BAADA ya kufanya mabadiliko kwenye Baraza lake la Mawaziri, Rais Jakaya Kikwete sasa anatarajia kuifumua sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumatano imebaini. Vyanzo vya habari kutoka ndani ya CCM, vilisema kuwa Rais Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho taifa, ameamua kuitisha vikao vya chama ghafla pamoja na mambo mengine, kufanya mabadiliko kwenye sekretarieti yake.
Duru za kisiasa kutoka ndani ya chama hicho tawala, zilisema kuwa mabadiliko hayo yanatokana na mmoja kati ya wajumbe wa sekretarieti, Januari Makamba, kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Sayansi Teknolojia na Elimu ya Juu.
Kama utakumbuka mara ya mwisho Rais Kikwete aliamua kuwaondoa mawaziri wote kwenye sekretarieti ya chama ili wajumbe hao waweze kufanya kazi muda wote. Alimwondoa Waziri Bernard Membe, Nape akalazimika kuachia u-DC. Kwa vile Makamba amekuwa waziri ni wazi kwamba ataachia nafasi hiyo na Rais ataijaza kwa kumteua mjumbe mwingine, kilisema chanzo chetu cha habari.
Wajumbe wengine wa sekretarieti hiyo ni pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Mhasibu Mkuu, Mwigulu Nchemba, Martin Shigela, Amina Makilage, Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenister Mhagama, John Chiligati, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Vuai Ali Vuai, Asha Juma na Katibu Mkuu, Willson Mkama.
Katika kujaza nafasi hiyo, Rais Kikwete anaweza kuwagusa wajumbe wengine kama ataona kuna ulazima wa kufanya hivyo.
Ukiachia mabadiliko hayo, vikao hivyo vya CCM ambavyo vinaanza Mei 11 hadi 14, vinajadili mambo mbalimbali, ikiwemo hali ya kisiasa ndani ya chama hicho hasa kipindi hiki ambapo kinakabiliwa na kukimbiwa na wimbi la wanachama wake.
Kuna mambo mazito ya kujadili. Kasi ya CHADEMA na ushindi wake Arumeru imeibua hofu, wimbi la wanahama wa CCM kuhamia CHADEMA, mpasuko ndani ya chama, suala la uchaguzi wa chama na mjadala wa Katiba ni baadhi ya mambo yatakayoibua mjadala mzito, alisema mtoa habari wetu.
Mtoa habari wetu alisema kuwa kikao hicho pia kinaweza kuwaweka kiti moto wabunge wa CCM walioungana na wenzao wa upinzani kutia saini za kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Kwa mujibu wa ratiba ya vikao hivyo kuanzia jana hadi Mei 11 kutakuwa na vikao vya maandalizi, Kamati ya Maadili kukutana Mei 12 asubuhi na Kamati Kuu (CC) chini ya Rais Kikwete itakutana siku hiyohiyo jioni.
Mei 12 kutakuwa na semina maalumu kwa wajumbe wote wa CC na NEC na Mei 14 itakuwa siku ya NEC.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Nape alisema kuwa vikao hivyo ni maalumu kwa ajili ya wajumbe kujadili mjadala wa Katiba mpya.
Alipoulizwa kama kuna hatua zozote ambazo zitachukuliwa na kwa baadhi ya wabunge waliosaini fomu ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Nape alisema hoja hiyo haipo na haiwezi kuwepo kwani wabunge hao walitoa haki yao Kikatiba kuwawakilisha wananchi wao.
Kwanza ikumbukwe kuwa Rais akiwa Tanga aliwapongeza wabunge kwa kuonyesha msimamo wao leo itakuwaje Rais tena awageuke na kuanza kuwawajibisha? Hilo halipo kabisa! alisema.
Katika hatua nyingine, Nape alisema mawaziri wote waliotuhumiwa wawajibishwe kwa uzito wa makosa yao kama watabainika kuhusika.
Hakuna mtu aliye juu ya sheria, kama mawaziri wanaotuhumiwa kufanya ubadhirifu wako ndani ya Baraza la Mawaziri au wale walioachwa ni lazima kila mmoja achukuliwe hatua kadiri ya kosa lake, kama leo hii Rais mstaafu Benjamin Mkapa kafikishwa mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi itakuwa Baraza la Mawaziri? alihoji Nape
Watanzania wanachotaka kwa sasa ni kuona HATUA KALI zinachukuliwa dhidi ya mafisadi! Tofauti na hapo hata kama yakifanywa mabadiliko gani ccm haina chake tena 2015.
JK bwana ananiacha hoi sana. mtu unaweza kufumua kitu ambacho hakijasukwa? yeye aseme anaiua moja kwa moja manake atakapoawatoa mavuvu zela Nape lazima waje waombe kombat huku pipoz power street.
Wanatapatapa na matamko ya CDM..ya kutaka kujitenga iwapo hawatapata mgombea wa urais kama wale vijana wa pwani walivyosema kuwa rais hatatoka kaskazini!wanataka kujitenga kuunda nchi ya Meru!kazi ipo hapo ngoja tuone
Watanzania wanachotaka kwa sasa ni kuona HATUA KALI zinachukuliwa dhidi ya mafisadi! Tofauti na hapo hata kama yakifanywa mabadiliko gani ccm haina chake tena 2015.
Nimesoma kurasa fulani wameandika matatizo ya Chuo Kikuu cha Dodoma. Inafaa Kamati Kuu imshauri rais amwondoe yule Profesa wa UDOM anayekiharibu chuo. Mimi naona wanafunzi wanaomaliza vyuo ni watu hatari sana kuliko wazee wa vijijini. Tukitenda mema vyuoni CCM itakuwa inajihakikishia uwingi wa wapiga kura katika chaguzi zijazo. Kinyume cha hapo ni madhara makubwa. CCM shinikiza kuondolewa kwa profesa wa Kiswahili anayetajwatajwa pale UDOM HARAKA. TUSIWE SIKIO LA KUFA HALISIKII........
JK hana ubavu wa kuifumua CCM. Juzi tu hapa alitaka kumuondoa Mkulo na wezi wenzie ilibidi akaombe ridhaa CC ya chama, leo hii mwombaji akawe mpaji, mmh! Puruzai za barazani hizi, hakuna jipya.
Na kama mmesahau, kumbukeni kile kikao cha kuvuana magamba last year. Baada ya Lowassa kumwaga data, nani aliyenywea zaidi ya JK?
Habari JF,
Kama anayohisi mwandishi ndio maudhui ya vikao; then makosa yamefanyika tangu siku nyingi na yana mzizi mrefu. Hit and run techniques may not work at the moment, naamini watanzania wa leo tunataka vitendo zaidi ya maneno. For decades , CCM leaders took this country for granted, it's time to learn a lesson.
CDM watasubili sana kwani CCM imejipanga na ina mizizi minene ambayo haing'ooki kwa mbwembwe za CDM ambazo hazina mafanikio kwa Taifa.CCM OYEEE! nasema CDM wanapenda na wanatamani CCM isambaratike lakini hiyo ni ndoto ya alinacha.CCM ina wenyewe na wenyewe ni wanachama na watanzania wanaojua na wanaoitakia mema Tanzania.Kidumu Chama Tawala Cha CCM.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.