Elections 2010 JK awa kinara wa kuvunja Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya mwaka 2010

Mchokonozi

Member
Nov 17, 2009
15
0
Aliposaini Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya mwaka 2010, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Mrisho Kikwete, hakutambua kwamba sheria hiyo ingerudi na kumhukumu kwa kuwa kinara wa kuivunja.

Akiwa kwenye kampeni zake alizoanzia Kanda ya Ziwa, kwenye mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza, JK ametoa ahadi kede kede ambazo zilijenga mazingira kuwashawishi wapiga kura kumchagua. Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, toleo Agosti 26, 2010, imeripotiwa kwamba alipokuwa mjini Katoro, Kikwete alilazimika kumtumia Waziri wa Nishati, William Ngeleja, kuwaelezea hatua ya Serikali iliyofikiwa kuhusu umeme kupelekwa kwenye mji huo, jambo ambalo linatafsiriwa kuwa ni "rushwa", kwani Ngeleja alilazimika kutoa ahadi kwamba umeme utaanza kuletwa mjini hapo kuanzia Januari 2011. Hili lilifanyika kwa lengo la kuwashawishi wananchi wa mji huo kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi, jambo ambalo limebainishwa kwenye Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 kuwa ni kosa, kwa mujibu wa sheria hiyo.

Ina maana kwamba, Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 INAKATAZA wagombea wa nafasi za kuchaguliwa, udiwani, ubunge na urais, kutoa ahadi kwa lengo la kuwashawishi wananchi kuwapigia kura. Kikwete amemtumia Ngeleja kutoa ahadi kwamba iwapo wananchi wataipigia kura, basi, miundombinu ya umeme itaanza kuwekwa mjini hapo na kwingineko karibu na hapo, kuanzia Januari 2011. HII NI RUSHWA!

Wewe mwananchi unayejiheshimu, unayeipenda nchi yako, una wajibu wa kutoipigia kura CCM kwa kuwa inatoa ahadi kushawishi kuchaguliwa. Haya tayari yamebainishwa kuwa ni makosa kisheria, na Tendwa anapaswa kumuengua mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa kuwa tayari ameivunja sheria aliyoisaini kwa mkono wake mwenyewe, akiwa Rais.

Iweje "rais", kiongozi wa nchi, awe wa kwanza kabisa kuvunja sheria aliyoiridhia mwenyewwe, tena kwa mbwembwe zote, kule Ikulu? Kumbe ulikuwa unafiki?

Atakayesema ya Ngoswe aachiwe Ngoswe ana lake jambo!

Tusitarajie utawala bora kwa mwendendo huu. Hakutakuwa na mabadiliko yoyote yale katika Awamu ya Tano!

Uongo uendelee!

--> Mchokonozi <--

Kura kwa Dk. Slaa TU!
 
Kikwete might have never done anything to be trusted so far, je hivi slaa angekua kwenye serikali kama presiding president, angekwepa ktumia rasilimali anazotumia JK?
 
Kikwete might have never done anything to be trusted so far, je hivi slaa angekua kwenye serikali kama presiding president, angekwepa ktumia rasilimali anazotumia JK?

Mpe nafasi uone kama atafanya au hatafanya!
 
Hata akivunja sheria Chief Justice kamteua yeye, IGP kamteua yeye, Magereza, PCCB nk. Tukubali tu tumepigwa mchanga wa macho
 
Kikwete might have never done anything to be trusted so far, je hivi slaa angekua kwenye serikali kama presiding president, angekwepa ktumia rasilimali anazotumia JK?

Suala ni whether ni sahihi au sio sahihi kutumia raslimali za walipakodi (majority of whom sio wana-CCM) kwa minajili ya kura.Naelewa logic ya swali lako lakini put it this way: as part of defence, mwizi amuulize hakimu angefanya nini if he were in their shoes!
 
Aliposaini Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya mwaka 2010, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Mrisho Kikwete, hakutambua kwamba sheria hiyo ingerudi na kumhukumu kwa kuwa kinara wa kuivunja.

Akiwa kwenye kampeni zake alizoanzia Kanda ya Ziwa, kwenye mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza, JK ametoa ahadi kede kede ambazo zilijenga mazingira kuwashawishi wapiga kura kumchagua. Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, toleo Agosti 26, 2010, imeripotiwa kwamba alipokuwa mjini Katoro, Kikwete alilazimika kumtumia Waziri wa Nishati, William Ngeleja, kuwaelezea hatua ya Serikali iliyofikiwa kuhusu umeme kupelekwa kwenye mji huo, jambo ambalo linatafsiriwa kuwa ni "rushwa", kwani Ngeleja alilazimika kutoa ahadi kwamba umeme utaanza kuletwa mjini hapo kuanzia Januari 2011. Hili lilifanyika kwa lengo la kuwashawishi wananchi wa mji huo kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi, jambo ambalo limebainishwa kwenye Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 kuwa ni kosa, kwa mujibu wa sheria hiyo.

