JK atua Dar apokewa na Maandamano ya wana CCM

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
JK atau Dar na kusema migogoro kama ya Kenya haiwezi kuwachukulia muda viongozi wa Au na badala yake wanajikita katia kuleta maendeleo ya Afrika. Kauli hii kidogo imeniacha hoi labda ningoje waandishi wenyewe waandike kesho . Uwanja ulikuwa kama kule CCM Dodoma .Ngoma na nyimbo za kumpamba. Kama kawaida hapa maneno ni CCM pekee . Wana CCM hata BOT na mashfa mengine ya wizi nk hawayajui wao ni matarumbeta na maguo ya kijani na njano .JK hakuchukua maswali na alipomaliza kusema makofi yakawa mengi na nikashindwa kujua makofi ni ya ninin. Mimi sasa naondoa laptop yangu naenda kupanda daladala kwenda mtoni kijichi nyumbani kwangu na yeye na msafara wake hao wanaondoka sasa wanaenda zao Ikulu kupongeza kwa kuukwaa Urais wa AU kama vile utatumalizia kashfa na kutuletea maendeleo kwa kasi ambayo tunaikata .
 
Thanks Lunyungu... unajua nini walio wengi huenda walichukuliwa kule vingunguti na Kipawa kisha kupewa Shs 2000 na nguo za kijani ilikuonyesha mapokezi ya kishindo......ukiwaambia hao hata Idd Amin aliishawahi kuwa mwenyekiti wa OAU hawawezi kuelewa ...kazi kweli kweli
 
Thanks Lunyungu... unajua nini walio wengi huenda walichukuliwa kule vingunguti na Kipawa kisha kupewa Shs na nguo za kijani ilikuonyesha mapokezi ya kishindo......ukiwaambia hao hata Idd Amin aliishawahi kuwa mwenyekiti wa OAU hawawezi kuelewa ...kazi kweli kweli

kikwete wa AU sio OAU watakucheka watu
 
Mwache abebe majukumu zaidi hata ulimwengu umjue alivyo msanii.CCM ni wagonjwa wa akili, kila mahali wao shuguli zote ni za chama tu..kijani na njano ndo rangi zao ya laana.
Yaliyofanyika Kenya ndio yafanyikayo hapa bongo kwa hiyo hana jipya zaidi ya kuyaona ya kawaida tu.

Ndio mkuu, hata Idd Amini aliwahi kuwa rais wa OAU! duh..
 
...JK, wewe weka shida chini na endelea ku-banjuka tuu, damu za watu hazipotei bure.
 
Mwache abebe majukumu zaidi hata ulimwengu umjue alivyo msanii.CCM ni wagonjwa wa akili, kila mahali wao shuguli zote ni za chama tu..kijani na njano ndo rangi zao ya laana.
Yaliyofanyika Kenya ndio yafanyikayo hapa bongo kwa hiyo hana jipya zaidi ya kuyaona ya kawaida tu.

Ndio mkuu, hata Idd Amini aliwahi kuwa rais wa OAU! duh..


Unajua nimejiuliza na bado najiuliza kwa nini viongozi wa CCM wanawatumia walalahoi kwa maslahi yao. Watawalipa na kuwaweka mitaani siku na kuwaimbisha sifa z Chama chetu lakini baada ya hapo wanaenda kufa kwa kukosa shilingi mia moja ya aspirini.Wanalala chini na kula chakula cha kuomba lakini wanasiasa wanaishia kwenye benz zao wanaenda Ikulu . Wana CCM wengi na hasa wapenzi wale wanao kuja kujaa airport kisa kumpongeza JK kuwa Prezido wa Au wana Ubongo ambao hauna akili . Wamekosa akili kabisa na sasa ndiyo matokeo .

