JK mawaziri wawili wanatuchefua unaweza kuwafanyia namna????

Kizito

Member
Feb 23, 2008
69
2
Pamoja na pongezi zetu kuhusu baraza lako jipya la Mawaziri lakini kuna mawaziri wawili wanatutia Kichefuchefu, Mmoja ni Profesa Mwandosya kosa la huyu msomi ni dogo sana lakini linaathali kubwa kiutendaji.

Alipokuwa akitembelea vyanzo vya maji Dar aliwaomba watendaji wake kutowataja Mawaziri wasiolipa maji ili wasije kuumbuka na badara yake alisema yeye yuko tayari kuwalipia tunachouliza kama waziri halipi mwenye mishahara miwili wa Ubunge na wa uwaziri analipiwa kwa nini usiwalipie wale wanao katiwa maji kila kukicha kwa kukosa sh 10 000/= tu? JK mwangalie huyu jamaa atatupatia hasara ndani ya Serikali.

Mwingine anaetuchefua ni Chenge huyu alisaidia kusaini mikataba yote mibovu iliyopo sasa hivi. kwa hiyo kuwepo kwake Ndani ya Baraza ataendelea kuilinda mikataba hiyo fanya namna JK.
 
..Hiyo ya chenge nakuunga mkono. Lakini hii ya Mwandosya naona unataka kumpakazia. Imekaa kama ya kwenye magazeti ya "The Sun". Lete data. Alitembelea chanzo kipi, na alimkataza mtendaji yupi asitaje jina la waziri. Usishushe hadhi ya JF!!
 
..Hiyo ya chenge nakuunga mkono. Lakini hii ya Mwandosya naona unataka kumpakazia. Imekaa kama ya kwenye magazeti ya "The Sun". Lete data. Alitembelea chanzo kipi, na alimkataza mtendaji yupi asitaje jina la waziri. Usishushe hadhi ya JF!!

Mwandosya ni mchafu tu si kwenye hayo maji pekee .Rada na mengineyo hadi kusomeshewa watoto huko nje .Yaani unataka ushahidi wa Mwandosya kuwa ni mchafu ?Muulize Mtanzania atakueleza vyema japokuwa atamtetea lakini anajua .Soma nondo ya Mzee wa Kijijini utajua zaidi .
 
Pamoja na pongezi zetu kuhusu baraza lako jipya la Mawaziri lakini kuna mawaziri wawili wanatutia Kichefuchefu, Mmoja ni Profesa Mwandosya kosa la huyu msomi ni dogo sana lakini linaathali kubwa kiutendaji.

Alipokuwa akitembelea vyanzo vya maji Dar aliwaomba watendaji wake kutowataja Mawaziri wasiolipa maji ili wasije kuumbuka na badara yake alisema yeye yuko tayari kuwalipia tunachouliza kama waziri halipi mwenye mishahara miwili wa Ubunge na wa uwaziri analipiwa kwa nini usiwalipie wale wanao katiwa maji kila kukicha kwa kukosa sh 10 000/= tu? JK mwangalie huyu jamaa atatupatia hasara ndani ya Serikali.

Mwingine anaetuchefua ni Chenge huyu alisaidia kusaini mikataba yote mibovu iliyopo sasa hivi. kwa hiyo kuwepo kwake Ndani ya Baraza ataendelea kuilinda mikataba hiyo fanya namna JK.

mhhh kazi kweli kweli!
 
Yaliyosemwa hapo chuu ni ukweli mtu, Mwandosya aliwambia DAWASCO wasiwataje mawaziri wanaodaiwa bill za maji, kwa kigezo kuwa wao ni mawaziri hivyo si vizuri kuwaumbua, lakini kumbuka mteja ni mtja na hatuangalii cheo cha mtu kwenye kulipa

Mkuu, sasa weka mambo wazi basi. Maana moto ya JF ni "where we dare to talk openly" Issue ya chenge inafahamika hata kwa watoto wachanga. Kama ni kweli huyo jamaa alisema hivyo, basi ndio hivyo tena...
 
Mwandosya ni mchafu tu si kwenye hayo maji pekee .Rada na mengineyo hadi kusomeshewa watoto huko nje .Yaani unataka ushahidi wa Mwandosya kuwa ni mchafu ?Muulize Mtanzania atakueleza vyema japokuwa atamtetea lakini anajua .Soma nondo ya Mzee wa Kijijini utajua zaidi .

Heshima mbele mkuu (tibwili)2. Issue iliyokuwa inaongelewa hapa ni ya DAWASA. Otherwise, nakubaliana na wewe.
 
Pamoja na pongezi zetu kuhusu baraza lako jipya la Mawaziri lakini kuna mawaziri wawili wanatutia Kichefuchefu, Mmoja ni Profesa Mwandosya kosa la huyu msomi ni dogo sana lakini linaathali kubwa kiutendaji.

