JK amuapisha IGP MPYA

Kibo10

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,277
8,837
Rais Kikwete amemuapisha Mkuu mpya wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna, Ernest Mangu muda mfupi uliopita, aahidi kupunguza changamoto za uhalifu.
 
attachment.php
 
Namkumbusha tu kufanya uchunguzi huru wa kifo cha Ally Zona, muuza magazeti aliyeuwawa pale Msamvu Morogoro na kitu chenye ncha kali...

Haya kubambikizia kesi wananchi, rushwa iliyokithiri, kushindwa kufanya upelelezi, kupeana vyeo kindugu nk hataweza kuyamudu maana na yeye amekulia kwenye mfumo huo huo. Unless anakuja mtu mpya kutoka nje ya jeshi hakuna kitakachobadilika
 
Hiyo siyo breaking news tena!!

Wewe upo kwenye tukio la kuteuliwa leo ameapishwa rasimi ili aanze kazi 1kuteuliwa ni breaking news pia kuapishwa ni tukio jingine ni breaking news pia umeelewa mkuu
 
Ameahidi kupunguza changamoto za Uhalifu badala ya kuzimaliza?
 
Alikuwa mkurugenzi wa uchunguzi wa makosa ya jinai so alikuwa chini ya Mwema ndani ya system ile ile hivyo sitegemei mabadiliko yoyote ya kiutendaji katika jeshi hili. Aniprove wrong tu
 
Namkumbusha tu kufanya uchunguzi huru wa kifo cha Ally Zona, muuza magazeti aliyeuwawa pale Msamvu Morogoro na kitu chenye ncha kali...

Haya kubambikizia kesi wananchi, rushwa iliyokithiri, kushindwa kufanya upelelezi, kupeana vyeo kindugu nk hataweza kuyamudu maana na yeye amekulia kwenye mfumo huo huo. Unless anakuja mtu mpya kutoka nje ya jeshi hakuna kitakachobadilika
Kero kubwa kuliko zote ni Tabia ya kuwabambikia watu kesi za Bunduki au kuwawekea Bangi unga Mafuvu ya Watu nk hii kero akithubutu kuitokomeza na wale Askari wote waliofanya Unyama huu washitakiwe kijeshi na kuwajibishwa ataonekana amekuja kivingine na kulisafirisha jeshi la Polisi kinyume na hapo Jeshi la polisi litaendelea kulalamikiwa juu ya kuwabambikia watu kesi.
 
Back
Top Bottom