Niltegemea watasimama na kumuuliza ndugu Rais wa Tanzania , Rais wa Nchi nzima , Rais wa Au, Mwenyekiti wa Chama Chetu ,Mkuu wa smiles , Mzee wa maneno mengi ambayo hayana tija , sasa leo umekuwa Rais wa Au lakini Tanzania bado wale wa madawa ya kulevya bado hatma yao au bado siku zao ? Vipi Bot kuwa na uchiunguzi double ? Vipi Spika kutufanya sisi sote wajinga ila ni yeye mwenye uwezo at least maswali haya ana majib yake maana mambo yote kwanza Chama then Nchi na yeye ndiye kwenye ufunguo wa Chama kwa sasa .Lakini hawakumuuliza nikagundua kwamba wana Ubongo bila akili sawa na Ngasongwa kuchukua cheti kule na kuwa mwana Falsafa lakini akaacha akili zote kwa profesa wake .
 
Ushirombo..acha dharau zako juu ya maeneo ya wanaokaa watu...ushawaona watu wa kipawa na Vingunguti wajinga sanaa na ww unaekaa masaki? kula kulala?Wale wake na watoto wa vigogo waliokuja airport nao wanakaa Kipawa na Vingunguti...

Lunyugu nae amesema kaenda na kaonesha anakaa wapi? Hizo Dharau ziache....kaa na ufikirie...
 
Thanks Lunyungu... unajua nini walio wengi huenda walichukuliwa kule vingunguti na Kipawa kisha kupewa Shs 2000 na nguo za kijani ilikuonyesha mapokezi ya kishindo......ukiwaambia hao hata Idd Amin aliishawahi kuwa mwenyekiti wa OAU hawawezi kuelewa ...kazi kweli kweli

Ushi wa rombo umenikumbusha mbali sana. Kwa kweli niliiona OAU kama ni kichekesho kikubwa walipoamua kumpa Nduli umwenyekiti wa umoja huo. Huyu naye wa kwetu ya ndani ya Tanzania yanamshinda huku atajikanyagakanyaga tu na hatimaye uwezo wake finyu kujulikana Afrika nzima na Ulimwengu pia.
 
Ushi wa rombo umenikumbusha mbali sana. Kwa kweli niliiona OAU kama ni kichekesho kikubwa walipoamua kumpa Nduli umwenyekiti wa umoja huo. Huyu naye wa kwetu ya ndani ya Tanzania yanamshinda huku atajikanyagakanyaga tu na hatimaye uwezo wake finyu kujulikana Afrika nzima na Ulimwengu pia.

Nadhani mpaka sasa dunia nzima inamjua uwezo wake...kuoata huo uenyekiti ni suala la protokali tu nionavyo...kwani alishindana na kina nani?
 
sasa sijui ndio kwa vile cuf wameandamana wakimpokea lipumba nao wamejibu mapigooo??

woooote vichwani kutupu hamna lolote ni katafuta umaaruf kwa migongo ya maskini tuu
 
n abt huyo mtalii kuwa rais wa Au..mwee Tanzania imemshinda ndio africa nzima sasa??yangu mie macho tuu ni hapo atakapotuabisha tu huko..
na sasa tungojee zianze trip za kwenda mabara mengine ku go jitambulisha..
 
Lunyungu mchango wako wa Awali umekinzana na mchango wa mwisho...Unasema wale waliofika pale hawana akili nawe ulifika pale vp?

Pia unawashambulia wafuasi eti wameshindwa kumuuliza JK, vipi wewe na Laptop yako ulifika pale kufanya nini? ulishindwa kuuliza au hukupewa nafasi? Jiulize kama wewe na utaalamu wako umeshindwa kuuliza sembuse mtu mwingine...ambae hata laptop hajui kitu gani...

Vp Airport na laptop wakati hakuna hotspot, au siku hizi ipo wireless pale...au mbwembe zako?
 
Kuna jambo gani la maana mpaka watu kuandamana hapo? I hope Watanzania tutajifunza mapema kwamba tunapoteza muda wetu kwenda kushinda airport kupokea viongozi.

Watu wangeandamana kupinga kuibiwa resources zetu, hapo ningeelwa, lakini tunaandama kuunga mkono mambo ya ushikaji na kuacha mambo ya maana.

Hiyo AU haina maana yoyote. Laiti viongozi wetu wangetumia muda wao vizuri kuleta maendeleo na kujenga haki kwenye nchi zao, hata hiyo migogoro inayotokea Afrika isingelikuwepo. Mpaka sasa JK hashindi nchini, sasa na jili cheo cha AU si ndio balaa kwa nchi?
 
Ushirombo..acha dharau zako juu ya maeneo ya wanaokaa watu...ushawaona watu wa kipawa na Vingunguti wajinga sanaa na ww unaekaa masaki? kula kulala?Wale wake na watoto wa vigogo waliokuja airport nao wanakaa Kipawa na Vingunguti...

Lunyugu nae amesema kaenda na kaonesha anakaa wapi? Hizo Dharau ziache....kaa na ufikirie...

Chuma mkuu nimekoseas wapi ? Kusema nina kaa mtoni Kijichi ama sijaelewa ? Hebu nisahihishe nijifunze Mkuu maana hakuna mkamilifu .
 
Ushirombo..acha dharau zako juu ya maeneo ya wanaokaa watu...ushawaona watu wa kipawa na Vingunguti wajinga sanaa na ww unaekaa masaki? kula kulala?Wale wake na watoto wa vigogo waliokuja airport nao wanakaa Kipawa na Vingunguti...

Chuma

I think your out of the context... sijaonyesha dharau hapo, kama unaelewa lugha za picha wala usingekuwa na shaka... hiyo Kipawa na vingunguti nina maana wasisiem kama kawaida yao huchukua watu wa karibu na haswa wale wasio na shughuli za maana....huwezi mshawishi mtu mwenye kazi yake aiache kisa 2000 ama tshirt za kijani zenye nembo ya jembe na nyundo kwenda uwanjani......nafikiri Chuma kabla hujacomment kitu soma na uelewe...maana hii inaweza kukuletea shida katika kuelewa simple logics... Chuma wewe nadhani unaleta dharau....sikai Masaki wala mimi si kula kulala kama wewe...kata issue hapa JF si lazima ukubalieane na mawazo yangu pia Chuma

Ushi wa Rombo
 
...JK, wewe weka shida chini na endelea ku-banjuka tuu, damu za watu hazipotei bure.

Kuna kijana mwanamuziki wa Kenya ana muziki una shairi kama hilo! Anasema "Life ni fupi na mi sijivungi, naweka shida chini natupa mikono juu, bah bah banjuka tu......Sisi tuna shida zetu tusikize zako kwa nini?" Labda JK kaupenda huu mstari kama mtangulizi wake Mkapa alivyuopenda ule wa "Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe" hadi wakauweka kwenye ilani ya uchaguzi. Natabiri hii ilani ya "Maisha bora kwa kila mtanzania" itakapochuja (mwaka kesho tu), tutaletewa hii ya "Banjuka tu"!
 
Sidhani kama alipokelewa na wanaccm bali watanzania ambao wamefurahishwa na heshima tuliopewa ya rais wetu kuwa mwenyekiti wa AU.JK nikama nabii ambaye wachache wenye akili ya mgando wanawaza kwa nini amepewa uchair lakini wenzetu wanatambua ubora wake.
 
Sidhani kama alipokelewa na wanaccm bali watanzania ambao wamefurahishwa na heshima tuliopewa ya rais wetu kuwa mwenyekiti wa AU.JK nikama nabii ambaye wachache wenye akili ya mgando wanawaza kwa nini amepewa uchair lakini wenzetu wanatambua ubora wake.


Fisadi vipi na huyo aliyemaliza muda wake ? Alikuwa bora kuliko wote ? Vipi hao walio tangulia walikuwa bora kuliko sisi ? Ubora upi wa JK unao uongelea hapa ? N aubaya upi wa marais wenzake ambao JK kauvuka na yeye kuwa bora ? Walitumia vigezo vipi vya Ubora kumpata JK ?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom