JK kwenda DAVOS wakati wananchi wake wanakufa kwa kukosa huduma za afya ni sahihi???

Patriote

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
1,718
1,047
Nimejaribu kuwaza na kuwazua nikagungua kuwa Rais wetu hana mapenzi na wananchi wake bali yupo madarakani kwa ajili ya kujitafutia maslahi yeye binafsi, anahangaika kutafuta sifa na international Night Out Allowances. Kama JK angekuwa nchini naimani huu mgomo wa madaktari ungekuwa umeshaishi. Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria alikatisha safari zake na kufwatilia kwa ukaribu suala la Boko Haram. Huyu wetu anasikia maDK wanagoma yeye ndo anaweka nguo kwenye sanduku kuelekea Davos, anaenda huko kwa faida ya nani ilhali anaacha watu wanakufa huku nyuma??Hawa sio wananchi anaokwenda kuwapigania huko Davos??Je angemtuma mtu mwingine huo ujumbe asingeupata???Kwa kweli kitendo alichokifanya kinaonesha jinsi anavyopuuza masuala muhimu ya kitaifa na kuelekeza nguvu kwenye masuala ya kipuuzi. Kwa kufanya hivyo ilitupasa tuwe barabarani kumshinikiza arudi nyumbani kumaliza suala la MaDK. Hivi VOTE OF NO CONFIDENCE INAPIGWAJE??MBONA MM NAHIC WATZ WENGI SANA SASA HIVI HATUNA CONFIDENCE NA HII SERIKALI???au vote hiyo inapigwa na WAFU??

Kumbekeni waathirika wakuu wa mgomo wa maDK ni sisi watega ndege, wenzetu wakiumwa mafua wanakwea ndege hao India, kimsingi huu mgomo unatuhusu sisi wapiga kura wa hali ya chini. So bila kushinikiza Serikali iumalize tunaoangamia ni sisi. Mimi nadhani hii ndiyo ilikuwa fursa nzuri ya kutukutanisha barabarani na kuandamana. Lakini tupo tunapumzika na kushabikia mgomo ilhali ndugu zetu wanapoteza maisha. Ni lini sisi tutakua tayari kupigania maslahi yetu???Mbona tumekuwa kama UNOKA wa Chinua Achebe???Ni tija gani ataileta tukamuelewa wakati sisi tupo bize misibani kwa kufiwa na baba zetu, mama zetu ndugu zetu na tumeachwa yatima??Hivi kwann nlizaliwa nchi ya watu wa hivi???Dah kwa uvumilivu huu hata moton sisi tutaishi bila shida, Mweh!!!
 
Nadhani pengine sasa ndiyo Watanzania tutaelewa kumbe nchi zingine zinapopelekewa kitu kinachoitwa "Regime Change" sababu huwa ni nini. Mara zote huwa tunaangalia kutoka nje na kulaani mfano pale Marekani inapomng'oa mjinga fulani madarakani kupitia wananchi wa nchi husika. Hali ilipofikia sasa tunaweza kuangalia kwa jicho la ndani maana sisi sasa ndiyo zamu yetu kuendeshwa na serikali ya kipumbavu. Tofauti ni kwamba Marekani haitakuja kuleta regime change na hivyo hilo linabaki kuwa jukumu la wananchi wenyewe.
Tatizo ni kwamba uoga ndiyo umeshika hatamu, badala yake watu wanaishi kwa matumaini tu kwamba siku inakuja uongozi wa kipuuzi wa Kikwete na genge lake la malumpeni utapigwa chini. Ukweli ni kwamba matumaini ni "state of mind", si kitu halisi, mpaka pale watu watakapovua uoga na kuitwaa nchi ndiyo tofauti itaonekana.
Regime change haiji kwa sanduku la kura wala majadiliano maana hiyo siyo asili ya Waafrika; sisi ni watu wa kupewa kibano tu ndiyo mambo yanaenda.
 
kwanza huko DAvos hata sijui kama anaelewa kinachofanyikaga..ni shida sana kuwa na rais mwenye ufinyu wa mawazo..yaani anapitwa hata na akina Kibaki wazee lakini akili iko sharp vibaya sana...huyu ni mzigo na janga kwa taifa...yaani kabila lake na dini anayotoka sijui kama tutakubali kuja kutawala hii nchi tena
 
To Richard: Cameron must focus on problems at home instead of trying to solve world problems. He should let Jacom Zuma solve African problems. SA economy is the largest in Africa, and can support some of those that needs economic boost.


If Tanzanians dont want to solve their problems, then nothing we can do as Brtis. ANC austed Thabo Mbeki to save the party . Tanzania rulling party must get rid of Jakaya Kikwete to remain the party it once was because the man is an embarrassment to say the least. I was in the audience and was shocked he could not answer the simple question posed to him


Tanzania people are some of the most hospitable in the EA region and do not deserve the kind of leadership they have. I think getting rid of their rulling party and current goverment may save their boat from sinking else they will be history. This happened in Kenya, Zambia during Kenneth Kaunda and will keep on spreading

Davos 2012: Day two, as it happened | Business | guardian.co.uk
 
Lakini mimi kinachonishangaza ni kwamba tumeshajua JK na serikali yake ni wababaishaji, lakini bado tunadhani ni lazma amalize miaka 10 ya kututawala hata kama amefail kudeliver. Ahadi zake hajazitekeleza, matatizo kila kukicha ni afadhali ya jana, nchi anazidi kuiuza kuna haja gani ya kuwa na liRais la hivi zaidi ya kutiwa Hasara tu???Okay tuseme hatukuwa na grounds za kuandamana. Jamani hata kwa kupitia mgomo wa madaktari bado tu hatujapata grounds??Ni grounds gani tunadhani ni sahihi kutufanya tuandamani zitakuwa zaid ya hizi za kutetea maisha yetu???au kwa kuwa si ndugu yako anayekosa matibabu muhimbili???au kwa kuwa sio wewe unayeumwa???kwann jukumu hili tuwaachie wagonjwa badala ya sisi tuliofit mtaani???Nani awatetee wagonjwa wanaobeep kifo sasa hivi kwa uzembe wa Serikali kushindwa kumalizana na wagonjwa.

Hivi tunadhani kuna ugumu gan kuitoa serikali babaishaj kama hii madarakani?? Nina imani kuwa asilimia kubwa sana ya wananchi wameshaichoka hii serikali na hivyo hata hao askari/wanajeshi tunaowaogopa na wao pia wameichoka hii serikali na wanataka utawala mpya. Miaka mi4 ijayo watakuwa wametumaliza kabisa hawa jamaa. Kama wameona ni lazma mbunge tena wa darasa la 7 kulipwa 200,000 kwa kutega **** Bungeni kwa kikao hata kama hachangii kitu au hata kama analala kama Komba/Mrema, kwanini Dk. anayeokoa maisha ya watu asilipwe 3.5M kwa mwezi??? Kimsingi nausupport mgomo wa maDK. Na tunasubiri maDK wamalizane na Serikali ili na Sekta nyingine probably Jeshi/Malecturers waiingie kwenye mgomo mwingine, mwendo ndo huo hadi 2015.


Hiki ndo kinachompeleka huko na kuacha watu wake wanakufa.

http://www.youtube.com/watch?v=Wcw349Y5Mio
 
Hii ni mada mpya tena ? Mbona mjadala uko hapa siku kadhaa sana
Usishangae Lunyungu kwa mganga hapakauki nyimbo!! JF ndo sehemu tunapotoa dukuduku letu. Kweli kuna mada nyingi zimetaja neno DAVOS wiki hii ila sidhani kama mada zote hizo zina mtazamo mmoja. Just see whether you can add something on the topic otherwise unaweza read others' comments. This is how we normally do!
 
Inauma sana aisee! Kwakweli uongozi wa huyu jamaa umetufikisha mahali pabaya sana.
 
huyo mbona kawaida kukimbia matatizo. we si unakumbuka sakata la umeme mwaka jana si alienda south africa kutazama kaburi. we kenya kaenda w/ mkuu yeye hataki kuwaachia wenzaku
 
Kama kikao hicho angeenda waziri wa Mambo ya Nchi za Nje au wa Kilimo au wa Fedha, nchi isingepoteza million 300 mana mawaziri hawaendi na Escort/kikosi kama anavyotembeaga Mkwele. So hardly wangeenda hapo watu wa4 na hao watu wangelipwa Allowance zao kwa ujumla isingefika 50 milion na huo ujumbe alioupeleka ungefika na aliotaka kuupata huko angeupata via TV na feedback toka kwa hao ambao wangemwakilisha. Lakin upungufu wa maono na ulafi unamfanya aende yeye. Yeye anadhani marais wenzake ambao hawajaenda ndio hawataki hayo maendeleo ambaye yeye ana uchu nayo sana???Yeye ndo kasafiri sana kuliko marais wa nchi nying, kahudhuria vikao km hvyo vingi tu mbona bado anashika mkia kwa umaskin??aoni kama kwenda kwake nje inawezekana kuna correlation na umaskini wetu???