Ina maana kwamba, Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 INAKATAZA wagombea wa nafasi za kuchaguliwa, udiwani, ubunge na urais, kutoa ahadi kwa lengo la kuwashawishi wananchi kuwapigia kura. Kikwete amemtumia Ngeleja kutoa ahadi kwamba iwapo wananchi wataipigia kura, basi, miundombinu ya umeme itaanza kuwekwa mjini hapo na kwingineko karibu na hapo, kuanzia Januari 2011. HII NI RUSHWA!

Wewe mwananchi unayejiheshimu, unayeipenda nchi yako, una wajibu wa kutoipigia kura CCM kwa kuwa inatoa ahadi kushawishi kuchaguliwa. Haya tayari yamebainishwa kuwa ni makosa kisheria, na Tendwa anapaswa kumuengua mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa kuwa tayari ameivunja sheria aliyoisaini kwa mkono wake mwenyewe, akiwa Rais.

Iweje "rais", kiongozi wa nchi, awe wa kwanza kabisa kuvunja sheria aliyoiridhia mwenyewwe, tena kwa mbwembwe zote, kule Ikulu? Kumbe ulikuwa unafiki?

Atakayesema ya Ngoswe aachiwe Ngoswe ana lake jambo!

Tusitarajie utawala bora kwa mwendendo huu. Hakutakuwa na mabadiliko yoyote yale katika Awamu ya Tano!

Uongo uendelee!

--> Mchokonozi <--

Kura kwa Dk. Slaa TU!

Jakaya kikwete hakutoa ahadi ili kuwashawishi wananchi wamchague tena, ila alikuwa anawaelezea wananchi mipango aliyokuwanayo ambayo anakusudia kuitekeleza endapo atapata tena fulsa ya kuongoza nchi. Hata nchi zilizoendelea kama USA, UK nk.wakati wa kampeni wagombea huelezea mikakati na mipango waliyonayo ambayo watatekeleza endapo watachaguliwa.Hivyo KIKWETE hajavunja sheria
 
Jakaya kikwete hakutoa ahadi ili kuwashawishi wananchi wamchague tena, ila alikuwa anawaelezea wananchi mipango aliyokuwanayo ambayo anakusudia kuitekeleza endapo atapata tena fulsa ya kuongoza nchi. Hata nchi zilizoendelea kama USA, UK nk.wakati wa kampeni wagombea huelezea mikakati na mipango waliyonayo ambayo watatekeleza endapo watachaguliwa.Hivyo KIKWETE hajavunja sheria

Wewe mbona unarukia jambo bila kulielewa...soma na huelewe kwanza kabla ya kuanza kuchangia...unaambiwa sheria aliyoiridhia mwenyewe yaani Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya mwaka 2010 inakataza vitendo vya kutoa ahadi na kujinadi kwa mtindo huo...wewe unaanza kuelezea habari za USA.Kwani wamarekani wakifanya lazima na Tanzania tufanye?Yaani mfano mzuri wa Demokrasia ndo huko Marekani?
 
Sheria ya uchaguzi ni mahususi kwa wapinzani na wasio kwenye mtandao tu
Huo ndiyo ukweli wenyewe na ambaye alitarajia kuwa Sheria ya Uchaguzi itawabana CCM ni kipofu. Kwa upande mwingine mimi naona kama CHADEMA wako passive sana. Kuna mambo mengi ambayo yanafanywa na CCM au vyombo vya dola kwa maslahi ya CCM ambavyo yanaweza kuwa-challenged mahakamani lakini hatuoni hatua yoyote inayochukuliwa. Kwa mfano pingamizi za CCM dhidi ya wagombea wa upinzani. Inaonekana kana kwamba pingamizi za CCM zikishakubaliwa inakuwa basi ndiyo mwisho. Matokeo yake CCM tayari ina magoli kibao hata kabla ya mechi kuanza. Kwani CHADEMA na vyama vingine hawana wanasheria wa ku-challenge pingamizi hizo? Wapi Tundu Lissu? Kuamini kuwa sheria hizi zinatungwa kwa ajili ya kutenda haki ni kujidanganya. Na kama CHADEMA wako tayari kucheza mchezo ambao wanajua matokeo yake toka mwanzo wanawakatisha tamaa watu wengi sana.
 
Back
Top Bottom