JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

Hivi wachumi wanaomzunguka ****** pale magogoni wana kazi gan? Dah bora BEN kuliko huyu mtu...hata kiberiti kushusha bei hawawezi kweli?????????????:A S 13::A S 13:
 
Walisimamishe bunge lisikae mda wa miaka 2 bila malipo, harafu fedha hizo ziingizwe sokoni. Hakuna wanachofanya wabunge hata bunge lisipokuwapo. Wabunge ni wezi na wizi uliopitishwa kisheria.
 
Hivi ule mradi wa kukataa mashangingi wa WM Pinda umeishia wapi?


Pinda akatae mashangingi, hivi wewe unamfahamu vizuri Pinda!?, ukimuona wawezafikiri ni mtoto wa mkulima sivyo ndugu yangu.

fanyia uchunguzi habari hii hapa chini, sijachunguza ila kama ni kweli nimesikitishwa nae sana!, tena nasisitiza kama ni kweli Waziri Mkuu hakuwatendea haki majirani zake ambao ni maskini na umeme wanausikia tu!

Kama angekuwa mtoto wa mkulima na mpenda watz angekubali mpango wa kuwekewa umeme kwenye shamba lake kule mikwambe Kigamboni kwa milioni 300 na hivyo mradi ule ungesaidia hata wananchi wengine, ila yeye aliukataa mradi huu kuwa ni gharama na kuamua kununua generator ya milion 200 ( atatumia yeye tu, Fikiria mafuta ya huu mtambo kwa siku) pia kaangalie jinsi katapiller inavyochonga barabara ya kwenda huko shamba kila mwezi!
 
Kila siku huwa nasema kwamba viongozi wa hii nchi wapo madarakani kwa ajili ya maslahi yao na familia zao na sio maslahi ya wananchi ambao wanatoa kodi zao......inasikitisha sana kwa kweli kuona watu wanavujisha pesa bila mpango wowote inatia huruma sana tena sana.....yaani inaonekana sasa jinsi JK alivyokuwa na upeo mdogo wa kufikiria kwenye madaraka yake.......
 
siku zote alikuwa wapi mpaka maji yamefika mdomoni ndio anaamkaa? kila miezi sita taarifa ya hali ya kiuchumi hutolewa na bank kuu, waziri wa fedha yupo nae mara kwa mara wakipata kikombe cha ghahawa, washauri wa kiuchumi anao kwenye ofisi yake binafsi etc etc lakini taaarifa hazipati za hali ilivyo
 
mfumuko wa bei unaweza kupunguzwa kwa kuongeza vyanza vya uzalishaji wa chakula, kuwepo kwa miundo mbinu mizuri, kuongeza ushindani wa kibiashara, mamlaka zinazo simamia biashara iwe tra, trading standards , fair competition na uslama wa taifa wafanye kazi zao kwa uadilifu
 
Nafikiri angekaa na jopo la washauri wake wa uchumi waone tatizo liko wapi kabla ya kutoa hili agizo kwa kutumia akili yake iliyo fupi kama mkia wa mbuzi akisaidiwa na Rijizi one na mkewe................!!!
 
Hivi huyu JK anaishi dunia gani. Kila kitu kwake ni kipya na anabaki kushangaa pasipo majibu. Hakuna tatizo hata moja ambalo ameweza kusimama na kutoa ufumbuzi wake. Anapozungumzia kupanda kwa bei ya vyakula halafu anasema fungueni maghala ambayo yamejaa mahindi pekee anamaanisha nini. Hivi anafikiri kwa kujaza mahindi kwenye soko ndiyo bei ya vyakula itapungua? Waliacha wajanja wachache wakaficha sukari kwa lengo la kupandisha bei lakini Serikali ilishindwa kufanya lolote. Sukari iliyokuwa inauzwa kati ya sh. 1400-1500 sasa inauzwa kwa sh. 1700-2000 kwa kilo. Mafuta ya kupikia lt 5 yalikuwa yanauzwa kati ya sh 14,000-16,000 kwa sasa mafuta hayo yanauzwa kati ya sh. 19,000-20,000. Kwa hali hii Mtanzania atawezaje kuyamudu maisha ilhal ongezeko hilo ni kwa kila kitu hadi nauli za daladala. Watu wakihoji Rais anasema wanataka kuangusha Serikali, anapoulizwa anabaki kushangaa na kipato cha Mtanzania kinazidi kuporomoka,

Tufanye nini katika hali kama hii ama ndiyo kiama kwa wanyonge kinatimia?


Mimi kweli namshangaa sana Rais wangu,
Kwanza hizi staili za kupitia wizara aliyemshauri kampotosha Rais. Hayo anayoyashangaa hadharani alipaswa kuyajua mapema. Siyo mbele ya Kamera. Hii staili imepitwa na wakati. Kwani yeye ndiye anajua sana kuliko JK Nyerere, mwinyi na Mkapa ambao hawakufanya hivyo?
Mfumuko wa bei haushuki kwa staili hiyo.Uchumi wa wapi huo?. Heri mimi ambaye sijawahi kumpigia kura.
 
hapana...unaposhusha kodi bei hupungua na watu hufanya manunuzi zaidi....kutokana na unafuu wa bei...watu watanunua zaidi(in terms of volumes) na wigo wa kodi kupanda....simple economics...kwa vile vat sio production cost
kwa bongo wananufaika hawazidi laki

teh list is the same, manji, rostam, mengi, el, mahoteli ya kitalii, kokakola, na makampuni ambayo main account ziko nje ya nchi

hizo kodi kwenye daily life sisi wa chini mchango wetu ni chini mno, ukiondoa paye

to me paye would have helped majority directly and indirectly
 
Makubwa haya. Kinachofuata ni uchapishaji wa hela nyingi pindi atakapopita wizara ya fedha na kuambiwa hali ya maisha ni ngumu na pato la mwanchi liko chini sana. Hahahahaaaa......i am so embarased to have a president like this!!!!?????!!!!!:embarassed2:
 
Sasa anapoamrisha kutoa chakula cha akiba, njaa ikija itakuwaje?? Wakati huo huo nasikia mvua mwaka huu si za kutosha hivyo mvuno hayategemewi kuwa mazuri!!
 
Mchakachuaji,
Rais wetu mgonjwa halafu unaweka heading hiyo. Umetushtua kidogo. Maagizo/ Ushauri wake huo una walakini. Haoni kutokuwa na kodi kwenye mafuta ya taa kunavyochangia uchakachuaji kwenye mafuta mengine?
Hallo WildCard unanokosea kusema mgonjwa,sema alikuwa mgonjwa!!! lakini baada ya kupata kikombe kwa Babu ameshapona.
 
Usalama wa Taifa walipaswa kuna na wataalamu wa kuthibiti mfumuko wa bei, kwani umfumuko wa bei unachangia kukosekana na usalama. Hii ni Hatari ya kuwa na Cocktail ya waagizaji wa bidhaa Nchini (importers), wanauwezo wa kukaa meza moja na kupanga kupandisha bei za bidhaa, lakini kama kungelikuwa na kitengo cha kudhibiti mfumuko wa bei hali isingekuwa hivi ilivyo. Kulitakiwa kuwe na mfumo wa kibiashara unaothibiwa usalama wa nchi, yaani kutafuta, kununua, kuingiza bidhaa muhimu kama mafuta, nafaka, sukari n.k na kuziuza kwa bei poa ilikulazimisha kushusha bei. Kwa mfano TPDC, na Mashirika ya Umma, yakiongozwa na Usalama wa taifa kwa kificho au wazi wakatumia pesa za serikali kuagiza bidhaa na kuuza kwa bei poa wafanyabiashara nao watashusha. Sio sahihi kwa serikali kujitoa kufanyabiashara, asali zake ni hizi...
you wrote sense mr/ms. Thank you important contribution. michango mingine ni yakivuvuvuvuvuzela tu. Hope they will lern from you. Tkanks again.
 
huyu nae jk akili zake fupi..yaani yeye anaona leo kupanda kwa gharama za maisha, wakati wenye akili waliliona hili mwaka mmoja tu tangu aupate urais(2006), licha ya CDM kumkumbusha lakini wapi....duh nimeamini jamaa alikuwa kwenye usingizi mzito, naona kaamshwa baada ya lile agizo la uingereza kwamba apunguze safari za nje....muheshiwa karibu nyumbani!!
 
hapa ndipo huwa nasema kuwa huyu jamaa sio kiongoz mzuri .......na haya mambo ya kipuuzi ndo unakuta mtu kama anthony lusekelo anapaza sauti na kusema rasi huyu ni mzuri...mara hivi mara vile....

ajabu kweli....nilishasema we have a president who cannot think beyond the next meal.
 
Usalama wa Taifa walipaswa kuna na wataalamu wa kuthibiti mfumuko wa bei, kwani umfumuko wa bei unachangia kukosekana na usalama. Hii ni Hatari ya kuwa na Cocktail ya waagizaji wa bidhaa Nchini (importers), wanauwezo wa kukaa meza moja na kupanga kupandisha bei za bidhaa, lakini kama kungelikuwa na kitengo cha kudhibiti mfumuko wa bei hali isingekuwa hivi ilivyo. Kulitakiwa kuwe na mfumo wa kibiashara unaothibiwa usalama wa nchi, yaani kutafuta, kununua, kuingiza bidhaa muhimu kama mafuta, nafaka, sukari n.k na kuziuza kwa bei poa ilikulazimisha kushusha bei. Kwa mfano TPDC, na Mashirika ya Umma, yakiongozwa na Usalama wa taifa kwa kificho au wazi wakatumia pesa za serikali kuagiza bidhaa na kuuza kwa bei poa wafanyabiashara nao watashusha. Sio sahihi kwa serikali kujitoa kufanyabiashara, asali zake ni hizi...

usalama wa taifa wengi wao ni wezi wakiongozwa na kim mgaya.......hawa wakipewa rungu hilo nakwambia utakuwal nyasi kaka.....wamejikita katika biashara haram na za kipuuzi kuliko maelezo......ushauri ni kuwa tulipaswa kuwa na mamlaka ya kuthibiti mfumko wa bei. lakini ukiwapa hawa watu wa ikulu sijui usalama wa taifa....nakwambia tutakaanga hata nzi tule wacha kabisa wale hawafai kamanda

 
hapo ndipo tunapoona upeo wake mdogo wa kufikiri.yeye anadhani tu kuingiza chakula cha akiba ndio kutapunguza mfumuko wa bei.kuna factors nyingi sana zinachangia,mfano bei ya mafuta.mfumuko wa bei unachangiwa zaidi na bei ya mafuta.akiweza kudhibiti bei ya mafuta,mfumuko na utapungua.lakini kwa sababu hana hata idea hizi,basi tujue tu inakula kwetu kwa sana tu mpaka 2015.inatia huruma kuwa na kiongozi ambaye ana mawazo duni kama huyu wa sasa.

naona aibu kusema sana kwani jana nimelisemea sana hili. Naamini itafi8ka wakati ataagiza pesa zichapishwe nyingi ili kuondoa umaskini tanzania na kuwafurahisha wananchi wasiichukie serikali. Tufunge na kuomba wakati tunaisubiria 2015. Mungu ibariki tanzania mungu tubariki walala hoi tunaoendeshwa au kuvutwa kama mkokoteni. Wakulima wameletewa vi-tractor vinaitwa power tilla (sijui spelling zake) ambazo zinatoa moshi kwa mbele na kuingia puani kwa anayelisukuma moja kwa moja. Baada ya miaka mitano wote watakufa kwa tb. Hiyo ndiyo sera ya kilimo kwanza au kuua kwanza?
 
Hamna dogo anataka kuwaleteeni nafuu kelele kwa saaannnnnnnnnnnnnnnnnnnnna au hamumwamini,haya tungoje kushuka kwa hiyo bei yaa unga iwe ya kuridhisha basi
 
Back
Top Bottom