Kwa kweli mambo yanayofanywa na Kikwete na CCM yake yanazidi kunichefua sana. Nakumbuka huyu JK kupitia kinana walisema hawawezi kushiriki midahalo kwa sababu ya ratiba yao imejaa mpaka siku ya mwisho wa kampeni. Mashabiki wa CCM walishangilia kama kawaida yao. Huyu huyu jamaa tumeona akijialika kwenye sherehe ya walimu, na sasa eti mgeni rasmi kwenye mechi ya TZ and Moroco, Je, muda umepatikana wapi. Je, kipi bora kati ya hayo na kufanyiwa 'interview' na watazania ambao unawaomba kazi tena kwa nguvu kubwa?. JK kuna uovu mkubwa sana ambao hataki uanikwe wakati wa mdahalo.Kama alivyosema mwezangu katika thread yake inakuwaje unaomba kazi, mwajiri anakwambia nikufanyie interview wewe unakataa! Kama watanzania tungekuwa serious hii nadhani ni sababu tosha yakumnyima kura. Lakini CCM inaona kila Mtanzania ni mjinga, ni mtu wa kudanganywa na kudanganyika! WATANZANIA TUSIKUBARI UPUMBAVU HUU WA KUDANGANYWA KAMA WATOTO WADOGO.