JK kukiri hali ya fedha serikalini ni mbaya

...Nchi ina utajiri wa kutisha...Dhahabu, Almasi, Tanzanet, misitu ardhi yenye rutuba ya hali ya juu lakini wanaofaidika ni wageni na mafisadi walio Serikalini na marafiki zao huku nchi ikishindwa kuwa na pesa hata za kujiendesha. Majirani zetu Botswana dhahabu yao wanagawana pasu kwa pasu na wawekezaji (50%) sie tunawaachia wachukuaji wachukue 97% ya mapato yote yanayotokana na dhahabu yetu ikiwafaidisha shareholders wao na wale walio katika managament positions za makampuni ya wachukuaji huku nchi ikikosa hata pesa za kulipa mishahara kwa Wafanyakazi wake!!!!
 
Yaani mambo bado kuwa magumu zaidi ya hapo subirini kidogo mtaona wengine wakikitoa wenyewe tu. Hela nyingi zilitumbuliwa kwenye uchaguzi kutoka kwenye vyanzo mbalimbali serikalini na sasa wahisani nao wametia ngumu ile mbaya bado tu kutangazwa.
 
Yaani mambo bado kuwa magumu zaidi ya hapo subirini kidogo mtaona wengine wakikitoa wenyewe tu. Hela nyingi zilitumbuliwa kwenye uchaguzi kutoka kwenye vyanzo mbalimbali serikalini na sasa wahisani nao wametia ngumu ile mbaya bado tu kutangazwa.


kabla hawajakitoa wakamateni ninyi wananchi.......
 
tokeni behewa la mwisho....nendeni mpaka kwenye kichwa cha treni mtoeni dreva hapo kwenye kiti...mbona kuna dreva mzuri tu anaweeza kuliendesha gari moshi hili kwa ustadi mkubwa!!?!! muwekeni huyo aendeshe na mtafika salama ...achaneni na hawa wezi na waongo wakubwa......
 
nilishawahi kusema...huyo rais hana tofaiti na mti wa ashok.....ule mti haufai kwa kivuli...haufai kwa kujengea.....haufai kwa kuchanwa mbao...haufai kwa kupikia kama kuni....haufai hata kuwa mkongojo wa babu...zaid sana ule miti hutumika kama mapango na makazi ya wale nyoka wa KIJANI!!!.........
 
Sasa anatuambia ili tufanye nini,serikali yake ni ya kulaumiwa moja kwa moja katika hili.Watanzania wazalendo tulisema kwamba serikali ilikokuwa inakwenda ilikuwa siko,igeuke lakini hatukusikilizwa.Matumizi mabaya ya fedha za uma,ikiwa ni pamoja na wizi wa wazi wa rasilimali za taifa,kutoa rasilimali za nchi kwa bei ya kutupa,misamaha ya kodi kwa njia za rushwa,kushindwa kuwa wabunifu katika ukusanyaji wa kodi,nk,nk.haya yote ndio yametufikisha hapa tulipo.FEDHA SASA ZIKO KWENYE MIFUKO YA WATEULE WACHACHE.Je akina Kikwete, tuwaache hivi hivi hata baada ya kufilisi taifa letu,no lazima tutawashughulikia,hatukubali.Nchi yetu ni tajiri mno,hatukupashwa kufika hapa.Kikwete ajiuzulu tupate mtu mwingine ambaye ataweka mikakati mizuri ya ku-manage uchumi wa nchi yetu.Ameshindwa.Muda uliobaki ni mwingi mno,tukiendelea naye atatupeleka makaburini.
JK akiri hali ni mbaya serikalini Send to a friend
Saturday, 04 February 2012 09:06
0digg
dola-jk.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Spika wa Bunge, Anne Makinda wakati wa maadhimishO ya Siku ya Sheria yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam jana.Kushoto ni Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman.Picha na Zacharia Osanga​
James Magai
RAIS Jakaya Kikwete amekiri kuwa katika kipindi hiki Serikali iko katika hali mbaya kifedha kiasi kwamba inashindwa kutekeleza shughuli katika idara mbalimbali kwa wakati. Rais Kikwete alitoa kauli hiyo jana wakati akitoa salaamu za maadhimisho ya Siku ya Sheria zilizofanyika nje ya Viwanja vya Mahakama Kuu Dar es Salaam. Kauli hiyo ya Kikwete ilitokana na kilio cha Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman kuwa Mahakama nchini imekuwa ikishindwa kutekeleza majukumu yake kwa mafanikio kutokana na ama kucheleweshewa pesa au kupewa chini ya mahitaji.

