatua gani?.

Mimi nimeifurahia sana kauli hii ya rais kwa sababu zifuatazo;

imetuonyesha ni rais wa jinsi gani tulienae.
imetuonyesha ni jinsi gani wabunge wa ccm walivyo.
na imetuthibitishia ni kweli ccm ni janga la kitaifa.

Kauli hii ni mbovu sana kutolewa na kiongozi wa nchi, rais mwenye mapenzi mema ni yule atakayesimamia haki hata kama atapigiwa kura ya kutokuwa na imani nae toka kwa wabunge wa chama chake, urais ni zaidi ya chama, ni maisha ya Watanzania 45m.

Tutafakari na tuchukue hatua.
 
Hapo ndipo ninapoukubali undumilakuwili wa JK katika michakato kama hii. Watu wameshanuka vibaya yeye ndiyo anajisafisha sasa.

Ndugu Lasambo unashangaa nini? JMK anatabia ya KUJIFICHA kwenye kivuli cha wengine! Hali inapokuwa MOTO, yeye HUKAA KIMYA.hali inapotulia ANAIBUKA na KUIISAFISHA. Hili sakata la Madaktari sio la kwanza. Anagalia haya:
1. Posho ya wabunge, anamtuma waziri mkuu na Kurugenzi yake ya habari kuongea. Yeye KIMYA!
2. Enzi zile za Richmond, baada ya kimya kirefu akaibukia Bungeni na "Kula Uliwe"!
3. Ishu ya Jairo haijakaa vizuri ndo sababu hatujamsikia! Tunapata hisia zake kupitia "Wasemaji wake".
Tusubiri kuona mengi!
 
01 MARCH 2012
Mbali na mgomo wa madaktari alielezea kusikitishwa na
mauaji ya Songea kwenye maandamano.

"Napenda kutumia nafasi hii
kuelezea masikitiko yangu kwa vifo hivyo na kutoa pole na rambirambi zangu na za wananchi wa Tanzania kwa ndugu wa marehemu wetu hao.

Tupo pamoja nanyi katika misiba hii mikubwa na majonzi.
Mahali penye alama, TOO LATE to say it today! Kwanini hatukumsikia palepale, ama baada ya kutoka ughaibuni? Amrijeshi mkuu ANASIKITIKA wakati ASKARI wake WANAUA RAIA? Eti TUKO PAMOJA!
 
Back
Top Bottom