Kwa kweli kinachoongelewa WEF hapa Davos kwa level ya uchumi wa nchi yake ni kiherehere tu ndicho kilichomleta hapa. Akisema kuna mengi aliyoyapata huku atakuwa katunga mana hawa hawadiscuss gizan au ndani ya Box. Huku presdaa kilichomleta kwa kweli ni Allowance tu. Yeye angebaki nyumbani kuhangaika na uchumi/matatizo ya nchi yake. Mambo ya level ya Dunia angewaachia wazungu wayadiscuss mana ndo level yao hiyo. Anachokifanya ni kama kijana wa kimasai LAIONI (vijana wasoenda jando) kutaka kuhudhuria kikao cha MOLANI (vijana woloenda jando). Kimsingi anaonekana ni mtovu wa nidhamu
 
Watanzania ni waoga sana ukitangaza maandamano ya kumpinga rais kwa kusafiri wakati anajua nyumbani kuna m gomo ni wachache sana watajitokeza. Lakini kwa tabia hii aliyoionyesha Rais wetu sijui kama atafika 2015. Naona kama vile mwakani kuna uchaguzi wa Rais!!
 
Huu uoga ni kuna kwa kuwa bado wengi wetu wananeemeka na huu mfumo wa wizi. Ila kadri tuendeleapo, naimani point itafika ambapo watu wakipima kati ya kuwa waoga na kukusanyika kwa maandamano ya kutetea maslahi zao, wataona ni cheap kuandamana kuliko kuvumilia/kuwa waoga. Twendeni tu. Na hapo ndipo hasa wengi wetu tunapopasubiria, hakika sio mbali.
 
Hizi threads zilishaletwa hapa kwa wingi na tukachangia wewe tena unaleta, mods ondoa hii bana!
 
Yuko Addis Ababa sasa hivi kula pesa $$

a4.jpg


a6.jpg
 
Rais anapokwenda nje ya nchi anaenda kwa niaba ya watanzania wote kwa kuwa tumemwamini.wanaobeza safari za rais nje ya nchi wana chuki na husuda.
 
Rais anapokwenda nje ya nchi anaenda kwa niaba ya watanzania wote kwa kuwa tumemwamini.wanaobeza safari za rais nje ya nchi wana chuki na husuda.
Kwani marais wa nchi nyingine ambao hawazuruli hovyo hawaaminiwi na wananchi wao?? hebu toa hoja kama ulienda shule. Kwan angetuma waziri angepungua nn??Angefanya hivyo angeokoa gharama za kubeba wapambe na mbwembwe nyingine za kirais??
 
JK bwaa ni kiongozi wa ajabu sana nahisi ndiyo Raisi mubovu Afirika Mashariki na Kati kama kuna atabisha alete ushahidi hapa jf,yaani akipata mualiko anahisi kuchanganyikiwa jamani watz hebu kusikubali hili,emergency ya madr kwake si kitu,bravo madr
 
Hata kama angekuwepo there wouldn't be any difference, ktk maamuzi hakuna mwenye busara pale.sema tungeokoa tu mamilion alotumia k ktk safari.kwa ufupi tu hatuna uongozi ni kundi la wababaishaji lililo idhinishwa na nec.
 
Rais anapokwenda nje ya nchi anaenda kwa niaba ya watanzania wote kwa kuwa tumemwamini.wanaobeza safari za rais nje ya nchi wana chuki na husuda.

Toka Rais ameanza kwenda nje ya nchi zooote alizozunguka,mbona hatuoni cha maana maisha ya
watanzania ndio kwanza yanazidi kuwa magumu,kilo ya sukari 2500,mchele 2500,unga 1500
maharage 2000 nk,nauli zinapanda kila siku,umeme ndio usiseme kabisa ulivyo juu,vitu vingine
tusiongelee ushabiki tu.Ninavyojua rais akienda nje ya nchi anaenda kwa faida yake na familia
yake maana ndio inayofaidika si kwa watanzania wote.
 
Rais anapokwenda nje ya nchi anaenda kwa niaba ya watanzania wote kwa kuwa tumemwamini.wanaobeza safari za rais nje ya nchi wana chuki na husuda.

Tumia kichwa kwa kuwaza na si kukurupuka tu na kuja jamvini na majibu kama unavyojisikia kwenda chooni na unaenda tu.

Humu kuna watu wanawaza na kutoa majibu.
Tumia kichwa chako vizuri.
 
Back
Top Bottom