Jaji Othman alisema fedha zilizoidhinishwa na Bunge mwaka 2011/2012 kwa ajili ya Mfuko wa Mahakama ni Sh 20bilioni, lakini katika kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba 31 walitegemea kuwa na Sh 10bilioni, lakini wamepewa Sh6,327,796,972 tu. Akijibu kilio hicho, Rais Kikwete alikiri kuwepo kwa uhaba wa fedha serikalini, lakini akabainisha kuwa hali hiyo imetokana na hatua ya kulipia malimbikizo ya madeni ya nyuma.

“Sehemu kubwa ya mapato ya Serikali katika hii nusu ya kwanza, imetumika kwa ajili ya kulipia malimbikizo ya madeni ya nyuma,” alisema Rais Kikwete bila kufafanua madeni hayo yaliyolipwa na kuongeza kuwa hata wizara nyingine nazo hazikuweza kupewa pesa kama zilivyostahili kwa mara moja. Alisema karibu madeni hayo yatamalizika kulipwa na kwamba mpaka sasa zimebakia kama Sh 40bilioni tu.

Pia Kikwete aliihakikishia Mahakama kuwa ataipatia kiasi chote cha fedha iliyoidhinishwa na Bunge huku akikiri kuwa hata kiasi hicho pia bado ni kidogo. “Itabidi hata tupunguze sehemu nyingine, kuna maeneo mengine wana bajeti ya matrilioni ambazo sidhani kama katika kipindi hiki cha miezi sita zitaweza kuwa zimetumika zote kwa mara moja,” alisema Rais Kikwete.

Jaji Mkuu Othman akifafanua zaidi ucheleweshaji wa pesa za matumizi ya Mahakama alisema kuwa inakuwa ni vigumu kuweza kupata mafanikio ya wazi na kwamba hali hiyo inachangia kukwamisha uendeshaji wa Mahakama.

“Tunashindwa kuwalipa wafanyakazi haki zao wanazostahili kwa sababu ya ukosefu wa stahili za uhamisho, pia inakuwa vigumu kuwahamisha mahakimu na wafanyakazi wengine," alisema.

Hivi sasa kuna mahakimu wa Mahakama za Mwanzo 75 na wafanyakazi wa kada nyingine 500 ambao wamekaa kwenye vituo vya kazi kwa zaidi ya miaka kumi. Hili linapunguza motisha, ufanisi na tija,” alisema Jaji Othman.
 
unatumia nini kufikiri wewe, kama akina Obama nao wanalalamika kuwa hali za nchi zao kiuchumi ni mbaya sembuse kanchi ketu kachanga

We Makupa ndo unafikiria kwa kutumia Kitundu cha katikati ya masaburi yako kupembua hoja..! Unathubutu kulinganisha Amerika na Tz kiuchumi, Tuseme ukweli huyu Mk'were anatuzingua tu, hamna kitu anafanya takwimu nyingi zathibitisha hili
 
unatumia nini kufikiri wewe, kama akina Obama nao wanalalamika kuwa hali za nchi zao kiuchumi ni mbaya sembuse kanchi ketu kachanga

Nani alikwambia nchi changa lazima iwe na matatizo ya kiuchumi? Tutakua baada ya miaka mingapi?
Ulipotokea mtikisiko wa kiuchumi duniani mlisema hamtatikisa. Huo upepo wa kuwatikisa umetoka wapi?
 
huyo unayemwita rais wako amechaguliwa na nani??....dhambi ya kuiba ushindi wa mtu mwingine ina mtafuna na ndio maana nchi imemshinda.......na ninyi mnaomfuta miguu hamna lolote zaid ya njaa ndio maana mnamfuta miguu....kama pesa hakuna hata hiyo mipango itatekelezwa?!!!

mtu anaeshindwa kulinda kura anaweza kweli kulinda rasilimali zetu?
 
sitaki kuchanganywa na wala sidanganyiki. Hivi bajeti ya mwaka huu haikuwa na pesa ya kulipa madeni? Ni madeni yapi ya nyuma ambayo hayakuwepo kwenye bajeti lakini sasa yanalipwa hata hivyo? TRAInasemekana imekusanya zaidi ya matarajio kwa maana ya asilimia 102 ni nini basi kinasababisha makusanyo yawe mengi zaidi ya makadirio ya matumizi na hata hivyo shughuli za maendeleo zilizopangiwa hayo makusanyo zisiyapate?
Nchi ya usanii mtupu hii!!
.
 
Tuambie ww kuhusu raisi wako na mipa
ngo ya nchi yako au ww wa italy mwenzetu
pesa nyingi wanazitumia kutafuta watu waliowatangaza wao kuwa wamekufa.......ni lazima nchi iishiwe pesa..watanzania amkeni..muondoeni huyo ni mzigo kwa taifa lenu
 
Tatizo anakuwa wa mwisho kuelewa kila jambo. Waliambiwa wakabisha, ngoja tuone mwisho.
 