Alipokuwa akitembelea vyanzo vya maji Dar aliwaomba watendaji wake kutowataja Mawaziri wasiolipa maji ili wasije kuumbuka na badara yake alisema yeye yuko tayari kuwalipia tunachouliza kama waziri halipi mwenye mishahara miwili wa Ubunge na wa uwaziri analipiwa kwa nini usiwalipie wale wanao katiwa maji kila kukicha kwa kukosa sh 10 000/= tu? JK mwangalie huyu jamaa atatupatia hasara ndani ya Serikali.

Mwingine anaetuchefua ni Chenge huyu alisaidia kusaini mikataba yote mibovu iliyopo sasa hivi. kwa hiyo kuwepo kwake Ndani ya Baraza ataendelea kuilinda mikataba hiyo fanya namna JK.

Hata mimi la Mwandosya sima uhakika nalo lakini la Chenge, bila ya shaka huyu hafai kabisa.

Poa moto JK anazo habari zake huyu (Chenge) nyingi tu, na akae mako wa kula.
 
Kuna tatizo gani mtu anapojitolea kumlipia mtu au watu wengine kwa sharti dogo la kutotaja jina au majina...?

Sioni kosa la Mwandosya hapo, zaidi ametumia uungwana wa kawaida kabisa katika kutatua tatizo.
 
JF, tusianze kuwa kijiwe cha kuharibu sifa za watu ili ku fulfill interest za watu fulani. Nafikiri Mwandosya kaliongelea suala la kutoanika majina ya Mawaziri wanaodaiwa maji magazetini ni suala la collective responsibility zaidi kwa watendaji wa serikali (Mawaziri)na yeye mwenyewe akiwemo. Leo hii Tuambiwe Waziri Masha kashindwa kulipa bill za maji, hii ni aibu kwa serikali na mawaziri wenzake. Haiwezekani tena Mwandosya akasimama kuwaambia wananchi walipie bill zao za maji wakati Mawaziri wenyewe hawalipi. Ndio maana akasema yeye atawalipia, sisi hatuna tatizo na malipo hayo. Lakini suala la kuwaanika hata mimi sikubaliani nalo kabisa na nalipinga kwa nguvu zangu zote. Watarudije kutuambia tukalipie maji wakati wao wameshindwa? Cha msingi kuna mawasiliano ya ndani ya serikali kiutendaji, wafikishiwe kwa utaratibu huo au hata kupelekwa tume ya maadili ya Viongozi.

Alichokosea Mwandosya ni kwamba ameliongea hili publically, suala alilotakiwa aliongee katika vikao vya ndani ya wizara na wakubaliane na watendaji wa Dawasco namna iliyo bora kuhakikisha mawaziri wanalipia bill zao kwa wakati unatakiwa.
 
Personally ninaieshimu JF kama kijiwe cha kuweka mambo hazarani pamoja na attached facts.Ningependa tupatiwe izo facts za uyo Prof kuhusiana na iyo STM yake tafadhali.

Otherwise Mark he is good,ingawa ana mabaya ya hapa na pale,mind you it was only Nyerere ambaye anaweza stand firmly na kusema ni msafi but currently no one kwa kweli.
What matters now ni extent ya ufisadi kama ule wa bil 133 n.k
 
Nchii hii haitafika kokote kule kama kila mtu hatatekeleza wajibu wake. haijalishi how minor that responsibility is. Sioni sababu ya Mwandosya kuongea in public kuhusu personal bills za mawaziri! kama hawawezi hata kutekeleza majukumu ya majumbani kwao how the hell can they be concerned with the prosperity of this country.

Mambo madogo kama haya can say a lot about a person, hapa naweza kusema walifanya makusudi kabisa kutokulipa hizo bills, sio kwamba hawana fedha, fedha wanazo, sio kwamba wamekosa muda wa kwenda kulipa hapana wanawafanyakazi wengi sana ambao wanaweza kuwatuma kwa shughili hii ndogo. sioni sababu wala kisingizio cha wao kutolipa hata kidogo.

Hawa hawa ndio wanakuja kukaa baadaye katika kubinafsisha mashirika nyeti kama haya pale yanaposhindwa kujiendesha, yatajiendeshaje kama haulipi ankara zako!!!!!!!!
 
Personally ninaieshimu JF kama kijiwe cha kuweka mambo hazarani pamoja na attached facts.Ningependa tupatiwe izo facts za uyo Prof kuhusiana na iyo STM yake tafadhali.

Otherwise Mark he is good,ingawa ana mabaya ya hapa na pale,mind you it was only Nyerere ambaye anaweza stand firmly na kusema ni msafi but currently no one kwa kweli.
What matters now ni extent ya ufisadi kama ule wa bil 133 n.k

KWA KUWA ULITAKA FACTS ZA HUYO PROFFESORR ZISOME HAPA KAMA ZILIVYOANDIKWA KWENYE GAZETI LA SERIKALI DAILY NEWS.

