JK atoa miezi sita CCM kutafuta sababu za kushindwa

Facts1

JF-Expert Member
Dec 23, 2009
307
28
Monday, 06 December 2010 08:45 Fredy Azzah

MWENYEKITI wa CCM, Jakaya Kikwete amewataka wanachama na viongozi wa chama hicho katika ngazi zote, kuaangalia kwa makini mambo ambayo yalisababisha chama hicho kushindwa kwenye baadhi ya maeneo katika uchaguzi mkuu uliopita.

Kikwete ambaye ni rais wa Jamhuri Muungano Tanzania, alisema hayo juzi jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na Jumuiya wa Wanawake wa chama hicho (UWT) Biafra wilayani Kinondoni.

“Shabaha yetu ni kuimarisha yale tuliyofanya vizuri, tufanye tathmini hii mapema ndani ya miezi hii mitatu au sita iwe imekamilika, tufanye tathimini katika ngazi zote, tukikamilisha tutajua wapi tumekosea wapi tumefanya vizuri, kwenye uchaguzi mkuu ujao tutaingia tukiwa na uhakika,” alisema Kikwete ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Kikwete ambaye alitoa hotuba fupi, aliwataka pia viongozi wa jumuiya hiyo, kuhakikisha wanawashawishi vijana na wasomi kujiunga katika jumuiya hiyo ili kuzidi kukiimarisha chama hicho.

Alisema juhudi za wanawake ndizo zilizokisaidia chama hicho kuibuka na ushindi, huku akiwaelezea kuwa walikuwa wakijitokeza kwa wingi katika mikutano ya kampeni pamoja na siku ya kupiga kura.

“Mnaotakiwa kupongezwa leo (juzi) ni nyie.., kupitia nyie hata wanaume na vijana walikipigia kura Chama Cha Mapinduzi,” alisema Kikwete.

Alisema serikali yake itaendelea kutoa nafasi za juu kwa wanawake, ili kutimiza lengo la usawa kitu ambacho alieleza kuwa ni sera ya CCM.
Kikwete alisema serikali yake itaendelea kuzitafutia ufumbuzi mila mbalimbali ambazo zinazowagandamiza wanawake na watoto.

Alifafanua kwamba, sambamba na hilo tume ya kurekebisha sheria inaendelea kupitia na kurekebisha sheria mbalimbali zinazogandamiza wanawake na watoto.

Awali, Mwenyekiti wa UWT mkoani Dar es Salaam, Zarina Madabida, alimtaka Rais Kikwete kutomfumbia macho kiongozi yeyote atakayekwamisha utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2010/15.

Alimtaka kuendelea kutoa mikopo ya fedha “mabilioni ya JK” na kumuomba ahakikishe kuwa masharti ya kuombea fedha hizo yanapunguzwa.

“Yale mabilioni yalitusaidia sana na tunaendelea kuunda vikundi ili kujikwamua, tunaomba uendelee kuzitoa hizo fedha lakini utusaidie ili mashariti yake yapunguzwe,” alisema Madabida.

Wakati huo huo, Rais Kikwete aliwakumbusha kuwa ukomo wa nafasi ya ubunge wa viti maalumu kupitia CCM utakuwa ni miaka 10 na kwamba baada ya kipindi hicho wabunge ambao watahitaji kurudi bungeni watalazimika kugombea kwenye majimbo,
“Tunataka viti maalumu iwe ni sehemu ya kujifua, baada ya vipindi viwili itabidi muende majimboni mkapambane,” alisema

Alisema CCM imeamua utaratibu huo ili kuondoa dhana ya wanawake kubebwa na pia kupunguza malalamiko katika uteuzi wa viti hivyo.

“Mambo ya kusema huyu kapendelewa yataisha, lakini muongeze ushirikiano na umoja, wanawake mkishikana hakuna mwanaume atakayewaweza, kwenye uchaguzi wa mwaka huu tumeona mmewatoa wanaume jasho kweli, ile dhana ya kuwa ukigombea na mwanamke unaona umepata mteremko sasa haipo,” aliongeza Kikwete.
 
