JK kutohudhuria mkutano wa EU!

The Khoisan

JF-Expert Member
Jun 5, 2007
15,337
12,907
JK kutohudhuria mkutano wa EU

2007-12-06 10:30:19
Na Gaudensia Mngumi


Rais Jakaya Kikwete hatashiriki mkutano wa nchi za Afrika na Ulaya unaotarajiwa kuanza Jumamosi ijayo jijini Lisbon, Ureno.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Rais hatakwenda kwenye kikao hicho cha AU na EU kutokana na kutingwa na majukumu mengi ya kitaifa.

Wizara ilisema kuwa badala yake Rais amemteua Waziri wa wizara hiyo Bw. Bernard Membe kuongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo mkubwa na wenye umuhimu kwa Afrika ambapo pamoja na mambo mengine utazungumzia ajenda za ushirikiano wa kibiashara na namna ya kuisaidia Afrika kupambana na ongezeko la joto duniani.

Wajumbe watakaoambatana na Waziri Membe ni pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Bw. Ali Mzee Ali mwingine atakayekuwa kwenye msafara wa Tanzania ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Bi. Anna Abdallah.

Mkutano huo wa EU na AU utaanza Jumamosi hadi Jumapili wiki hii nchini Ureno na kwa upande mwingine Desemba 9 siku ambayo Tanzania inaadhimisha kumbukumbu ya miaka 46 ya Uhuru wa Tanganyika.

Mkutano huo ulikumbwa na changamoto nyingi ambapo Waziri Mkuu wa Uingereza Bw. Gordon Brown, ameususia kwa madai ya kupinga ushiriki wa Rais wa Zimbabwe Bw. Robert Mugabe.

Alisema hatakwenda Lisbon iwapo Rais Mugabe ataalikwa, lakini viongozi wa Afika walipinga vitisho hivyo na kusisitiza kuwa kama kiongozi huyo wa Zimbabwe hatashiriki nao pia wataususia.

SOURCE: Nipashe
 
JK Bwana!
Ingekuwa US asingekacha! Kwa vile imekuwa Ureno ndo anamtuma Membe- kwa nini trip za US hamtumi Membe amwakilishe?

Sherehe za Uhuru must be a priority though!
 
Ametingwa na majukumu ya kitaifa ya KUTISHIA VIONGOZI WANAOZEMBEA KUWA WASIPOJIREKEBISHA ATAWATANGAZA KWA WANANCHI......Chui wa karatasi
 
Walau kwa mara ya kwanza nimesikia Rais ansema yuko busy na mambo ya ndani....sawa Mheshimiwa tuhudumie na sisi, umeenda sana kule nje kwa wakubwa na umetuletea story nyingi sana.
 
Huyu jamaa nashindwa kumuelewa, natamani sana nifahamu grade zake pale Bcom, i wounder about his capabillity. He shows lack of knowledge and decision making.
 
Huyu jamaa nashindwa kumuelewa, natamani sana nifahamu grade zake pale Bcom, i wounder about his capabillity. He shows lack of knowledge and decision making.

jhajasoma Bcom kasoma B.A Economics pale Mlimani ,Sababu ya kutokwenda Ureno ni kwasababu ya siku ya kuadhimisha Uhuru wa Tanganyika,Hawezi kuacha siku hiyo na akaenda huko Ulaya,sababu yeye ndiye amri jeshi mkuu wa nchi na lazima akague gwaride siku hiyo ya jumapili.ila kama isingekuwa hivyo angekwenda huko.
 
Kwani mkutano ni lini? angalieni mumesahau kuwa sherehe ya uhuru wa Tanganyika, au mumesahau hata uhuru wa nchi yenu?
 
