Shoo Gap
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 246
- 71
Shirikisho la michezo ya Idara za serikali, wizara na ofisi za wakuu wa mikoa(SHIMIWI) limetangaza kusitishwa kwa michezo hiyo iliyokuwa ifanyike Tanga 17th September -2nd October.
Wadadisi wa mambo wanasema maandalizi yote yalishakamilika na fedha zilishatengwa, lakini jana ghafla yametangazwa kusitishwa, hivyo hakutakuwepo na mashindano hayo mwaka huu. "Wanaogopa mkusanyiko mkubwa kama huu wa wafanyakazi toka idara zote za serikali na mikoa yote huenda ukatumiwa na TUCTA kuendelea kumwaga 'sumu' kwa wafanyakazi, ili wasimpe kura aliyezikataa" alisikika mfanyakazi mmoja akisema.
Serikali itakuwa imepata hasara kubwa kwa kusitisha mashindano haya kwani, idara karibu zote walishafanya booking za hoteli na kulipia advance, baadhi ya idara zilishafanya manunuzi ya vifaa vya michezo, na gharama kubwa ilishatumika kufanya maandalizi kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja.
HII SIO DALILI NZURI HATA KIDOGO.
Wadadisi wa mambo wanasema maandalizi yote yalishakamilika na fedha zilishatengwa, lakini jana ghafla yametangazwa kusitishwa, hivyo hakutakuwepo na mashindano hayo mwaka huu. "Wanaogopa mkusanyiko mkubwa kama huu wa wafanyakazi toka idara zote za serikali na mikoa yote huenda ukatumiwa na TUCTA kuendelea kumwaga 'sumu' kwa wafanyakazi, ili wasimpe kura aliyezikataa" alisikika mfanyakazi mmoja akisema.
Serikali itakuwa imepata hasara kubwa kwa kusitisha mashindano haya kwani, idara karibu zote walishafanya booking za hoteli na kulipia advance, baadhi ya idara zilishafanya manunuzi ya vifaa vya michezo, na gharama kubwa ilishatumika kufanya maandalizi kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja.
HII SIO DALILI NZURI HATA KIDOGO.