Mimi ni mtanzania na kwa haki yangu yakikatiba kama ilivy hainishwa ktk kifungu cha18 ninao uhuru wakutoa mawazo hata pasipo kumtusi mtu. Mh Rais wa jamuhur ya muungano wa Tanzania tumesikia meng sana kuhusu wewe na sasa kama sio kutuomba radhi njoo ktk hadhira ujitete! Mh Rais kuna usemi unasema ukiona mwenzako ananyolewa basi wewe tia maji, ila kuonyesha haitoshi kuna usemi mwingine unasema. Lisemwalo kama halipo basi lina kuja, mh Rais Bundi mweusi na sio mweupe anakulilia ukiwa umebakisha muda mfupi kustaafu. Nimekuwa nafuwatilia vile unaongoza nchi hii nakuona ukimya wako pindi kelele zavuma juu ya Jamuhuri hii basi kumekuwa ni stail yakuficha ukweli ama kuwahada watanzania upo makini. Well mimi ninalo taka nikusikia toka kwako ukikana wewe sio fisadi. Maana kama umefikia hatuwa yakununulia Suti na wafanyabiashara na watu wanatoa a real pics yakile wamekiona ina manisha dhiki zako ndizo zimekupeleka ikulu nasio dhiki za wa Tanzania. Asemaye juu ya jambo fulani basi uwenda ametumwa ama anao ukweli anataka kuusema hivyo huu ni mwanzo meng yatakuja uking'atuka ktk kiti. Napenda kukumbusha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa amekuwa akisikia kelele za Bundi mweupe baada ya kustaafu ila wewe utasikia kelele za Bundi mweusi hvyo ustaafu wako utajaa dhiki zakuojiwa najuwa hutoamini ila soma alama Za Nyakati Mubaraka wa Misri anasubiria kunyongwa ikiwa hukumu itapita! Je wewe ni nani? Mh Rais watanzania kwa pamoja twaitaji kusikia toba yako ama ujitetee na sio Rwemamu na ngonjera zake. Tunataka baba aonge nasio watoto. Aman yetu ni ya muhimu sana ila ktk hili aman itapotea. Asante.