tembeleh2
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 765
- 165
Source:blogu ya michuzi.
Taarifa ya ikulu kwa vyombo vya habari inasema kwamba, Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania jana (29/2/2012) ametoa mwaliko kwa wadau mbali mbali kuwasilisha majina ya watu ambao wadau hao wanawapendekeza kuwamo katika tume ya kuratibu na kukusanya maoni kuhusu katiba mpya.
Wadau waliopatiwa mwaliko huo kupitia gazeti la serikali no.66 la ijumaa iliyopita (24/2/2012) ni pamoja na vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, jumuia za kidini, asasi za kiraia na pamoja na jumuiya,taasisi pamoja na makundi mengine yenye malengo yanayofanana.Mwaliko huo vile vile utatangazwa kwenye magazeti ya kawaida. Mwisho wa kupokea majina hayo ni machi 16,2012.
Taarifa ya ikulu kwa vyombo vya habari inasema kwamba, Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania jana (29/2/2012) ametoa mwaliko kwa wadau mbali mbali kuwasilisha majina ya watu ambao wadau hao wanawapendekeza kuwamo katika tume ya kuratibu na kukusanya maoni kuhusu katiba mpya.
Wadau waliopatiwa mwaliko huo kupitia gazeti la serikali no.66 la ijumaa iliyopita (24/2/2012) ni pamoja na vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, jumuia za kidini, asasi za kiraia na pamoja na jumuiya,taasisi pamoja na makundi mengine yenye malengo yanayofanana.Mwaliko huo vile vile utatangazwa kwenye magazeti ya kawaida. Mwisho wa kupokea majina hayo ni machi 16,2012.