Kero kubwa kuliko zote ni Tabia ya kuwabambikia watu kesi za Bunduki au kuwawekea Bangi unga Mafuvu ya Watu nk hii kero akithubutu kuitokomeza na wale Askari wote waliofanya Unyama huu washitakiwe kijeshi na kuwajibishwa ataonekana amekuja kivingine na kulisafirisha jeshi la Polisi kinyume na hapo Jeshi la polisi litaendelea kulalamikiwa juu ya kuwabambikia watu kesi.Namkumbusha tu kufanya uchunguzi huru wa kifo cha Ally Zona, muuza magazeti aliyeuwawa pale Msamvu Morogoro na kitu chenye ncha kali...
Haya kubambikizia kesi wananchi, rushwa iliyokithiri, kushindwa kufanya upelelezi, kupeana vyeo kindugu nk hataweza kuyamudu maana na yeye amekulia kwenye mfumo huo huo. Unless anakuja mtu mpya kutoka nje ya jeshi hakuna kitakachobadilika