Jamani hivi Tanganyika si ilishakufa?. kusherehekea uhuru wake ina maana gani wakati haipo?. mimi nafikiri siku ya Muungano, ile ya kuzaliwa Tanzania haswaa ndo ingepaswa kupewa kipaumbele. otherwise kusherehekea siku kuu ya Tanganyika kwa gharama ya kuacha kufanya kazi zenye Maslahi Kwa Tanzania ni kutoutendea haki upande wa pili wa muungano. hili mnalionaje?
 
Ndugu ni lazima uhuru usherekewe kwa nguvu zote. Jambo hilo lisipuuzwe kabisa. Gamba la nyoka naona kama historia ya nchi yako inakutoka..angalia sana! Muungano wa Tanganyika na Zanzibari sio uliotupatia uhuru. Tulipata uhuru kabla ya muungano na baada ya kuwa na uhuru kwa miaka 3 ndio wazee wetu wakaamua kuunganisha nuvu ya pamoja ili kuleta ushindani wa kitaifa katika mataifa.
Udhuru wa JK kutohudhuria huo mkutano ninausupport kabisa. There is no way aondoke aende kwenye mkutano wakati wananchi na taifa zima wanasherehekea historia ya nchi yao kuwa huru. Hata marais wenzake wangemcheka sana. Kwa hiyo kwa hili....naomna tumuelewe.
 
Hivi wanapotangaza hizi sherehe huwa wanasema WTZ tunasherekea sikukuu gani vile? Uhuru wa nchi gani? Maana Tanganyika haiko kwenye misamiati ya SISIM!!!!
 
Wanasema :Tunashehekea uhuru wa chi yetu" au "Tunashekea uhuru wa Tanzania au "Tanzania independent day"
Hakuna sababu ya kulitumia jina la la zamani (tanganyika) eti kwasababu tulilpota uhuru tulikuwa bado hatujaungana
 
Ktk wasifu wote JK is right ku-deligate hiyo safari kwa Ben Membe.

Uhuru ni uhuru haijalishi kuwa ni wa unguja au Kyela,pengine tusaidiane kwa data ni lini gwaride la uhuru lilimkosa Amir Jeshi wake mkuu ukiondoa Mkapa alipoumwa mguu na Kaimu Rais Shein kubeba mikoba lakini Ben alijikuta anafidia gwaride lake hilo baada ya mgombea mwenza wa Mbowe kufa na kusogeza mbele campaign hiyo kumpatia haki Benjamin Mkapa ukaguzi wa kumi wa gwaride la uhuru.

Tupatieni data pevu sana ktk hili otherwise Comrade JK yuko sahihi kuliko kawa
 
Jamani hivi Tanganyika si ilishakufa?.

..ilikufa lini?kwani tanzania ni nini?...tanganyika + zanzibar = tanzania! simple math!

kusherehekea uhuru wake ina maana gani wakati haipo?. mimi nafikiri siku ya Muungano, ile ya kuzaliwa Tanzania haswaa ndo ingepaswa kupewa kipaumbele.

..do you want to rewrite history?unakumbuka the soviet union?

otherwise kusherehekea siku kuu ya Tanganyika kwa gharama ya kuacha kufanya kazi zenye Maslahi Kwa Tanzania ni kutoutendea haki upande wa pili wa muungano. hili mnalionaje?

..kwani wao hawasherehekei ya kwao? mbona wana bendera yao na wimbo wao wa taifa?

..au unataka nasi tuulizie vya kwetu?
 
Lakini kwanini tusema ni sherehe za uhuru wa Tanzania badala ya Tanganyika??? Hivi kwa nini SISIM hawataki kusikia Tanganyika inatajwa?? Kama kweli Tnganyika imebadilika kuwa Tanzania basi sherehe za mapinduzi ya Zanzibar wawe wanasema mapinduzi ya Tanzania pia!!!!
 
He cant win! Kama angeenda Lisbon ooh Vasco Da Gama... Kabaki kuenzi siku yetu ya uhuru still u complain...

Jamani hata uhuru wetu nao tumesahau! Kweli hiki kizazi kipya... kakamua kwenda kwa mbele..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom