LATTICE BOND
JF-Expert Member
- May 30, 2011
- 219
- 48
Tunatakiwa kabla ya kuandika katiba mpya yafanyike marekebisho ya katiba iliyopo ili kutoa mwanya unaoruhusu vyama vyote vya siasa kufutwa na kuundwa upya pasipo kutumia majina ya awali. Kwa kufanya hivyo ushawishi wa vyama vya awali utaondolewa rasmi miongoni mwa watendaji wa serikali. Kwa kuondoa ushawishi wa wanasiasa kutasaidia kupata mwelekeo chanya wa uwajibikaji kuelekea katiba mpya. Kama tutakimbilia kuandika Katiba mpya katika kipindi hiki ambacho ndugu yetu Nape na wenzake wanaamini nchi hii ni yao [nukuu ya hotuba yake tarehe 9/10/2011] tutabaki kulekule tunapopakataa!! Pia mali zote [assets] za ccm na vyama vingine zirudishwa serikali sambamba na kuvifuta.