Mchokonozi
Member
- Nov 17, 2009
- 15
- 0
Aliposaini Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya mwaka 2010, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Mrisho Kikwete, hakutambua kwamba sheria hiyo ingerudi na kumhukumu kwa kuwa kinara wa kuivunja.
Akiwa kwenye kampeni zake alizoanzia Kanda ya Ziwa, kwenye mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza, JK ametoa ahadi kede kede ambazo zilijenga mazingira kuwashawishi wapiga kura kumchagua. Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, toleo Agosti 26, 2010, imeripotiwa kwamba alipokuwa mjini Katoro, Kikwete alilazimika kumtumia Waziri wa Nishati, William Ngeleja, kuwaelezea hatua ya Serikali iliyofikiwa kuhusu umeme kupelekwa kwenye mji huo, jambo ambalo linatafsiriwa kuwa ni "rushwa", kwani Ngeleja alilazimika kutoa ahadi kwamba umeme utaanza kuletwa mjini hapo kuanzia Januari 2011. Hili lilifanyika kwa lengo la kuwashawishi wananchi wa mji huo kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi, jambo ambalo limebainishwa kwenye Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 kuwa ni kosa, kwa mujibu wa sheria hiyo.
Ina maana kwamba, Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 INAKATAZA wagombea wa nafasi za kuchaguliwa, udiwani, ubunge na urais, kutoa ahadi kwa lengo la kuwashawishi wananchi kuwapigia kura. Kikwete amemtumia Ngeleja kutoa ahadi kwamba iwapo wananchi wataipigia kura, basi, miundombinu ya umeme itaanza kuwekwa mjini hapo na kwingineko karibu na hapo, kuanzia Januari 2011. HII NI RUSHWA!
Wewe mwananchi unayejiheshimu, unayeipenda nchi yako, una wajibu wa kutoipigia kura CCM kwa kuwa inatoa ahadi kushawishi kuchaguliwa. Haya tayari yamebainishwa kuwa ni makosa kisheria, na Tendwa anapaswa kumuengua mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa kuwa tayari ameivunja sheria aliyoisaini kwa mkono wake mwenyewe, akiwa Rais.
Iweje "rais", kiongozi wa nchi, awe wa kwanza kabisa kuvunja sheria aliyoiridhia mwenyewwe, tena kwa mbwembwe zote, kule Ikulu? Kumbe ulikuwa unafiki?
Atakayesema ya Ngoswe aachiwe Ngoswe ana lake jambo!
Tusitarajie utawala bora kwa mwendendo huu. Hakutakuwa na mabadiliko yoyote yale katika Awamu ya Tano!
Uongo uendelee!
--> Mchokonozi <--
Kura kwa Dk. Slaa TU!
Akiwa kwenye kampeni zake alizoanzia Kanda ya Ziwa, kwenye mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza, JK ametoa ahadi kede kede ambazo zilijenga mazingira kuwashawishi wapiga kura kumchagua. Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, toleo Agosti 26, 2010, imeripotiwa kwamba alipokuwa mjini Katoro, Kikwete alilazimika kumtumia Waziri wa Nishati, William Ngeleja, kuwaelezea hatua ya Serikali iliyofikiwa kuhusu umeme kupelekwa kwenye mji huo, jambo ambalo linatafsiriwa kuwa ni "rushwa", kwani Ngeleja alilazimika kutoa ahadi kwamba umeme utaanza kuletwa mjini hapo kuanzia Januari 2011. Hili lilifanyika kwa lengo la kuwashawishi wananchi wa mji huo kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi, jambo ambalo limebainishwa kwenye Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 kuwa ni kosa, kwa mujibu wa sheria hiyo.
Ina maana kwamba, Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi ya 2010 INAKATAZA wagombea wa nafasi za kuchaguliwa, udiwani, ubunge na urais, kutoa ahadi kwa lengo la kuwashawishi wananchi kuwapigia kura. Kikwete amemtumia Ngeleja kutoa ahadi kwamba iwapo wananchi wataipigia kura, basi, miundombinu ya umeme itaanza kuwekwa mjini hapo na kwingineko karibu na hapo, kuanzia Januari 2011. HII NI RUSHWA!
Wewe mwananchi unayejiheshimu, unayeipenda nchi yako, una wajibu wa kutoipigia kura CCM kwa kuwa inatoa ahadi kushawishi kuchaguliwa. Haya tayari yamebainishwa kuwa ni makosa kisheria, na Tendwa anapaswa kumuengua mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa kuwa tayari ameivunja sheria aliyoisaini kwa mkono wake mwenyewe, akiwa Rais.
Iweje "rais", kiongozi wa nchi, awe wa kwanza kabisa kuvunja sheria aliyoiridhia mwenyewwe, tena kwa mbwembwe zote, kule Ikulu? Kumbe ulikuwa unafiki?
Atakayesema ya Ngoswe aachiwe Ngoswe ana lake jambo!
Tusitarajie utawala bora kwa mwendendo huu. Hakutakuwa na mabadiliko yoyote yale katika Awamu ya Tano!
Uongo uendelee!
--> Mchokonozi <--
Kura kwa Dk. Slaa TU!