Mwandosya: Ministers to pay water bills promptly
JIANG ALIPO
Daily News; Thursday,February 21, 2008 @18:03
NEWLY appointed Minister for Water and Irrigation, Prof Mark Mwandosya, has promised to facilitate prompt payment of water bills by his fellow cabinet members who have failed to do that in time.

Speaking at the final day of his three-day tour of the water sources and distribution areas in Dar es Salaam and Coastal regions on Wednesday, Prof Mwandosya said that he will always try to remind fellow cabinet members to settle their bills in time.

“My main concern is the image of the ministers, as the image of the government is portrayed in the personality and behaviour of its ministers,” explained Prof Mwandosya. “If the aim of Dawasco is to get my colleagues pay their bills in time, I can be of help,” he stressed.

The Dar es Salaam Water and Sewage Company (DAWASCO), is the company that has a duty to operate the city’s water and sewage systems, including collection of revenue from its customers. During his last day of the visit, the minister visited the water treatment plants in Kimara Suca, Ubungo Kibangu, Mabibo Mzambarauni, Mabibo Sahara and Mtoni.

In his tour, Prof Mwandosya had a chance to see water supply kiosks which have been built by Dawasco to serve during shortage days. The kiosks are run by local committees. The Dawasco Chief Operations Officer, Mr Jackson Midala, told the minister that there are 158 such kiosks in the city. He added that the company plans to open 254 more kiosks.
 
Prof Mwandosya said that he will always try to remind fellow cabinet members to settle their bills in time.

“My main concern is the image of the ministers, as the image of the government is portrayed in the personality and behaviour of its ministers,” explained Prof Mwandosya. “If the aim of Dawasco is to get my colleagues pay their bills in time, I can be of help,” he stressed.

Sijaona kosa hapo
 
Mwandosya kachemsha hapana kumtetea...

Kama MAWAZIRI HAWALIPI waanikwe tu...wazembe hao ndio wanaotuchelewesha....KUWAFICHA Maana yake ni kuficha UOZO. Yaaani image zao na personality zao muhim kuliko maslahi ya Taifa..kesho mje kuibinafsisha mle vyenu 10%

Hivi Personality ya LOWASSA ilivyoharibiwa itakuwa sawa na wazir wa Kawaida?
Kutokulipa BILls ni lack of sense of responsilty....lack of sense of Ownership...ahh hiki changu???...acha tu twende hivyo hivyo!!! EBO!!!...usiharibu NCHI kwa UZEMBE wako...

Dawasco..TANESCO hapana kuzembea watu sasa ikiwa wazir na wengine hawajalipa kata HUDUMA!!!...wanapewa pesa wao kwenda ktk ULEVI na ANASA
 
Chuma, Wahenga wanasema ukipenda chongo utaita kengeza! Ndio kinachoondelea hapa. Kwasababu moja au nyingine Huyu prof kapendwa sana hapa sasa hata amwage utumbo gani atatetewa tu. Kama waziri na kipato chake halipi bill kwa taasisi ya umma ambayo inaendeshwa kwa hizo bills, unadhani ana sifa ya kuheshimika na kupewa dhamana ya kutunza maslahi ya umma huohuo katika jungu kuu? Halafu mtu anasema huyu alindwe na aheshimiwe na raia wanamtetea asemaye hayo!

Mwandosya kachemsha hapana kumtetea...

Kama MAWAZIRI HAWALIPI waanikwe tu...wazembe hao ndio wanaotuchelewesha....KUWAFICHA Maana yake ni kuficha UOZO. Yaaani image zao na personality zao muhim kuliko maslahi ya Taifa..kesho mje kuibinafsisha mle vyenu 10%

Hivi Personality ya LOWASSA ilivyoharibiwa itakuwa sawa na wazir wa Kawaida?
Kutokulipa BILls ni lack of sense of responsilty....lack of sense of Ownership...ahh hiki changu???...acha tu twende hivyo hivyo!!! EBO!!!...usiharibu NCHI kwa UZEMBE wako...

Dawasco..TANESCO hapana kuzembea watu sasa ikiwa wazir na wengine hawajalipa kata HUDUMA!!!...wanapewa pesa wao kwenda ktk ULEVI na ANASA
 
Mwandosya kachemsha hapana kumtetea...

Kama MAWAZIRI HAWALIPI waanikwe tu...wazembe hao ndio wanaotuchelewesha....KUWAFICHA Maana yake ni kuficha UOZO. Yaaani image zao na personality zao muhim kuliko maslahi ya Taifa..kesho mje kuibinafsisha mle vyenu 10%

Hivi Personality ya LOWASSA ilivyoharibiwa itakuwa sawa na wazir wa Kawaida?
Kutokulipa BILls ni lack of sense of responsilty....lack of sense of Ownership...ahh hiki changu???...acha tu twende hivyo hivyo!!! EBO!!!...usiharibu NCHI kwa UZEMBE wako...

Dawasco..TANESCO hapana kuzembea watu sasa ikiwa wazir na wengine hawajalipa kata HUDUMA!!!...wanapewa pesa wao kwenda ktk ULEVI na ANASA

halafu wakome kubinafsisha mali zetu bila ya kura zetu za maoni.
Kama hawalipi bill basi ni nini wanacholipa?? inaonehsa hata Ada za shule za woto wao wanalipiwa. Je mishahara na bonus pamoja na hela za kifisadi wanapeleka wapi?? Wanaweka hazina mbinguni nin???
 
tunachouliza kama waziri halipi mwenye mishahara miwili wa Ubunge na wa uwaziri analipiwa kwa nini usiwalipie wale wanao katiwa maji kila kukicha kwa kukosa sh 10 000/= tu?


Kama Mwandosya anawalipia kwa pesa yake ya mfukoni hiyo ni poa tu, tena wangepokea huo mshiko hapohapo na kumpa risiti yake.

Watu wengi huwa hawanashindwa kulipa bili za maji sababu huwa ni kubwa sana ukilinganisha na uwezo wao lakini kuna ambao huwa hawalipi sababu hizo bili huwa ni ndogo sana ukilinganisha na uwezo wao. Nafikiri TANESCO wangeanzisha utaratibu wa kufuata hizo bili majumbani kwa vigogo na kuwachaji na pesa ya mafuta!
 
Pamoja na pongezi zetu kuhusu baraza lako jipya la Mawaziri lakini kuna mawaziri wawili wanatutia Kichefuchefu, Mmoja ni Profesa Mwandosya kosa la huyu msomi ni dogo sana lakini linaathali kubwa kiutendaji.

Alipokuwa akitembelea vyanzo vya maji Dar aliwaomba watendaji wake kutowataja Mawaziri wasiolipa maji ili wasije kuumbuka na badara yake alisema yeye yuko tayari kuwalipia tunachouliza kama waziri halipi mwenye mishahara miwili wa Ubunge na wa uwaziri analipiwa kwa nini usiwalipie wale wanao katiwa maji kila kukicha kwa kukosa sh 10 000/= tu? JK mwangalie huyu jamaa atatupatia hasara ndani ya Serikali.

Mwingine anaetuchefua ni Chenge huyu alisaidia kusaini mikataba yote mibovu iliyopo sasa hivi. kwa hiyo kuwepo kwake Ndani ya Baraza ataendelea kuilinda mikataba hiyo fanya namna JK.


.....mzee kizito acha conspirancy...huyo mwandosya hana hata wiki mbili wizarani...unategemea awe amefanya nini....lete dataz acha kuleta majungu hapa...??? ...zaidi ya hilo tutaendelea kumwamini mwandosya kuwa anafaa kwa hata rais wa tanzania 2010 iwapo MUUNGWANA ataona busara ya kutogombea second term.....
 
.....mzee kizito acha conspirancy...huyo mwandosya hana hata wiki mbili wizarani...unategemea awe amefanya nini....lete dataz acha kuleta majungu hapa...??? ...zaidi ya hilo tutaendelea kumwamini mwandosya kuwa anafaa kwa hata rais wa tanzania 2010 iwapo MUUNGWANA ataona busara ya kutogombea second term.....
Naona umemshikia bendera Muungwana
 
Jamani, alichosema Mwandosya makes sense in one way, in order kwake kwenda kuomba fedha za matumizi za Dawasco, he has to go through the cabinet first, kabla hawaja request bungeni. Sasa kama kuna Waziri hajalipa, mpeni majina yeye ili akawapatie hizo pesa, na siyo kutaja taja tu hadharani, huko ni kutafuta sifa tu kwa Dawasco...kama juzi walivyo wakatia maji jeshi. Sasa kama unawataja taja hovyo si watamsumbua huko kwenye cabinet. Hiyo inaitwa Diplomacy, plain and simple. Mchezo wa kutajataja watu hadharani kisa billi...kama hawajalipa, kuna procedures za kufuata. Pesa zitalipwa, mnajuaje kama wengine bili hawakupata, there could be many reasons why hawajalipa, what if wamekuwa overcharged for poor service? there ar emany things behind it ambayo hayatuhusu katika huduma za maji kati ya watu na Dawasco ambayo haihusu press. Dawasco siyo chombo cha siasa, mbona hawataji deni la ikulu...

Hawa Dawasco wanahitaji management mpya ishughulikie PR department yao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom