Kikwete awaonya wanafunzi vyuo vikuu:
Imeandikwa na Mwandishi Maalumu, Dodoma; Tarehe: 27th November 2010 @ 07:20 Imesomwa na watu: 333; Jumla ya maoni: 0
RAIS Jakaya Kikwete, amewataka wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, kujiepusha kutumiwa na wanasiasa na badala yake kuelekeza nguvu zao katika masomo.
Alitoa kauli hiyo mkoani hapa jana katika mahafali ya kwanza ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na kuwaasa kuwa wanasiasa wanafanya hivyo kwa maslahi yao kwa kuwa walishamaliza masomo yao.
Kwa nyie mnaoendelea na masomo yenu, elekezeni nguvu zenu kwenye masomo. Hilo ndilo lililowaleta hapa. Msikubali kurubuniwa na wanasiasa. Hawa wanataka kuwatumia tu kwa manufaa yao kwa sababu masomo yao walikwishamaliza.
Ukijiingiza katika michezo hii ya siasa ni dhahiri utaharibikiwa. Ama utashindwa na kulazimika kurudia masomo ama utafukuzwa kabisa baada ya kushindwa kupata alama za kukuwezesha kuendelea mbele au hata kurudia mitihani, alisema Rais Kikwete ambaye pia alitunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima (PhD).
Aliwaasa wanafunzi hao kujishughulisha na jukumu lililowaleta chuoni hapo ambalo ni kusoma na wala siyo kushiriki siasa.
Msiwape nafasi wanasiasa kwa sababu watawaharibieni muda na malengo yenu. Mtawaharibia wazazi wenu mipango yao waliyokuwa nayo kwa kuwaleta chuoni.
Ingawa hakuweka wazi sababu ya kutoa onyo hilo kama Rais na mzazi, lakini katika miaka ya hivi karibuni, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimekuwa kikitumia siasa za ndani ya vyuo vikuu nchini, kuhamasisha vijana kujiunga na chama hicho.
Baada ya kupewa Shahada hiyo ya heshima, Rais Kikwete aliitunuku kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Watanzania wote wa Tanzania kwa kuunga mkono kwa dhati sera ya Serikali yake ya kuifanya elimu kuwa sekta kiongozi katika mgawo wa bajeti.
Mbali na Rais Kikwete, UDOM pia imemtunukia PhD mwanasiasa mkongwe wa Tanzania, Hayati Rashid Mfaume Kawawa ambaye alifariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.
Mpaka sasa UDOM ambacho ndio chuo kikuu kikubwa kuliko vyote nchini, kina eneo lenye nafasi ya kilometa za mraba 15,600, wanafunzi 20,000 kati ya wanafunzi 40,000 watasoma kwenye chuo hicho ujenzi utakapokamilika.
Rais Kikwete amerejea Dar es Salaam jana jioni kutoka Dodoma na leo atakuwa na shughuli ya kuapisha Baraza jipya la Mawaziri.
Source: Habari leo
Najiuliza: Hivi wakati hawa wanafunzi wa UDOM wanamtolea mchango (1 Million) wa kuchukua fomu za kugombea urais mbele ya kadamnasi mbona hakuwakatalia????????
AU IKIWA NI YEYE SAWA BUT WENGINE NONGWA???????
Na hili gazeti la habari leo halioni aibu kila kibaya kuhusisha na CHADEMA????????????
Imeandikwa na Mwandishi Maalumu, Dodoma; Tarehe: 27th November 2010 @ 07:20 Imesomwa na watu: 333; Jumla ya maoni: 0
RAIS Jakaya Kikwete, amewataka wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, kujiepusha kutumiwa na wanasiasa na badala yake kuelekeza nguvu zao katika masomo.
Alitoa kauli hiyo mkoani hapa jana katika mahafali ya kwanza ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na kuwaasa kuwa wanasiasa wanafanya hivyo kwa maslahi yao kwa kuwa walishamaliza masomo yao.
Kwa nyie mnaoendelea na masomo yenu, elekezeni nguvu zenu kwenye masomo. Hilo ndilo lililowaleta hapa. Msikubali kurubuniwa na wanasiasa. Hawa wanataka kuwatumia tu kwa manufaa yao kwa sababu masomo yao walikwishamaliza.
Ukijiingiza katika michezo hii ya siasa ni dhahiri utaharibikiwa. Ama utashindwa na kulazimika kurudia masomo ama utafukuzwa kabisa baada ya kushindwa kupata alama za kukuwezesha kuendelea mbele au hata kurudia mitihani, alisema Rais Kikwete ambaye pia alitunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima (PhD).
Aliwaasa wanafunzi hao kujishughulisha na jukumu lililowaleta chuoni hapo ambalo ni kusoma na wala siyo kushiriki siasa.
Msiwape nafasi wanasiasa kwa sababu watawaharibieni muda na malengo yenu. Mtawaharibia wazazi wenu mipango yao waliyokuwa nayo kwa kuwaleta chuoni.
Ingawa hakuweka wazi sababu ya kutoa onyo hilo kama Rais na mzazi, lakini katika miaka ya hivi karibuni, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimekuwa kikitumia siasa za ndani ya vyuo vikuu nchini, kuhamasisha vijana kujiunga na chama hicho.
Baada ya kupewa Shahada hiyo ya heshima, Rais Kikwete aliitunuku kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Watanzania wote wa Tanzania kwa kuunga mkono kwa dhati sera ya Serikali yake ya kuifanya elimu kuwa sekta kiongozi katika mgawo wa bajeti.
Mbali na Rais Kikwete, UDOM pia imemtunukia PhD mwanasiasa mkongwe wa Tanzania, Hayati Rashid Mfaume Kawawa ambaye alifariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.
Mpaka sasa UDOM ambacho ndio chuo kikuu kikubwa kuliko vyote nchini, kina eneo lenye nafasi ya kilometa za mraba 15,600, wanafunzi 20,000 kati ya wanafunzi 40,000 watasoma kwenye chuo hicho ujenzi utakapokamilika.
Rais Kikwete amerejea Dar es Salaam jana jioni kutoka Dodoma na leo atakuwa na shughuli ya kuapisha Baraza jipya la Mawaziri.
Source: Habari leo
Najiuliza: Hivi wakati hawa wanafunzi wa UDOM wanamtolea mchango (1 Million) wa kuchukua fomu za kugombea urais mbele ya kadamnasi mbona hakuwakatalia????????
AU IKIWA NI YEYE SAWA BUT WENGINE NONGWA???????
Na hili gazeti la habari leo halioni aibu kila kibaya kuhusisha na CHADEMA????????????