Elections 2010 JK, Lowasa na Rostam wakitawala Tz kwa miaka 5 ijayo itakuwaje?

H6MohdH6

Member
Oct 8, 2010
43
3
JK na washirika wake wakuu, Lowasa na Rostam, wakiendelea kutawala kwa miaka 5 ijayo wa-Tz tujiaandae kuona sehemu kubwa ya nchi yetu imeuzwa na sisi wenyewe tumeuzwa utumwani kwa Waarabu na Wahindi ili kushibisha tu matumbo yao na tamma yao ya fedha.Tumerudia zile zama za viongozi wetu kutuuza utumwani kwa bei ya shanga na kaniki walizopewa na wanunuzi wa watumwa ili wawape wake zao wavae, wapendeze.

Inabidi wa-Tz tutumie akili yetu kweli kweli na tuwe na ujasiri kweli kweli ili kupambana na hali hii na kuhakikisha dhamira ya hawa akina Mangungo, Sultani wa Msovero wa leo, wakishirikiana na Tippu Tippu, kamwe haitafanikiwa. Kamwe tusikubali nchi yetu kuuzwa nasi kuuzwa utumwani karne hii ya 21 tena tukiwa machomacho!
 
You've heard of the National Socialist German Workers' Party, right?

There's your answer.
 
Back
Top Bottom