Elections 2010 JK aongoza matokeo ya awali

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,314
33,108

Monday, 01 November 2010 16:14

Salim Said
matokeoawali.jpg
Matokeo ya awali

MATOKEO ya awali katika nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanaonyesha kuwa, mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete anaongoza kwa asilimia 64 ya kura zilizotangazwa dhidi ya asilimia 25 za Dk Willibrod Slaa wa Chadema.

Kikwete ameshinda katika majimbo ya Babati Mjini mkoani Manyara, Korogwe Mjini Tanga, Nkenge Kagera, Singida Mjini, Mafia Pwani na Tarime mkoani Mara huku Dk Slaa akishinda katika baadhi ya majimbo ya Kanda ya Ziwa.

Mgombea wa CUF profesa Ibrahim Lipumba anashikilia nafasi ya tatu kwa kupata asilimia nane na Peter Mziray akiambulia asilimia moja.

Wagombea wengine wote waliobaki wanashikilia nafasi ya mwisho kwa kupata asilimia 0.0 ya kura zilizohesabiwa na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Hata hivyo kazi ya kukusanya, kujumlisha na kutangaza matokeo inaendelea.

Tafadhali endelea kufuatilia hapa.

chanzo: Gazeti la Mwananchi
 

Monday, 01 November 2010 16:14

Salim Said
matokeoawali.jpg
Matokeo ya awali

MATOKEO ya awali katika nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanaonyesha kuwa, mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete anaongoza kwa asilimia 64 ya kura zilizotangazwa dhidi ya asilimia 25 za Dk Willibrod Slaa wa Chadema.

Kikwete ameshinda katika majimbo ya Babati Mjini mkoani Manyara, Korogwe Mjini Tanga, Nkenge Kagera, Singida Mjini, Mafia Pwani na Tarime mkoani Mara huku Dk Slaa akishinda katika baadhi ya majimbo ya Kanda ya Ziwa.

Mgombea wa CUF profesa Ibrahim Lipumba anashikilia nafasi ya tatu kwa kupata asilimia nane na Peter Mziray akiambulia asilimia moja.

Wagombea wengine wote waliobaki wanashikilia nafasi ya mwisho kwa kupata asilimia 0.0 ya kura zilizohesabiwa na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Hata hivyo kazi ya kukusanya, kujumlisha na kutangaza matokeo inaendelea.

Tafadhali endelea kufuatilia hapa.

chanzo: Gazeti la Mwananchi

Hongera za awali Mheshimiwa Kikwete, Mungu akupe umri mrefu uendelee kutuongoza kwa busara na hekima kama kipindi kilichopita. Tumeona Zanzibar, kwa mara ya kwanza tumeshuhudia, chini ya uongozi na busara zako, kura zimeenda vizuri na hakuna vurugu wala fujo na Maalim Seif kakubali matokeo mara tu baada ya kura kutangazwa. Ahsante Kikwete
 
Msianze kupeana hongera mapema. kwa taarifa yenu, bado tunatafakari matokeo ya urais yalivyopatikana. kwa haraka haraka tu inaonekana kuna uwizi mkubwa sana wa kura za urais uliofanywa. ngojeni tu tutaona kitakachoendelea. rais mpenda mafisadi, nusu ya muda wake anashinda nje ya nchi na ambaye chini ya uongozi wake maisha yameendelea kuwa magumu zaidi, hawezi kuchaguliwa kwa kura nyingi kiasi hicho. lazima kuna namna hapa. watanzania wa leo siyo wa jana. lazima matokeo ya urais yatazamwe na kupitiwa kwa umakini mkubwa sana.
 
Hayo matokeo ya Raisi yana walakin, kuna mapungufu kibao yalionekana katika baadhi ya vituo, mfano unakuta karatasi za kujaza matokeo ya raisi hazipo (Fomu 21A), ati zimesahaulika. Sikupata logic ya kuwa na fomu za kujaza matokeo ya Diwani na Mbunge bila kuwepo kwa matokeo ya Raisi. Hayo matokeo ililazimu kujazwa kweny photocopy na si original form, sijui hizo original zilipelekwa wapi na kwa nia gani.
 
Back
Top Bottom