Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,267
- 33,039
Kwa maelezo yako Hao askari wawili hawakumuuwa huyo Jenerali kombe kwa Makusudi kama ni hivyo Rais J.K . Ana haki ya kuwaachia huru ingawa Mahakama kuu ilitoa Adhabu ya kifo. Je Tuangalie Sheria yetu inasemaje je mtu akiuwa kwa bahati mbaya anaweza kuhukumiwa Adhabu ya Kifo? Na hata kama atahukumiwa na Mahakama Kuu adhabu ya kifo mwamuzi wa mwisho ni Rais ,Rais akitia saini ndipo anaweza huyo mtu kuuwawa Natanguliza hivyo asanteni...Rais Jakaya Kikwete amewaachia huru askari polisi wawili Koplo Juma Mswa na Konstebo Mataba Matiku waliokuwa wamehukumiwa adhabu ya kifo mwaka 1998 baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi Mkurugenzi wa zamani wa Usalama wa Taifa, Luteni Jenerali Imran Kombe. Wamekuwa gerezani takriban kwa miaka 16, wamechiwa huru kwa huruma ya Rais ambaye alipunguza adhabu hiyo ya kifo, kuwa kifungo cha miaka miwili jela.
Kombe aliuawa kwa kupigwa risasi nne kifuani Juni 30, 1996 baada ya polisi waliokuwa wakisaka gari aina ya Nissan Patrol mali ya W. Ladwa, kumfananisha na mtuhumiwa sugu wa wizi wa magari.
::Mwananchi::