JK akiri hali ni mbaya serikalini Send to a friend
Saturday, 04 February 2012 09:06
0digg
dola-jk.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Spika wa Bunge, Anne Makinda wakati wa maadhimishO ya Siku ya Sheria yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam jana.Kushoto ni Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman.Picha na Zacharia Osanga​
James Magai
RAIS Jakaya Kikwete amekiri kuwa katika kipindi hiki Serikali iko katika hali mbaya kifedha kiasi kwamba inashindwa kutekeleza shughuli katika idara mbalimbali kwa wakati. Rais Kikwete alitoa kauli hiyo jana wakati akitoa salaamu za maadhimisho ya Siku ya Sheria zilizofanyika nje ya Viwanja vya Mahakama Kuu Dar es Salaam. Kauli hiyo ya Kikwete ilitokana na kilio cha Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman kuwa Mahakama nchini imekuwa ikishindwa kutekeleza majukumu yake kwa mafanikio kutokana na ama kucheleweshewa pesa au kupewa chini ya mahitaji.

Jaji Othman alisema fedha zilizoidhinishwa na Bunge mwaka 2011/2012 kwa ajili ya Mfuko wa Mahakama ni Sh 20bilioni, lakini katika kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba 31 walitegemea kuwa na Sh 10bilioni, lakini wamepewa Sh6,327,796,972 tu. Akijibu kilio hicho, Rais Kikwete alikiri kuwepo kwa uhaba wa fedha serikalini, lakini akabainisha kuwa hali hiyo imetokana na hatua ya kulipia malimbikizo ya madeni ya nyuma.

“Sehemu kubwa ya mapato ya Serikali katika hii nusu ya kwanza, imetumika kwa ajili ya kulipia malimbikizo ya madeni ya nyuma,” alisema Rais Kikwete bila kufafanua madeni hayo yaliyolipwa na kuongeza kuwa hata wizara nyingine nazo hazikuweza kupewa pesa kama zilivyostahili kwa mara moja. Alisema karibu madeni hayo yatamalizika kulipwa na kwamba mpaka sasa zimebakia kama Sh 40bilioni tu.

Pia Kikwete aliihakikishia Mahakama kuwa ataipatia kiasi chote cha fedha iliyoidhinishwa na Bunge huku akikiri kuwa hata kiasi hicho pia bado ni kidogo. “Itabidi hata tupunguze sehemu nyingine, kuna maeneo mengine wana bajeti ya matrilioni ambazo sidhani kama katika kipindi hiki cha miezi sita zitaweza kuwa zimetumika zote kwa mara moja,” alisema Rais Kikwete.

Jaji Mkuu Othman akifafanua zaidi ucheleweshaji wa pesa za matumizi ya Mahakama alisema kuwa inakuwa ni vigumu kuweza kupata mafanikio ya wazi na kwamba hali hiyo inachangia kukwamisha uendeshaji wa Mahakama.

“Tunashindwa kuwalipa wafanyakazi haki zao wanazostahili kwa sababu ya ukosefu wa stahili za uhamisho, pia inakuwa vigumu kuwahamisha mahakimu na wafanyakazi wengine," alisema.

Hivi sasa kuna mahakimu wa Mahakama za Mwanzo 75 na wafanyakazi wa kada nyingine 500 ambao wamekaa kwenye vituo vya kazi kwa zaidi ya miaka kumi. Hili linapunguza motisha, ufanisi na tija,” alisema Jaji Othman.

Wakati anaapishwa mwaka 2005 nakumbuka neno moja kubwa alilosema (NIMEHEMEWA) alikuwa anajua maana yake??
 
wewe mwenyewe hapo matonya namba moja.utatueza nini mpya.acha wenye akili timamu na wenye mapenzi na nchi yetu wawahudumie walalamikaji kama wewe.

unategemea nini kama nchi yenye utajiri mkubwa wa rasilimali kuendelea kuwa omba omba?
 
Kwani Obama ni nani mpaka akilalamika iwe ajabu? Swala ni sababu za kukosekana hizo fedha; Kikwete anadai ni kutokana na kulipia madeni ya nyuma, huu ni uongo mtupu na usio na aibu. Fedha zimekwisha kutokana na matumizi mabaya na wizi wake yeye na serikali yake na chama chao, hakuna ukweli wowote kuhusu madeni hapo.

Pia akina obama kulalamika siyo sababu ya sisi kuzidi kuwa omba omba. Hapa bila unafiki Jk siyo uongozi wake legelege ndo unasababisha yote haya, wakati ni sasa kuwa mstarabu na kuonyesha uzalendo wa kujiuzulu atuachie nchi yetu wenyekuweza watuongoze
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom