BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Imetolewa mara ya mwisho: 22.11.2008 0010 EAT
JK kufanya mabadiliko
*Vigogo wengi wahaha,wakosa usingizi
*Ni walioshindwa kwenda na kasi mpya
Na Mwandishi Wetu
Majira
RAIS Jakaya Kikwete huenda akafanya mabadiliko makubwa ya wakuu wa wilaya mbalimbali nchini hivi karibuni ili kuhakikisha anapata wachapakazi makini hasa katika kipindi hiki utawala wake ukielekea kutimiza miaka mitatu, vyanzo vya kuaminika Serikalini vimelithibitishia Majira.
Kwa mujibu wa habari za ndani Serikalini, mabadiliko hayo makubwa, huenda yakatangazwa mwezi ujao, iwapo Rais ataamua, na yataibua mtikisiko katika utawala wa wilaya nyingi ambako wengi kati ya wakuu hao wameonekana kujisahahu kiutendaji na kufanyakazi aidha kwa mazoea au wakiacha kulinda maslahi ya wananchi badala yake wakikumbatia wawekezaji,matajiri au wengine kutokuwa na mbinu mpya katika utawala.
Chanzo hicho kilicho katika safu andamizi za Serikali, kilisisitiza kuwa timu mpya ya wakuu hao wa wilaya tayari imeshapangwa na kitu kilichobaki kwa sasa ni hatua ndogo ndogo za mwisho.
"Uamuzi huo wa mabadiliko utatangazwa hivi karibuni inawezekana kabisa mwezi ujao au mapema Januari na hii imetokana na baadhi ya wakuu hao kutowajibika ipasavyo hivyo kukwamisha juhudi za Serikali iliyoko madarakani," kilisema chanzo hicho.
Kiliendelea kusema kuwa sura kadhaa mpya za wakuu hao zinatarajia kujitokeza na uteuzi huo ambao unafanywa na Rais Jakaya Kikwete akipata ushauri wa karibu kutoka kwa Waziri Mkuu wake, Bw. Mizengo Pinda, unaelezwa utakuwa makini zaidi ili kuhakikisha hawachukuliwi watu ambao utendaji wao utakuwa na upungufu tena hasa wakati huu Serikali inapoelekea kukamilisha malengo ya sera zake katika awamu ya kwanza ya uongozi wa Rais Kikwete kabla hajaomba tena ridhaa ya kuongoza awamu ya pili mwaka 2010.
Aidha chanzo hicho kiliendelea kusema kuwa fungu la fedha ambalo lilikuwa limekwamisha uteuzi huo mpya tayari limepatikana ambalo litawawezesha watendaji wapya na wale wa zamani watakaobadilishwa kusafiri kutoka mahali walipo na kwenda katika vituo vyao vipya vya kazi.
"Unajua sasa hivi mambo yamebadilika, hawataki tena kuangalia ukada wa chama au mambo ya siasa. Kinachotakiwa ni uchapakazi hivyo kuna hatari ya wengi kupoteza nafasi walizonazo kwani lengo kubwa lililokuwepo ni kuwajibika kwa wananchi lakini wamekuwa hawasaidii chochote kwenye nafasi walizopewa.
Wanatakiwa wakuu wa wilaya ambao watakaa kwenye nafasi zao na kuwajibika kama Serikali ya Awamu ya Nne ilivyokusudia. Ubabaishaji sasa hivi hautakiwi," kilisisitiza chanzo chetu.
Wiki iliyopita Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda alifanya ziara mkoani Dodoma ambako aliwaambia wakuu wa mikoa na wilaya kuwa watapimwa kwa vigezo vipya ambavyo vitawekwa ili kubaini utendaji wao na watakaoshindwa wataondolewa.
Bw. Pinda alisema kuwa viongozi wote wa ngazi hiyo wanatakiwa kuwajibika hasa kwa kuwafikia wananchi vijijini ambako watahamasisha kilimo chenye tija ili kuleta mabadiliko katika sekta ya kilimo.
Rais Jakaya Kikwete pia amekuwa akikutana na vituko vya baadhi ya wakuu wa wilaya kuonekana wanafanyakazi kwa mazoea tu katika ziara zake nyingi za mikoani hali iliyomfanya katika baadhi ya maeneo alazimike kuwasimajisha watendaji kujibu maswali hadharani.
Hata katika ziara za Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Bw. Edward Lowassa, matukio ya wakuu hao wengi kuonekana wanafanyakazi kwa kukurupuaka yalionekana huku malalamiko ya wananchi katika vyombo vya habari wakati fulani yakiwahusisha wakuu hao katika tuhuma kama vile kukumbatia wawekezaji wanaonyanyasa wananchi, kushindwa kwao kuwasikiliza wananchi na kutatua shida zao na wengi pia kukosa mbinu madhubuti za kiutawala.
Wakuu wote wa wilaya 137 zilizopo nchini waliwahi kuitwa kwenye semina maalum iliyofanyika kwenye Hoteli ya Ngurdoto, Arusha, ambako 'walifundwa' na Rais Jakaya Kikwete mwenyewe na viongozi wengine waandamizi Serikalini ili wajue wajibu wao katika kuwatumikia wananchi.
Vyanzo vyetu vimepasha zaidi kuwa mkutano huo uliohudhuriwa na wakuu hao kwa furaha na matumaini, ndio ambao sasa ni sehemu ya kitanzi chao, kwani utekelezaji wa yaliyokubaliwa katika mkutano huo, ni fimbo mojawapo itakayotumika 'kuwachapa' wale walioshindwa kutimiza wajibu wao.
JK kufanya mabadiliko
*Vigogo wengi wahaha,wakosa usingizi
*Ni walioshindwa kwenda na kasi mpya
Na Mwandishi Wetu
Majira
RAIS Jakaya Kikwete huenda akafanya mabadiliko makubwa ya wakuu wa wilaya mbalimbali nchini hivi karibuni ili kuhakikisha anapata wachapakazi makini hasa katika kipindi hiki utawala wake ukielekea kutimiza miaka mitatu, vyanzo vya kuaminika Serikalini vimelithibitishia Majira.
Kwa mujibu wa habari za ndani Serikalini, mabadiliko hayo makubwa, huenda yakatangazwa mwezi ujao, iwapo Rais ataamua, na yataibua mtikisiko katika utawala wa wilaya nyingi ambako wengi kati ya wakuu hao wameonekana kujisahahu kiutendaji na kufanyakazi aidha kwa mazoea au wakiacha kulinda maslahi ya wananchi badala yake wakikumbatia wawekezaji,matajiri au wengine kutokuwa na mbinu mpya katika utawala.
Chanzo hicho kilicho katika safu andamizi za Serikali, kilisisitiza kuwa timu mpya ya wakuu hao wa wilaya tayari imeshapangwa na kitu kilichobaki kwa sasa ni hatua ndogo ndogo za mwisho.
"Uamuzi huo wa mabadiliko utatangazwa hivi karibuni inawezekana kabisa mwezi ujao au mapema Januari na hii imetokana na baadhi ya wakuu hao kutowajibika ipasavyo hivyo kukwamisha juhudi za Serikali iliyoko madarakani," kilisema chanzo hicho.
Kiliendelea kusema kuwa sura kadhaa mpya za wakuu hao zinatarajia kujitokeza na uteuzi huo ambao unafanywa na Rais Jakaya Kikwete akipata ushauri wa karibu kutoka kwa Waziri Mkuu wake, Bw. Mizengo Pinda, unaelezwa utakuwa makini zaidi ili kuhakikisha hawachukuliwi watu ambao utendaji wao utakuwa na upungufu tena hasa wakati huu Serikali inapoelekea kukamilisha malengo ya sera zake katika awamu ya kwanza ya uongozi wa Rais Kikwete kabla hajaomba tena ridhaa ya kuongoza awamu ya pili mwaka 2010.
Aidha chanzo hicho kiliendelea kusema kuwa fungu la fedha ambalo lilikuwa limekwamisha uteuzi huo mpya tayari limepatikana ambalo litawawezesha watendaji wapya na wale wa zamani watakaobadilishwa kusafiri kutoka mahali walipo na kwenda katika vituo vyao vipya vya kazi.
"Unajua sasa hivi mambo yamebadilika, hawataki tena kuangalia ukada wa chama au mambo ya siasa. Kinachotakiwa ni uchapakazi hivyo kuna hatari ya wengi kupoteza nafasi walizonazo kwani lengo kubwa lililokuwepo ni kuwajibika kwa wananchi lakini wamekuwa hawasaidii chochote kwenye nafasi walizopewa.
Wanatakiwa wakuu wa wilaya ambao watakaa kwenye nafasi zao na kuwajibika kama Serikali ya Awamu ya Nne ilivyokusudia. Ubabaishaji sasa hivi hautakiwi," kilisisitiza chanzo chetu.
Wiki iliyopita Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda alifanya ziara mkoani Dodoma ambako aliwaambia wakuu wa mikoa na wilaya kuwa watapimwa kwa vigezo vipya ambavyo vitawekwa ili kubaini utendaji wao na watakaoshindwa wataondolewa.
Bw. Pinda alisema kuwa viongozi wote wa ngazi hiyo wanatakiwa kuwajibika hasa kwa kuwafikia wananchi vijijini ambako watahamasisha kilimo chenye tija ili kuleta mabadiliko katika sekta ya kilimo.
Rais Jakaya Kikwete pia amekuwa akikutana na vituko vya baadhi ya wakuu wa wilaya kuonekana wanafanyakazi kwa mazoea tu katika ziara zake nyingi za mikoani hali iliyomfanya katika baadhi ya maeneo alazimike kuwasimajisha watendaji kujibu maswali hadharani.
Hata katika ziara za Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Bw. Edward Lowassa, matukio ya wakuu hao wengi kuonekana wanafanyakazi kwa kukurupuaka yalionekana huku malalamiko ya wananchi katika vyombo vya habari wakati fulani yakiwahusisha wakuu hao katika tuhuma kama vile kukumbatia wawekezaji wanaonyanyasa wananchi, kushindwa kwao kuwasikiliza wananchi na kutatua shida zao na wengi pia kukosa mbinu madhubuti za kiutawala.
Wakuu wote wa wilaya 137 zilizopo nchini waliwahi kuitwa kwenye semina maalum iliyofanyika kwenye Hoteli ya Ngurdoto, Arusha, ambako 'walifundwa' na Rais Jakaya Kikwete mwenyewe na viongozi wengine waandamizi Serikalini ili wajue wajibu wao katika kuwatumikia wananchi.
Vyanzo vyetu vimepasha zaidi kuwa mkutano huo uliohudhuriwa na wakuu hao kwa furaha na matumaini, ndio ambao sasa ni sehemu ya kitanzi chao, kwani utekelezaji wa yaliyokubaliwa katika mkutano huo, ni fimbo mojawapo itakayotumika 'kuwachapa' wale walioshindwa kutimiza wajibu wao.