Monday, 06 December 2010 08:45 Fredy Azzah

MWENYEKITI wa CCM, Jakaya Kikwete amewataka wanachama na viongozi wa chama hicho katika ngazi zote, kuaangalia kwa makini mambo ambayo yalisababisha chama hicho kushindwa kwenye baadhi ya maeneo katika uchaguzi mkuu uliopita.

Kikwete ambaye ni rais wa Jamhuri Muungano Tanzania, alisema hayo juzi jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na Jumuiya wa Wanawake wa chama hicho (UWT) Biafra wilayani Kinondoni.

"Shabaha yetu ni kuimarisha yale tuliyofanya vizuri, tufanye tathmini hii mapema ndani ya miezi hii mitatu au sita iwe imekamilika, tufanye tathimini katika ngazi zote, tukikamilisha tutajua wapi tumekosea wapi tumefanya vizuri, kwenye uchaguzi mkuu ujao tutaingia tukiwa na uhakika," alisema Kikwete ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Kikwete ambaye alitoa hotuba fupi, aliwataka pia viongozi wa jumuiya hiyo, kuhakikisha wanawashawishi vijana na wasomi kujiunga katika jumuiya hiyo ili kuzidi kukiimarisha chama hicho.

Alisema juhudi za wanawake ndizo zilizokisaidia chama hicho kuibuka na ushindi, huku akiwaelezea kuwa walikuwa wakijitokeza kwa wingi katika mikutano ya kampeni pamoja na siku ya kupiga kura.

"Mnaotakiwa kupongezwa leo (juzi) ni nyie.., kupitia nyie hata wanaume na vijana walikipigia kura Chama Cha Mapinduzi," alisema Kikwete.

Alisema serikali yake itaendelea kutoa nafasi za juu kwa wanawake, ili kutimiza lengo la usawa kitu ambacho alieleza kuwa ni sera ya CCM.
Kikwete alisema serikali yake itaendelea kuzitafutia ufumbuzi mila mbalimbali ambazo zinazowagandamiza wanawake na watoto.

Alifafanua kwamba, sambamba na hilo tume ya kurekebisha sheria inaendelea kupitia na kurekebisha sheria mbalimbali zinazogandamiza wanawake na watoto.

Awali, Mwenyekiti wa UWT mkoani Dar es Salaam, Zarina Madabida, alimtaka Rais Kikwete kutomfumbia macho kiongozi yeyote atakayekwamisha utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2010/15.

Alimtaka kuendelea kutoa mikopo ya fedha "mabilioni ya JK" na kumuomba ahakikishe kuwa masharti ya kuombea fedha hizo yanapunguzwa.

"Yale mabilioni yalitusaidia sana na tunaendelea kuunda vikundi ili kujikwamua, tunaomba uendelee kuzitoa hizo fedha lakini utusaidie ili mashariti yake yapunguzwe," alisema Madabida.

Wakati huo huo, Rais Kikwete aliwakumbusha kuwa ukomo wa nafasi ya ubunge wa viti maalumu kupitia CCM utakuwa ni miaka 10 na kwamba baada ya kipindi hicho wabunge ambao watahitaji kurudi bungeni watalazimika kugombea kwenye majimbo,
"Tunataka viti maalumu iwe ni sehemu ya kujifua, baada ya vipindi viwili itabidi muende majimboni mkapambane," alisema

Alisema CCM imeamua utaratibu huo ili kuondoa dhana ya wanawake kubebwa na pia kupunguza malalamiko katika uteuzi wa viti hivyo.

"Mambo ya kusema huyu kapendelewa yataisha, lakini muongeze ushirikiano na umoja, wanawake mkishikana hakuna mwanaume atakayewaweza, kwenye uchaguzi wa mwaka huu tumeona mmewatoa wanaume jasho kweli, ile dhana ya kuwa ukigombea na mwanamke unaona umepata mteremko sasa haipo," aliongeza Kikwete.
Kwanza sababu za kushindwa vibaya anajua wala haihitaji utafiti. Ni kupoteza muda na kuleta majungu tu!
Pili amesahau yaliyompata yule mama wa Arusha mjini? Ngoja awadanganye watapigwa na kuisha!
 
Ya nini kutafuta kuandikia mate wakati wino upo?????? CCM is 50 years old- sehemu kubwa ya population ya Tanzania (over 90%) ya wapiga kura ni umri takriban miaka 18 mpaka 45!!!!!! Hawa jamaa hawajui CCM na wala hawaitaki kwa sababu over 90% imejaa maneno matupu-hakuna kitu!!! Mwaka 2005 watanzania milioni 11 walikuwa masikini; mwaka 2010 (miaka mitano tu baadaye) masikini wako milioni 12!!!!! Sehemu kubwa ya population hii ni waelewa-wanajua 2015 masikini watakuwa milioni 13!!!!! Na hawa ndiyo waathirika wakuu wa sera na ufisadi wa CCM!!!!! Kwa hiyo ni wale wazee tu waliokuwepo miaka ya 1970 wakati CCM inazaliwa ndiyo wamebaki kuwa wanachama wa CCM!!!! Kikwete asilazimishe mambo, watanzania hawamtaki ingawa ametumia katiba mfu kujitwalia madaraka ya laana!!!!! wamemchoka kama walivyoichoka CCM!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kazi nzuri CCM.
Tathmini ni muhimu. CCM tukifanya tathmini ya kina, ya kisayansi na ya kijasiri, mwaka 2015 asilimia 80 ya viti vilivyokwenda upinzani Tanzania Bara vitarudi CCM. Hata CHADEMA wangefanya tathmini ya kweli kujua kwanini Slaa hakushinda au angalau hawakupata wabunge zaidi ya 80 wa majimbo kama walivyojigamba awali ingewasaidia. Bahati mbaya tathmini yao inaishia kwenye wimbo wa CCM wamechakachua kura! Tathmini ya aina hii itawapeleka kaburi la kisiasa mwaka 2015. Mimi siwapendi Chadema lakini nawapa tu ushauri wa bure.
 
YAANI rAIS MZIMA HAJUI KWA NINI WANANCHI WALIMPIGA CHINI? HADI AKALAZIMISHA KUINGIA MADARAKANI
 
Mmmhhh, ama kweli!!!! Wahenga husema siku zote MWIZI WAKO ataonekana MSTARI wa mbele sana kuonekana kukusaidia kukitafuta kitu kilekile ambacho moyoni mwake ANAJUA FIKA kwamba aliekikwapua si mwingine bali ni yeye yeye.

Haishangazi sana kusikia TAATHMINI kufanyika, anyway!!!!
 
Mmmhhh, ama kweli!!!! Wahenga husema siku zote MWIZI WAKO ataonekana MSTARI wa mbele sana kuonekana kukusaidia kukitafuta kitu kilekile ambacho moyoni mwake ANAJUA FIKA kwamba aliekikwapua si mwingine bali ni yeye yeye.

Haishangazi sana kusikia TAATHMINI kufanyika, anyway!!!!

Hatoe pia miezi sita kwa ajili ya kutafuta mmiliki wa DOWANS
 
Bila Mahakama ya kimataifa ICC kutuambia kwamba wenye DOWANS ni Rostam Aziz, Edward Lowasa, Ridhiwani Kikwete, Lau Masha, William Ngeleja na wengine au hapana, HAKUNA RUKSA TANESCO kutumia kodi zetu kufanya biashara KICHA na baadhi yetu Wa-Tanzania ambao sasa wamepata wendawazimu na UFISADI wote huu wa kutisha.

Wa-Tanzania, lazima tufikirie sana juu ya hili kwa sababu FEDHA ZINAZOTUMIKA kutuhonga KANGA, VITENGE, PILAU na Mikopo yenye masharti nafuu mara nyingi hukwapuliwa kupitia TANESCO na mikataba mingine mingi INAYOTIWA UBOVU kwa maslahi ya kutuibia kutoka hazina yetu ya taifa.

Siku zote ukisikia TANESCO mitambo chakavu au hiki au kile kimekua vipi basi moja kwa moja ujue maandalizi yako njiani kwa wale wafanyabiashara fulani ambao huchangia sana CCM kwenye chaguzi zake kurudisha gharama zao kwa kuingiza nchini MIJENERETA KIBAO kwa jina la kuokoa taifa na giza. Mmmhhh, misheni town kila kona!!!
 
Utafiti hafanyika kwa kitu kisicho julikana ili kijulikanee kupitia utafiti huo. Ama kufanya utafiti kwa kitu ambacho kiko wazi ni upotevu wa resources ambazo zingeweza kutumika kwa tafiti zingine
 
Kazi nzuri CCM.
swahiba

binafsi naona ni kitu cha kusikitisha sana kusikia maneno haya kutoka kwa mwenyekiti wa chama... hii inaeonyesha mawili... either hakijui chama chake au hawajui wananchi wake

Any ruling system has a very good internal control yenye kipimajoto independent lakini ndani ya chma na pia hutumia intelligence information kuwa na sababu... INAONEKANA HAVIPO AU HAVITUMIWI

KIBAYA ZAIDI NI HIZI BLANKET ASSIGNMENT KWENYE PUBLIC, WHERE IS THE ACCOUNTABILITY?
 
Kumbe hata yeye anajua alishindwa tuende nao taratibu mwisho watatoboa siri.

Ndugu Kwinini, nakubaliana na wewe kabisaaaaaaaaaaaaaaa!! Ni kwamba tu tulikua hajaelewa ujumbe uliofichama nyuma ya kauli ya mwenzetu huyu. Ni kweli kwamba kwa hicho alichokisema, Wa-Tanzania hatuhitaji kutafsiriwa zaidi maana yake. Mmmmhhhhh!!!

Kipindi si kirefu huenda wakaweanza wenyewe kwa wenyewe kuweka mambo hadharani zaidi. Time will tell!!!!
 
Kwa msaada tu sababu ya kwanza ni yeye mwenyewe - kudanganywa kila kukicha, kuanguka ovyo majukwaani, kusafiri bila mpango, kukumbatia mafisadi, kutokufanya maamuzi magumu, kuleta utani kwenye masuala ya msingi mfano kuwaletea wajawazito Bajaji kwa ajili ya kuwakimbiza labour room, na la mwisho wizi wa kura!!!!
 
'm not suprised at all. Si alishawahi sema hajui kwanin Tz ni maskin? Tatizo ni upeo mdogo wa kuelewa
 
Monday, 06 December 2010 08:45 Fredy Azzah

MWENYEKITI wa CCM, Jakaya Kikwete amewataka wanachama na viongozi wa chama hicho katika ngazi zote, kuaangalia kwa makini mambo ambayo yalisababisha chama hicho kushindwa kwenye baadhi ya maeneo katika uchaguzi mkuu uliopita..............

“Shabaha yetu ni kuimarisha yale tuliyofanya vizuri, tufanye tathmini hii mapema ndani ya miezi hii mitatu au sita iwe imekamilika, tufanye tathimini katika ngazi zote, tukikamilisha tutajua wapi tumekosea wapi tumefanya vizuri, kwenye uchaguzi mkuu ujao tutaingia tukiwa na uhakika,” alisema Kikwete ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano/

Anachotaka kujua ni kwanini walishindwa kuchakachua kwenye hayo maeneo. Wakishabainisha hizo sababu basi wazipatie ufumbuzi. Waje na mbinu mpya za kuwawezesha kuchakachua kwenye uchaguzi ujao. Kumbuka motto ya ccm ni USHINDI NI LAZIMA.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom